Herbalist Dr MziziMkavu
JF-Expert Member
- Feb 3, 2009
- 42,872
- 34,363
FAIDA ZA KITUNGUU SAUMU:
Kitunguu thaum kina harufu ya pekee isiyowapendeza watu wengi, ingawa kimebeba siri nyingi za tiba. Kwa ajili hiyo maanayake kwa kilatini ni : harufu ichomayo, na kwa kiarabu lugha ya Quraan huitwa: fuum, nayo ndio sahihi zaidi; kwasababu thaum ni lafdhi ya kihieroglifu ya kifirauni (hieroglyphic).
Allah S.W amesema:
" Na (kumbukeni habari hii kadhalika) Mliposea: Ewe Mussa! hatuwezi kusubiri chakula cha namna moja tu, basi tuombee kwa Mola wako atutolee vile vinavyooteshwa na ardhi kama mboga zake, matango yake, fuum (kitunguu thaum) zake, adesi zake na vitunguu vyake." (2:61)
Iliandikwa katika piramidi (pyramid) huko Misri tangu miaka 4500 iliopita kuwa kitunguu thaum kilikuwa wakipewa wajenzi ya piramidi. Walikuwa wakila kitunguu thaum ili wapate nguvu na nishati.
Mwandishi wa kitabu juu ya tiba zinazotokana na kitunguu thaum alimnasihi mfasiri wake kuwa " Iwapo unataka nguvu, nishati na uwekevu basi kula tembe ya kitunguu thaum na glasi ya maji kila siku kabla ya kula chakula. Daud Al-Antaky ameeleza katika kitabu chake cha Tadhkira kuwa kitunguu thaum hupoza zaidi ya maradhi 40.
Wale wapiganaji wa miereka wa huko Roma walikuwa wakila kitunguu thaum kabla ya kupigana ili wapate nguvu na wepesi.
Imethibitishwa kisayansi kuwa kitunguu thaum husafisha damu kutokana na mafuta (cholestrol) ambayo husababisha magonjwa ya mishipa ya ateri na maradhi ya moyo, na pia husafisha damu kutokana na vijidudu na maikrobati kuliko (antibiotic) vengine. Pia imethibitishwa kwa kuzuia kuenea kwa sumu ya nyoka katika mwili wa mwanaadam na pia husafisha maida kutokana na vimelea (parasites).
Rais wa matabibu, Ibn Sina amesema kuhusu kitunguu thaum: "Kitunguu thaum hulainisha na kuondoa gesi, hutoa vidonda katika ngozi, huhifadhi maji. Vumbi lake likichanganywa na asli akipakwa mwenye ukoma litamfaa, kitunguu thaum humfaa mwenye maradhi magonjwa ya mishipa na nyonga (sciatia). Maji yake (yaliotolewa kwa kupikwa) hutuliza maumivu ya meno, vilevile hufaa kwa kikohozi.
Kitunguu thaum kimekusanya protein 49% mafuta muhimu ya sulphur 25% na kiasi flani cha chumvi, homoni (hormones) zitiazo nguvu za kiume na vinavyoteremsha hedhi.
BAADHI YA MARADHI YANAYOTIBIWA NA KITUNGUU SAUMU:
Kiuasumu:
Saga tembe tano za kitunguu thaum, changanya na asali kikombe kimoja kilichochanganywa na habbasouda na kunywa papo hapo. Kunywa asubuhi na jioni. Paka mafuta ya kitunguu thaum pahala panapouma iwapo ni sumu ya nyoka au paka nje ya tumbo iwapo umekunywa sumu.
Kusafisha tumbo:
Kabla ya kula chakula, meza tembe za kitunguu thaum na baadae kunywa maji ya shimari yaliyochanganywa na asali kwa muda wa wiki moja.
Kiyeyusha mafuta (Cholestrol):
Unapokula chakula kila siku, weka katika kachumbari kiasi cha tembe 2 vilivyosagwa ule pamoja na kachumbari.
Kiongeza mkojo chenye kusafisha njia za mkojo:
Chemsha vizuri hairi, na baada ya kupoa tia tembe 3 za kitunguu thaum zilizosagwa. Kunywa kinywaji hicho kila siku kabla ya kula na kunywa juisi ya limau/ndimu.
