Mfalme Ogu wa Bashani: Mnefili pekee aliyepona kwenye Gharika la Nuhu

Mfalme Ogu wa Bashani: Mnefili pekee aliyepona kwenye Gharika la Nuhu

jimmykb197. Mkuu nifafanulie hapa

4 Nao Wanefili walikuwako duniani siku zile;tena ,baada ya hayo ,wana wa Mungu walipoingia kwa binti za binadamu,wakazaa nao wana;hao ndiyo waliokuwa watu hodari zamani ,watu wenye sifa.
Mwanzo 6 :4
Wana wa Mungu ni wale wacha Mungu wanaotenda mapenzi Ya Mungu katika maisha yao.

Ukisoma Waebrania unaona wazi mwandishi anasema hakuna malaika yeyote ambaye Mungu amemwita mwanaye ila amewafanya malaika kuwa miale ya moto.
Lakini mcha Mungu anaitwa mwana Wa Mungu kwa mujibu wa Biblia. Zaburi 2:7, Matendo 13:33, Waebrania 1:5.

Kwa hiyo kama wana Wa Mungu waliwaona wana wa wanadamu ni wazuri na kujichukulia yeyote na kisha kuzaa nao maana yake walifanya kwa matakwa yao wenyewe na wala si kwa mwongozo Wa Mungu.

Zingatia kwamba mahusiano kati ya wana Wa Mungu na wana wa wanadamu Mungu hakupendezwa nayo na ndiyo maana unaona kizazi hiki cha wanefili kimekuja wakati uovu umezidi sana duniani kiasi kwamba miaka ya mbeleni baada ya haya majitu yaliyotokana na mahusiano yaliyolaaniwa kuzidi katika uovu kuliko hata wazazi wao, Mungu akaamua kuuangamiza ulimwengu wote, ndipo Nuhu na jamaa yake ya karibu sana wakapona maangamizi hayo.

Haya majitu yalikuwa hodari na mashuhuri kwa wakati ule sababu yalikuwa na nguvu, na pia hii ilikuwa ni ishara ya wazi hakikuwa kizazi cha kawaida, mbaya zaidi walitegemea nguvu zao na si kumtegemea Mungu, hivyo walikuwa mbali sana na mapenzi ya Mungu na kuona walijitosheleza sababu ya uwezo waliokuwa nao. Nadhani umepata chochote japo kidogo.
 
naomba kujuzwa kuwa hao Wana Wa Mungu ndio malaika. Ushahidi wowote wa kimaandiko?
Binafsi sijaona sehemu inayo hakikisha kwamba wana Wa Mungu ndiyo malaika, ila ukisoma kisa hiki kupitia kitabu (Biblia ya Roman Catholic) huwa ina maelezo ya ziada kwa chini yanayotoa ufafanuzi zaidi ili kumwelewesha mambo ya ziada msomaji. Hapo ndipo utakuta neno lililoandikwa "Wana wa Mungu au malaika Wa Bwana"
Ila ukisoma katika hali ya ufunuo unaona wazi wana Wa Mungu wakati mwingine ndiyo hao hao wanaitwa mahali pengine malaika Wa Bwana. Kwa sababu hapa wana wa Mungu tafsiri ingine inakuja kuwa ni miungu.

Kwa hiyo kwa ushauri wangu tu jitahidi sana kuushirikisha zaidi ufahamu wako ili upate kuelewa baadhi ya mambo mengine, maana kwa akili tu ya kawaida kuna wakati akili inakataa kabisa kupokea kwa sababu ni mambo yanayohusiana sana na roho.
 
