Mfanyakazi usithubutu kuacha kazi kwa kushawishiwa kwa njia yoyote ile

Mfanyakazi usithubutu kuacha kazi kwa kushawishiwa kwa njia yoyote ile

Eti kuna wale wanaacha kazi na kujiunga na network marketing kama D9 (kama wanavyodai), hii ni kweli?
 
Yaaap cryptocurrency ni kila siku boss but not other pairs ambazo ni only 5 days
But crypto ni kwa baadhi ya brokers tu
Ni kweli mkuu cyrpo ni 24/7, Nilijua jamaa anamaanisha pairs nyingine.
 
Kuna watu wameibuka siku hizi, wanajiita Inspirational Or motivational speakers, hawa wanakula sana hela za vijana kwa semina za ujanja ujanja wakihamasisha vijana wajiajiri wakati wao wameajiriwa.
yaani hao ndiyo sitaki hata kuwasikia
 
Habari wanajukwaa!

Uzi huu ni maalumu kwa ajili ya waajiriwa wa serikali na wale wa sekta binafsi. Pia unawahusu wale watakaoajiriwa siku za machoni.

Kuna upuuzi siku hizi unasambazwa sana na watu mbalimbali unaohusu kupondea ajira(kuajiriwa) na kutukuza kujiajiri.

Katika haya maisha kila mtu ana mpango kazi wake kichwani wa kumwezesha kufika mahali pale anapopahitaji, ili kufika mahali unapopalenga unahitaji ushauri kwa sehemu ndogo sana.

Kwanini niseme ushauri unahitajika kwa sehemu ndogo sana?

1. Wewe ndiwe mwenye picha halisi ya kule uendako na utakako

2. Watu wengi hawawezi kubeba mzigo wa mwingine kama mzigo wao. Watu wamejawa wivu (hasa ngozi nyeusi)

3. Watu wanaishi kwa maigizo, mfano humu ndani mtu utakuta amekosa ajira na sasa anasajili line kwa mwezi anaingiza laki mbili tu ila ukiomba ushauri yeye atajiintroduce kama mmiliki wa kampuni na hana mpango wa kuajiriwa tena maishani mwake.

Unaweza kujiajiri ukiwa mwajiriwa na kuzikabili changamoto nyingi kwa urahisi zaidi ya yule asiyeajiriwa. Kivipi?
(A) Ni rahisi kupata mtaji
(B) Ni rahisi kukuza mtaji wako pindi unapoona biashara yako ina soko zuri
(C) Unaweza kuwageuza wafanyakazi wenzako kuwa kama soko la awali huku ukisoma somo la biashara kwa vitendo

Note:
Usiache kazi mpaka pale utakapoona biashara yako inaweza kuendelea kukuingizia fedha hata kama unaumwa ,hapa namanisha mpaka pale itakapojiendesha yenyewe. Uwe jela, uwe umelazwa n.k system iwe inaoperate, kinyume na hapo usithubutu.

Pia napenda kusema kuwa mafanikio ni pale moyo wa mtu unaporidhika na vile alivyo na si kumiliki magorofa au kampuni. Mwingine hata kuwa mpika chai wa waziri kwake ni mafanikio hivyo acha kumbughudhi ili ajione mnyonge aache kazi.
Well said
 
Huwezi kufanikiwa kama umeajiliwa..kuajiliwa kunabana muda,na kukosa fursa duniani..funguka ....
 
Sasa wote tutaacha kazi tuje forex???
Wengine wakafuge, wengine muende forex, wengine wakalime, wengine tubaki kuhudumia umma....
Hapo kwenye kilimo umenena. Ndo mana Mi sitaki kuja Mjini. Napambana na ngedere shambani.
 
Ashauriki mkuu.... Kasema ananyanyasika kazini na mshahara ni Mdogo unaishia kwenye pango LA nyumba ata kununua godoro na kitanda imekua issue sahivi anamwaka mmoja kazini na miezi kadhaa
Mwache aitikie wito wa MOYONI mwake
 
1.Jaribu kuchukua mshahara wako na ugawanye kwa masaa anayotumia kazini
Utakutana kwa lisaa unalipwa 500,1000 au 2000 Je jiulize una malengo ya kufikia wapi katika maisha yako?

2. Kumbuka kiasi chat mshahara unacholipwa ni 10% ya kile unachokizalisha kwa kampuni au taasisi husika unayofanyia kazi yaani kama unalipwa 500,000 kwa mwezi basi uwezo wako wa kuzalisha ni 5,000,000 sasa jiulize mpaka lini utaendelea kuzalisha kiasi kikubwa na wewe kulipwa ma mshahara kadogo?

Shida kubwa kwa waajiriwa ni kujisahau, kuridhika na kushindwa kuruhusu akili kufunguka kujiongezea kipato.
 
Braza nyumba ushamvua jamaa?au unaogopa kuishi kama Lucifer.haaa
Mwanagu ndo nimeambiwa ijumaa naingiziwa mpunga liwalo na liwe bora nichukue mjengo nipangishe coz mi nipo kwenye nyumba ya bure ya serikali
 
Back
Top Bottom