Kuharisha damu (Dysentery):
Chukua tembe ya kitunguu thaum uikatekate na uile; fanya hivyo kwa muda wa wiki moja na bora zaidi ukinywa na mafuta ya zaituni kijiko kimoja.
Gesi na Indegestion:
Kunywa juisi ya pea iliyochanganywa na tembe 3 za kitunguu thaum kabla ya kulala kila siku.
Kutibu Typhoid:
Kata tembe 5 za kitunguu thaum, changanya ndani ya maziwa ya moto yaliyochanganywa na asali kunywa kabla ya kulala. Pia paka uti wa mgongo mafuta ya kitunguu thaum yaliyochanganywa na mafuta ya zeti, na asubuhi vuta moshi wa kitunguu thaum kwa muda wa dakika 5.
Kidonda kilichooza:
Ponda kitunguu thaum mpaka iwe laini kama marhamu halafu jifunge nacho kwa kutumia bendeji, japo kitawasha lakini kitazuia ugonjwa wa gangrene ambao unaweza ukapelekesha kukatwa kiungo. Vilevile unaweza kusafisha kidonda kwa kuchanganya kitunguu thaum kilichosagwa kikatiwa maji vuguvugu (warm water) na kikasafishwa kidonda.
Mishipa:
Kata tembe za kitunguu thaum na umeza kwa maziwa ya moto (sio moto sana) yenye matone ya ambari kabla ya kulala kila siku, dawa hii huipa mishipa nguvu.
Homa ya mafua (Influenza):
Kunywa juisi ya machungwa na juisi ya limau zilizochanganywa na tembe 7 za kitunguu thaum kunywa juisi hiyo kabla ya kulala. Vuta moshi wa kitnguu thaum.
Mafua:
Meza tembe za kitunguu thaum baada ya chakula pamoja na juisi ya kitunguu thaum iliyochanganywa na juisi ya limau pamoja na kuvuta moshi wa kitunguu thaum.
Saratani (Cancer):
Katika kitunguu thaum kuna kiini kinachozuia saratani, kwa kila mgonjwa wa saratani anashauriwa ale kwa wingi kitunguu thaum na karoti (carrot).
Kifua kikuu (cha mapafu):
Kila asubuhi kabla ya kula chakula meza tembe 3 za kitunguu thaum, saga ule pamoja na mkate na jioni vuta moshi wake.
Kipindupindu (cholera):
Ili kujikinga na maradhi hayo wakati kikienea, kula kijiko kimoja cha kitunguu thaum kilichosagwa na kukorogewa katika asali baada ya kila chakula.
Kutoa minyoo:
Ponda tembe 3 za kitunguu thaum, tia ndnai ya maziwa na kunywa (bila kutia sukari) jioni kabla ya kulala na asubuhi kunywa mafuta ya mbono.
Upele:
Chukua tembe 5 za vitunguu thaum uvisage na uvikoroge katika shahamu na paka pale penye upele kuazia jioni mpaka asubuhi na ukoshe kwa maji ya moto tumia kwa muda wa wiki moja.
Mbaa kichwani:
Ponda uzuri vitunguu thaum 3 na uvikoroge katika siki ya tofaha (Apple vinegar) katika chupa ya bilauri (sio plastiki) na uache juani kwa muda wa wili moja. Baada ya hapo jipake kichwani pamoja na kusugua kwa muda wa wili 1 na baada ya wiki jipake mafuta ya zeituni.
Nguvu za kiume:
Saga kitunguu thaum kitie ndani ya mafuta ya zeti na weka katika moto mdogo mdogo mpaka iwe rangi ya manjano na tia katika chupa na wakati wa haja jipake katika dhakari na osha baada ya saa moja.
Kujenga misuli na kutia nguvu:
Kila siku kabla ya kula kunywa kikombe kikubwa cha maziwa ya ngamia yaliyotiwa tembe 2 za kitunguu thaum iliyosagwa. Kunywa kwa muda wa mwezi mmoja mfululizo.
