Mfanyakazi wangu akikaa dukani anauza zaidi yangu

Mfanyakazi wangu akikaa dukani anauza zaidi yangu

Pantomath

JF-Expert Member
Joined
Jan 4, 2019
Posts
842
Reaction score
3,449
Nimeamini kuna watu wana kismati tuu. Wakati naanzisha hii biashara nilikaa mwenyewe kwa mda flani ambao nilikua free,
Nikaona mauzo yanaenda poa tuu,

Baada ya majukumu ya kikazi kuanza nikatafuta sista duu haswaa, nikamuweka pale, Mauzo yalashukaa, sio kama hana lugha nzuri, anahudumia vzr na ni mzoefu sana

Kwa ufupi kwake niliweka matarajio makubwa ila mwishowe ni disappointment, Baada ya mda akapata mishe nyingne kwa uzuri wake akasepa na hatimaye hivi karibuni ataolewa na Moja ya wateja wake kipindi yuko hapa kazini.

Sasa sababu ilikua ghafla ikabidi nimchukue mdogo wangu akiwa anasubiri kwenda zake chuo. Huyu hana uzoefu wowote yaani siku nampeleka dukani nampa maelekezo nafanya ile tuu basi ila sikua na imani, kuachana na yote hayo bado ni mtoto.

Kwakua mwanzo biashara haikua ikienda basi nilijiwekea kila mwisho wa week ndio naulizia mauzo. Huyu ndio nikakaa kimya kabisa mpk week ya pili ndio nikauliza kiunyonge. Sikutegemea, alinipa mauzo ambayo sio mimi wala yule tulishawahi fikisha hata kwa mwezi, sikuamini, n

Nikahisi ni upepo tuu wa week mbili, cha kushangaza upepo huo ni miezi bado unaendelea, Week hii nikapata ka likizo nikasema nirudi nikakae mwenyewe,

Nimeishia kula za uso, Hapa nimemwambia kesho rudi golini na Nitakua nakulipa rasmi itakusaidia matumizi chuo, ada mahitaji mengine tuachie sisi au ukikwama niambie.

Mwanzo yeye na wazazi walisema haina haja ya kumlipa yeye anafanyia kazi ya ndani kwahio nikawa nampa tuu kajipesa kwa kushtukiza.

Nimepiga mahesabu kila kile kipo sawa.
 
Aliefanya biashara kufika hapo ni yule alieolewa kwa sababu huwezi anza biashara ghafla bin vuuu...ikawa sawa...hapo lazima kuna kama miezi 6 hadi 12 ya kuhaso halafu ndio kila kitu kinakua sawa hata ukiweka hapo mtu gani wateja watakuja sababu wanajua mahali wanapopata huduma.Biashara zote ni nzuri uvumilivu na subra ni muhimu.
 
Umenikumbusha mbali Mkuu! Enzi hizo kule msasani kuna jamaa alikua anaduka hili la mangi, Sasa akapiga kazii akafungua duka lingine tegeta pale akamuachia mdogo wake.

Yule dogo akalikuza lile duka likakua sana, Sasa Bro mtu ikawa mara moja moja kwa wiki anakuja kukaa golini pale kuangalia muenendo wa biashara, huwezi kuamini watu wakiona jamaa kakaa golini hawaendi, wanaulizana, Nani yuko Dukani? Kaka mtu au mdogo mtu? Kama kaka mtu basi watu wanapita kwenda mtaa wa pili kununua mazaga!
 
Umenikumbusha mbali Mkuu! Enzi hizo kule msasani kuna jamaa alikua anaduka hili la mangi, Sasa akapiga kazii akafungua duka lingine tegeta pale akamuachia mdogo wake.

Yule dogo akalikuza lile duka likakua sana, Sasa Bro mtu ikawa mara moja moja kwa wiki anakuja kukaa golini pale kuangalia muenendo wa biashara, huwezi kuamini watu wakiona jamaa kakaa golini hawaendi, wanaulizana, Nani yuko Dukani? Kaka mtu au mdogo mtu? Kama kaka mtu basi watu wanapita kwenda mtaa wa pili kununua mazaga!
Dhaaaa hii n kweli na ilinishanitokea tabata
Aiseeee mara nyingi kauli nzuri na mazoea
Mazur na wateja ndo yanainua biashara
 
Aliefanya biashara kufika hapo ni yule alieolewa kwa sababu huwezi anza biashara ghafla bin vuuu...ikawa sawa...hapo lazima kuna kama miezi 6 hadi 12 ya kuhaso halafu ndio kila kitu kinakua sawa hata ukiweka hapo mtu gani wateja watakuja sababu wanajua mahali wanapopata huduma.Biashara zote ni nzuri uvumilivu na subra ni muhimu.
Sio kweli... Alafu soma tena vzuri alivyo andika
 
Ndiyo maana mimi huwa naamini sio kila mtu anaweza fanya biashara. Biashara ni kismati skills na uzoefu (sio mtaji). Kama huna hizi sifa achana na kufikiri kufanya biashara.
 
Ndiyo maana mimi huwa naamini sio kila mtu anaweza fanya biashara. Biashara ni kismati skills na uzoefu (sio mtaji). Kama huna hizi sifa achana na kufikiri kufanya biashara.

Hamna usidanganyike....biashara ni usimamizi.

Kitu pekee nitakuambia mbinu na maaujanja yeyote utayapata ukisha anza fanya hyo biashara...biashara zina siri nyingi sanaa kwa kawaida ukianza utaona kwa juu juu faida / profits zake ni ndogo sanaa ila ukiingia kuna corners nyingi sana utajifunza hasa ukisimamia biashara yako mwenyewe pale mwanzo mwanzo.....utajikuta unakua mbunifu on the process.

Biz nyingi sana zina siri nyingi sanaa.....mfano: kuna stock za bei rahisi kutoka kwa watu wenye shida....unakuta kuna issue unaitiwa kitu flani sehem flani utapata bei

Ya kitonga na still unakuja uza at the same market price at ur shop na hata kama mzigo flani huna watu wana dalalia hadi wafanya biashara wengine ipo sana hii kwa biashara za mjini (mambo ni mengi sana, huwezi yajua hadi uwe kwenye game stahimili kama mwaka hivi utajifunza mengi sana)

One thing i gurantee you....ogopa sana watu wanaouza material za ujenzi / vifaa vya umeme / spare za magari with significant stock ni multi - millionaires waone hivi hivi tu.

Biashara ni mtandao. Amini nakuambia.
 
Back
Top Bottom