Kitu ninachokijua kwa sehemu ndogo tu kwa uelewa wangu mdogo ni kwamba, Mungu akitaka kufanya jambo lake hashindwi kulifanya, huyo mnefili aliyesalia kwa kufikiri fikiri tu yaweza kuwa alikuwa mimba wakati wa gharika labda.
Kinyume na hapo yaliyobakia yote ni vigumu kukubaliana nayo kwa sababu tangu mvua kunyesha mpaka maji kuanza angalau kupungua ni zaidi ya mwaka! Sasa huyo ni kiumbe gani mwenye mwili ambaye hali wala kunywa kwa mwaka mzima kwenye dharuba nzito namna hiyo?!!!
mvua ilinyesha siku 40 tu watu waliteketea ndani ya siku hizo,hizo habari za mwaka umezipata wapi mkuu,kukaa siku 40 bila kula inawezekana hata yesu alifanya hivyo
 
kuna movie fulani niliiona kuwa kuna tetemeko litaikumba dunia, volcano na aina zote za natural disaster.. halafu kuna jamaa alikua anahubiri kwisha kwa dunia watu wakawa hawamwelewi....

mwisho wa siku yakatokea kweli na huyo star wa hio movie.. atapewa ramani na huyo jamaa ambayo inaonesha mahala ambapo hapatakumbwa na hayo matatizo...

wakati huo madon wa dunia washatengeneza manyambizi ambazo zina kila huduma ndani yake.. ya kukimbilia kiama.. mwisho wa siku zile nyambizi baada ya kupata misuko suko siku nyingi zitafika South Africa Good hope.. Kwa maana kuwa Africa haitazama.


Hata sikuelewaga maana yake.
Na jina lake silijui wakuu nadhani wengi wetu tumeionaga
2012
 
mvua ilinyesha siku 40 tu watu waliteketea ndani ya siku hizo,hizo habari za mwaka umezipata wapi mkuu,kukaa siku 40 bila kula inawezekana hata yesu alifanya hivyo
Ni kweli gharika ilikadumu kwa siku 40, lakini maji yalipata nguvu kwa siku 150! Basi soma hiyo Mwanzo sura ya nane yote utapata muda na idadi kamili ambayo maji yalikaa katika uso wa nchi.
 
majini
Halafu msipende kuwafananisha malaika na majini jaman ni viumbe wawili tofauti kabisa jaman majini ni kama sisi tu wanadam baadhi ya sifa zao na zetu zinafanana
hawajaumbwa na udongo inakuaje wawe kama wewe au unamaanisha nini
 
mvua ilinyesha siku 40 tu watu waliteketea ndani ya siku hizo,hizo habari za mwaka umezipata wapi mkuu,kukaa siku 40 bila kula inawezekana hata yesu alifanya hivyo
Ukisoma Mwanzo 7:21-24, utaona hakuna kitu kilichosalia chenye mwili kilichokuwa nje ya safina mkuu. Mungu huwa habahatishi hata
 
Nauliza tu wakati huyo mnefili kajishikiza nuhu akupewa taarifa na Mungu
Mwanzo 8:1-.....
Inasema nuhu alituma njiwa akaangalie Hali ya hewa nje kwanini asingemwambia huyo mnefili aliyejishikiza kwenye hiyo sarina aangalie Hali ya hewa na amjulishe
Na ukisema hakujua kuwa kuna huyo mtu kwanini alichukua njiwa na sio kumuuliza Mungu juu ya Hali ya hewa huko nje au sijakuelewa?
 
Kingine huyo musa alimchoma na mkuki may ambaye ni mkubwaaa kana kwamba musa alionekana kama panzi je kwa skill yako panzi anawezakukuchoma na mkuki ukafa?
Namaanisha kama Mimi mwanadamu nina saizi ya panzi kimwonekano hata mkuki wangu ni sawa nakijiti cha unyasi hakuna ukweli hapo
 