Kinga ya taunni na ukimwi:
Ngao kubwa ya maradhi mabaya ni Kumcha Allah S.W mwanzo na mwisho wa siku. Chukua juisi ya kitunguu thaum uichanganye na asali na unywe utafanya hivo pamoja na kumsha Allah S.W
Kitunguu thaum kina harufu ya pekee isiyowapendeza watu wengi, ingawa kimebeba siri nyingi za tiba. Kwa ajili hiyo maanayake kwa kilatini ni : harufu ichomayo, na kwa kiarabu lugha ya Quraan huitwa: fuum, nayo ndio sahihi zaidi; kwasababu thaum ni lafdhi ya kihieroglifu ya kifirauni (hieroglyphic).
Allah S.W amesema:
" Na (kumbukeni habari hii kadhalika) Mliposea: Ewe Mussa! hatuwezi kusubiri chakula cha namna moja tu, basi tuombee kwa Mola wako atutolee vile vinavyooteshwa na ardhi kama mboga zake, matango yake, fuum (kitunguu thaum) zake, adesi zake na vitunguu vyake." (2:61)
Iliandikwa katika piramidi (pyramid) huko Misri tangu miaka 4500 iliopita kuwa kitunguu thaum kilikuwa wakipewa wajenzi ya piramidi. Walikuwa wakila kitunguu thaum ili wapate nguvu na nishati.
Mwandishi wa kitabu juu ya tiba zinazotokana na kitunguu thaum alimnasihi mfasiri wake kuwa " Iwapo unataka nguvu, nishati na uwekevu basi kula tembe ya kitunguu thaum na glasi ya maji kila siku kabla ya kula chakula. Daud Al-Antaky ameeleza katika kitabu chake cha Tadhkira kuwa kitunguu thaum hupoza zaidi ya maradhi 40.
Wale wapiganaji wa miereka wa huko Roma walikuwa wakila kitunguu thaum kabla ya kupigana ili wapate nguvu na wepesi.
Imethibitishwa kisayansi kuwa kitunguu thaum husafisha damu kutokana na mafuta (cholestrol) ambayo husababisha magonjwa ya mishipa ya ateri na maradhi ya moyo, na pia husafisha damu kutokana na vijidudu na maikrobati kuliko (antibiotic) vengine. Pia imethibitishwa kwa kuzuia kuenea kwa sumu ya nyoka katika mwili wa mwanaadam na pia husafisha maida kutokana na vimelea (parasites).
Rais wa matabibu, Ibn Sina amesema kuhusu kitunguu thaum: "Kitunguu thaum hulainisha na kuondoa gesi, hutoa vidonda katika ngozi, huhifadhi maji. Vumbi lake likichanganywa na asli akipakwa mwenye ukoma litamfaa, kitunguu thaum humfaa mwenye maradhi magonjwa ya mishipa na nyonga (sciatia). Maji yake (yaliotolewa kwa kupikwa) hutuliza maumivu ya meno, vilevile hufaa kwa kikohozi.
Kitunguu thaum kimekusanya protein 49% mafuta muhimu ya sulphur 25% na kiasi flani cha chumvi, homoni (hormones) zitiazo nguvu za kiume na vinavyoteremsha hedhi.
BAADHI YA MARADHI YANAYOTIBIWA NA KITUNGUU SAUMU:
Kiuasumu:
Saga tembe tano za kitunguu thaum, changanya na asali kikombe kimoja kilichochanganywa na habbasouda na kunywa papo hapo. Kunywa asubuhi na jioni. Paka mafuta ya kitunguu thaum pahala panapouma iwapo ni sumu ya nyoka au paka nje ya tumbo iwapo umekunywa sumu.
Kusafisha tumbo:
Kabla ya kula chakula, meza tembe za kitunguu thaum na baadae kunywa maji ya shimari yaliyochanganywa na asali kwa muda wa wiki moja.
Kiyeyusha mafuta (Cholestrol):
Unapokula chakula kila siku, weka katika kachumbari kiasi cha tembe 2 vilivyosagwa ule pamoja na kachumbari.
Kiongeza mkojo chenye kusafisha njia za mkojo:
Chemsha vizuri hairi, na baada ya kupoa tia tembe 3 za kitunguu thaum zilizosagwa. Kunywa kinywaji hicho kila siku kabla ya kula na kunywa juisi ya limau/ndimu.