Kingine huyo musa alimchoma na mkuki may ambaye ni mkubwaaa kana kwamba musa alionekana kama panzi je kwa skill yako panzi anawezakukuchoma na mkuki ukafa?
Namaanisha kama Mimi mwanadamu nina saizi ya panzi kimwonekano hata mkuki wangu ni sawa nakijiti cha unyasi hakuna ukweli hapo
Hapa mwandishi anajitahidi kuelezea namna wale wapelelezi kwa namna walivyoingiwa na hofu na fedheha ndani mwao, ndiyo walivyojiona wao nafsi zao mbele ya yale majitu, hii ilikuwa ni fikra tu ya wale wapelelezi na ndiyo maana baada ya kwenda kutoa taarifa hiyo mbaya kwa wenzo, Mungu aliwakasirikia akawaapia hawataingia katika nchi ile kwa sababu waliwavunja wenzao moyo hata wakamkosea Mungu. Na wale waliowatia moyo wenzao ambao ni Joshua na Kalebu, wao waliingia katika ile nchi na wakamiliki sehemu ya urithi wao
 
Hapa mwandishi anajitahidi kuelezea namna wale wapelelezi kwa namna walivyoingiwa na hofu na fedheha ndani mwao, ndiyo walivyojiona wao nafsi zao mbele ya yale majitu, hii ilikuwa ni fikra tu ya wale wapelelezi na ndiyo maana baada ya kwenda kutoa taarifa hiyo mbaya kwa wenzo, Mungu aliwakasirikia akawaapia hawataingia katika nchi ile kwa sababu waliwavunja wenzao moyo hata wakamkosea Mungu. Na wale waliowatia moyo wenzao ambao ni Joshua na Kalebu, wao waliingia katika ile nchi na wakamiliki sehemu ya urithi wao
Umesoma story ya jamaa jamaa kasema waisrael walikuwa kwenye mahema na wakati huo Huyu ogu akainua mlima kuwaponda bahati mbaya nusu ilimwangukia akaja musa akamchoma alafu anaonyesha Hamas alikuwa mkubwa mno sasa huo mkuki si ungekuwa kama kijiti
 
Mungu alikua na haja gan
Hii nadharia umesema ndiyo yenye mashiko,sijaelewa ina mashiko kwa nani,kama ni kwako ni sawa...

Kwangu mimi nadharia hii naiona haina mashiko kabisa mkuu.Nasema hivi kwasababu zifuatazo..

1;Suala la yeye "kupewa kazi ya kuiangalia safina ili isigngane na mawe"ni nadharia ya kuchekesha sana maana unataka kumfanya Mungu kama asiyejiweza na kuelewa alilokuwa anafanya.Kwanza ni mawe gani hayo? Maana maji yalifunika milima yote,kuna jiwe kubwa zaidi ya mlima Kilimanjaro kwa mfano?Lakini unapaswa tu uelewe kwamba suala zima la gharika ni suala lilisimamiwa na Mungu,sijuwi kama unaelewa ni nini maana ya Mungu kwa ujumla wake.....

2;Unadaio kuwa "kwa akili ya kawaida dunia nzima izame halafu wewe pekee uwe kwenye boti,hivi waliokufa watakuacha kweli?",yaani hiki nacho ni kichekesho kingine mkuu. Kwanza safina siyo boti,pili safina ilijengwa kwa namna ya ajabu na kwa maelekezo ya Mungu mwenyewe unadhani unaweza ivunja? Kwa kutumia nini? Halafu ukiwa kwenye maji huku ukipigania uhai wako? Are you serious?

Mungu aliwajuwa hao majitu vizuri sana na kwakuwa yeye aliisimamia "shoo"haya unayofikiria ni kama kitu cha kuchekesha sana kwake...

Hii nadharia yako haina mashiko kabisa hata kiduchu....

Hii nadharia inajaribu kuelezea namna kizazi cha Wanefili kilivyokuja kupatikana baadaye,baada ya gharika.Inawezekana au isiwezekane ukizingatia sababu kuu ya gharika ni hao hao Wanefili na sidhani kama Mungu angeruhusu ikawa hivi japokuwa inaweza ikawezekana pia...

Hii nadhara nayo haifai kabisa.Hii nadharia inataka kumfanya Mungu asiwe Mungu kabisa maana kama tu mtu anaweza kupanda kwenye mlima halafu Mungu atake kumuua na ishindikane kwasababu kapanda kwenye mlima huyo siyo Mungu ni kitu kingine kabisa...

Inawezekana lakini swali kubwa ni namna ilivyowezekana....

Wanefili wa kabla ya gharika walifikia futi 30 hivyo huyu OGu unayemsema hapa sijaona uajabu wake.Ninachokielewa ni kwamba Wanefili wa baada ya gharika walikuwa na urefu wa futi 10 hadi 18 hivyo walikuwa wadogo kiumbo kuliko wale wa kipindi kile cha kabla ya gharika....

Majengo ya kustaajabisha hayapatikani mashariki ya kati pekee mkuu,yapo dunia nzima kuanzia Puma Punku kule Bolivia hadi Urusi mpaka kwenye kisiwa cha Sardinia kule Italy ambapo baadhi ya watafiti wanasema kwamba inawezekana ilikuwa ni moja ya ground Zero ya Wanefili wa kabla yagharika maana walishafukua mabaki makubwa sana ya hawa Wanefili.Moja ya fuvu lililowashangaza ni lile ambalo waliweza kuingiza kwenye eye socket ylile fuvu,ule upanga refu wenye makali kila upande,upanga maarufu wa vitani na ulizama wote na ulipogota kisogoni sehemu pekee iliyobakia nje ni ile sehemu ya kushikia tu...

Unaweza tu kufikiria lilikuwa ni fuvu kubwa kwa kiwango gani...

Mabaki ya majitu haya yenye urefu wa zaidi ya futi 25 yamefukuliwa maeneo mengi sana America ya kusini,kaskazini,Africa,Ulaya na Asia hivyo huyo unayemsema hakuwa peke yake labda baada ya gharika kama ulivyoelezea hapo juu kwasababu baada ya gharika Wanefili walikuwa wadogo kiumbo...[/QUO
najiuliza hivi kwanini Mungu ajisumbue kuleta gharika mpaka safina ijengwe ili kuwaua hao watu wakati angeweza kutamka tu wote wafe na wakafariki
 
Ukisoma Mwanzo 7:21-24, utaona hakuna kitu kilichosalia chenye mwili kilichokuwa nje ya safina mkuu. Mungu huwa habahatishi hata
Mkuu soma kitabu cha kumbukumbu na joshua.... Mungu aliapa kuwamaliza wacanaan wote na alisema joshua asiwaonee huruma ila mwisho wa siku mbona Mungu aliwaacha wagibeoni hadi mfalme suleiman alipowaua baadhi yao Mungu alileta ukame mkubwa israel

Mungu ana makusudi na kila jambo huenda alimuacha kwa makusudi yake kama ambavyo aliangusha ukuta wa yeriko ila alimuacha RAHAB pekee
 
Umesoma story ya jamaa jamaa kasema waisrael walikuwa kwenye mahema na wakati huo Huyu ogu akainua mlima kuwaponda bahati mbaya nusu ilimwangukia akaja musa akamchoma alafu anaonyesha Hamas alikuwa mkubwa mno sasa huo mkuki si ungekuwa kama kijiti
Ukisoma vitabu vya wayahudi utakuta mkuki pekee ulikuwa na futi 12 na kilichomuua sio mkuki pekee bali pia vipande vya mawe makubwa vilivyotokana na mlima kupasuka katikati alipokuwa anajaribu kuubeba
 
Mkuu soma kitabu cha kumbukumbu na joshua.... Mungu aliapa kuwamaliza wacanaan wote na alisema joshua asiwaonee huruma ila mwisho wa siku mbona Mungu aliwaacha wagibeoni hadi mfalme suleiman alipowaua baadhi yao Mungu alileta ukame mkubwa israel

Mungu ana makusudi na kila jambo huenda alimuacha kwa makusudi yake kama ambavyo aliangusha ukuta wa yeriko ila alimuacha RAHAB pekee
2Samwali 21:2, Wagibeoni ni kabila inayotokana na Waamori, ambao hapo awali walipaswa na wao wauwawe wote kama wengineo, lakini wao walipoona Waisrael wana nguvu wakaamua kufanya ujanja na hivyo waisrael wakawa apia wagibeoni kwamba hawatawauwa, basi kwa kuwa waliwaapia pasipo kutafuta kusudi la Mungu, Mungu aliwaacha na baadaye wakagundua kumbe hawa walikuwa wenyeji wa nchi ile! Basi wakaamua kuwapa kazi ngumu na kuchanja kuni nk, hivyo wakaachwa hai kwa makubaliano hayo ndiyo maana wakaishi miongoni mwa waisrael.