Kuharisha damu (Dysentery):
Chukua tembe ya kitunguu thaum uikatekate na uile; fanya hivyo kwa muda wa wiki moja na bora zaidi ukinywa na mafuta ya zaituni kijiko kimoja.
Gesi na Indegestion:
Kunywa juisi ya pea iliyochanganywa na tembe 3 za kitunguu thaum kabla ya kulala kila siku.
Kutibu Typhoid:
Kata tembe 5 za kitunguu thaum, changanya ndani ya maziwa ya moto yaliyochanganywa na asali kunywa kabla ya kulala. Pia paka uti wa mgongo mafuta ya kitunguu thaum yaliyochanganywa na mafuta ya zeti, na asubuhi vuta moshi wa kitunguu thaum kwa muda wa dakika 5.
Kidonda kilichooza:
Ponda kitunguu thaum mpaka iwe laini kama marhamu halafu jifunge nacho kwa kutumia bendeji, japo kitawasha lakini kitazuia ugonjwa wa gangrene ambao unaweza ukapelekesha kukatwa kiungo. Vilevile unaweza kusafisha kidonda kwa kuchanganya kitunguu thaum kilichosagwa kikatiwa maji vuguvugu (warm water) na kikasafishwa kidonda.
Mishipa:
Kata tembe za kitunguu thaum na umeza kwa maziwa ya moto (sio moto sana) yenye matone ya ambari kabla ya kulala kila siku, dawa hii huipa mishipa nguvu.
Homa ya mafua (Influenza):
Kunywa juisi ya machungwa na juisi ya limau zilizochanganywa na tembe 7 za kitunguu thaum kunywa juisi hiyo kabla ya kulala. Vuta moshi wa kitnguu thaum.
Mafua:
Meza tembe za kitunguu thaum baada ya chakula pamoja na juisi ya kitunguu thaum iliyochanganywa na juisi ya limau pamoja na kuvuta moshi wa kitunguu thaum.
Saratani (Cancer):
Katika kitunguu thaum kuna kiini kinachozuia saratani, kwa kila mgonjwa wa saratani anashauriwa ale kwa wingi kitunguu thaum na karoti (carrot).
Kifua kikuu (cha mapafu):
Kila asubuhi kabla ya kula chakula meza tembe 3 za kitunguu thaum, saga ule pamoja na mkate na jioni vuta moshi wake.
Kipindupindu (cholera):
Ili kujikinga na maradhi hayo wakati kikienea, kula kijiko kimoja cha kitunguu thaum kilichosagwa na kukorogewa katika asali baada ya kila chakula.
Kutoa minyoo:
Ponda tembe 3 za kitunguu thaum, tia ndnai ya maziwa na kunywa (bila kutia sukari) jioni kabla ya kulala na asubuhi kunywa mafuta ya mbono.
Upele:
Chukua tembe 5 za vitunguu thaum uvisage na uvikoroge katika shahamu na paka pale penye upele kuazia jioni mpaka asubuhi na ukoshe kwa maji ya moto tumia kwa muda wa wiki moja.
Mbaa kichwani:
Ponda uzuri vitunguu thaum 3 na uvikoroge katika siki ya tofaha (Apple vinegar) katika chupa ya bilauri (sio plastiki) na uache juani kwa muda wa wili moja. Baada ya hapo jipake kichwani pamoja na kusugua kwa muda wa wili 1 na baada ya wiki jipake mafuta ya zeituni.
Nguvu za kiume:
Saga kitunguu thaum kitie ndani ya mafuta ya zeti na weka katika moto mdogo mdogo mpaka iwe rangi ya manjano na tia katika chupa na wakati wa haja jipake katika dhakari na osha baada ya saa moja.
Kujenga misuli na kutia nguvu:
Kila siku kabla ya kula kunywa kikombe kikubwa cha maziwa ya ngamia yaliyotiwa tembe 2 za kitunguu thaum iliyosagwa. Kunywa kwa muda wa mwezi mmoja mfululizo.
Kinga ya taunni na ukimwi:
Ngao kubwa ya maradhi mabaya ni Kumcha Allah S.W mwanzo na mwisho wa siku. Chukua juisi ya kitunguu thaum uichanganye na asali na unywe utafanya hivo pamoja na kumsha Allah S.W