Kwa kuwa wazee wa kiIsrael waliwaapia wazee wa waamori, Mungu husimamia agano, hivyo Sauli alipowauwa kwa sababu ya faida ya Waisrael Mungu akakumbuka kile kiapo cha miaka hiyo! Ndiyo akaleta adhabu kwa Israeli iliyosababishwa na kosa la mfalme Sauli.

Na kisa cha Rahabu kipo wazi, naye aliapiwa usalama wake na waisrael kwa vile aliwaficha wasionekane na askari wenyeji wa nchi. Nadhani umeelewa
 
Canopy theory mkuu inaelezea ivo na bado tafiti zinafanywa kuipa nguvu zaidi

Na kuna nyingine inaelezea kuhusu kukutwa kwa mali kale za baharini juu ya milima huko Caucasus ambayo imewabakiza na maswali kivp maji ya baharini yafike juu ya mlima hadi yaache mabaki ya vitu vya baharini na sio caucasus tu ila milima karibu kila bara ina hiyo tendency je bado haiwezi kueleza uwepo wa gharika kuu
Canopy theory is just a conspiracy, no scientific study has ever backed it!
Hakuna maji ya kutosha huko juu kuweza kunyesha na kufunika uso wadunia!
 
Wana wa Mungu ni wale wacha Mungu wanaotenda mapenzi Ya Mungu katika maisha yao.

Ukisoma Waebrania unaona wazi mwandishi anasema hakuna malaika yeyote ambaye Mungu amemwita mwanaye ila amewafanya malaika kuwa miale ya moto.
Lakini mcha Mungu anaitwa mwana Wa Mungu kwa mujibu wa Biblia. Zaburi 2:7, Matendo 13:33, Waebrania 1:5.

Kwa hiyo kama wana Wa Mungu waliwaona wana wa wanadamu ni wazuri na kujichukulia yeyote na kisha kuzaa nao maana yake walifanya kwa matakwa yao wenyewe na wala si kwa mwongozo Wa Mungu.

Zingatia kwamba mahusiano kati ya wana Wa Mungu na wana wa wanadamu Mungu hakupendezwa nayo na ndiyo maana unaona kizazi hiki cha wanefili kimekuja wakati uovu umezidi sana duniani kiasi kwamba miaka ya mbeleni baada ya haya majitu yaliyotokana na mahusiano yaliyolaaniwa kuzidi katika uovu kuliko hata wazazi wao, Mungu akaamua kuuangamiza ulimwengu wote, ndipo Nuhu na jamaa yake ya karibu sana wakapona maangamizi hayo.

Haya majitu yalikuwa hodari na mashuhuri kwa wakati ule sababu yalikuwa na nguvu, na pia hii ilikuwa ni ishara ya wazi hakikuwa kizazi cha kawaida, mbaya zaidi walitegemea nguvu zao na si kumtegemea Mungu, hivyo walikuwa mbali sana na mapenzi ya Mungu na kuona walijitosheleza sababu ya uwezo waliokuwa nao. Nadhani umepata chochote japo kidogo.
Je wewe ni mwana wa Mungu? Na je ukioa wana wa binadamu utazaa wanefili?, au siku hizi duniani tumebaki wana wa Mungu tu? Na je kama tumebaki wana wa Mungu(kwa sifa za wana wa Mungu kibiblia) hukumu ya kazi gani?
 
Back
Top Bottom