Mfuko bora wa pesheni ni upi kwa walimu watarajiwa?

Mfuko bora wa pesheni ni upi kwa walimu watarajiwa?

Realbest

JF-Expert Member
Joined
Aug 5, 2013
Posts
812
Reaction score
300
Naomba ushauri mfuko bora wa pensheni kwa walimu watarajiwa ni upi?
 
Realbest naungana na wewe kusubiri michango ya wadau wengine ili tupate kuwianisha mifuko hii ya pensheni, kwa maana siku hizi mifuko iko mingi sana!
 
Last edited by a moderator:
Wadau mfuko bora ni LAPF,nimewahi huzuria semina zao,ukokotoaji wa mafao yao n mzuri.Hii imewafanya kupata tuzo kwa miaka 5 mfululizo kama mfuko bora wa hifadhi ya jamii nchini.
 
Mfuko wa LAPF umetulia sana asikudanganye mtu, hiyo mingine inapumulia mirija.
 
Kama ndio kwanza unaanza kazi haijalishi ni mfuko upi mzuri kwsbu serikali iko mbioni kuharmonize fomula ya mafao kwa mifuko yote na hatimaye kumerge kuwa na mfuko 1 tuu. Chance ni kubwa km unaanza kazi leo ukaingia katika hii new plan!
 
LAPF ndio mpango mzima kwa sasa. hapa kigoma wafanyakazi walio kwenye mifuko mingine hasa pspf na nssf wamekuwa wakilalamika na kuomba wajiunge na LAPF ingawa sheria hairuhusu kuhama mfuko labda ujiunge kwa mfumo wa kuchangia we mwenyewe kwa hiyari
 
LAPF ndio mpango mzima kwa sasa. hapa kigoma wafanyakazi walio kwenye mifuko mingine hasa pspf na nssf wamekuwa wakilalamika na kuomba wajiunge na LAPF ingawa sheria hairuhusu kuhama mfuko labda ujiunge kwa mfumo wa kuchangia we mwenyewe kwa hiyari

pspf ndo bora zaidi
 
PSPF NDOO MPANGO MZIMA. UKIJIUNGA NA LAPT UTAKUJANIKUMBUKA. Washauri na rafiki zako unaowapenda na kuwajali. PSPF ndo mfuko wenye mafao matamu.
 
Wadau mfuko bora ni LAPF,nimewahi huzuria semina zao,ukokotoaji wa mafao yao n mzuri.Hii imewafanya kupata tuzo kwa miaka 5 mfululizo kama mfuko bora wa hifadhi ya jamii nchini.

Mwalmu wenu unacho sema nazani inaweza kuwa ni sahihi sababu na mm nmewah huzuria semina moja wapo, napia nmewah shauriwa na mkuu mmoja akadai LPF nimfuko mzuri kwa sasa na baadaye
 
PSPF NDOO MPANGO MZIMA. UKIJIUNGA NA LAPT UTAKUJANIKUMBUKA. Washauri na rafiki zako unaowapenda na kuwajali. PSPF ndo mfuko wenye mafao matamu.

Toa facts tukuelewe, unless una maslahi binafsi na hiyo fund
 
Unasemaje PSPF ni bora mbona unashindwa kucompete na LAPF au kwasbb walimu wengi wapo huko?tunataka mfuko wenye sera nzuri,utawala bora,ukokotoaji mzuri na mengineo.Wadau tusijiunge na mfuko kwa kufuata mkumbo.
 
Msijiunge na mifuko kwa kufuata mkumbo au kwavile ulisha wahi kuhudhuria semina zao.

Kujeni na facts zinazoeleweka kila upande (anaependelea mfuko fulani atoe fact) na kisha tutazipambanua wenyewe moja baada ya nyingine.
 
Unasemaje PSPF ni bora mbona unashindwa kucompete na LAPF au kwasbb walimu wengi wapo huko?tunataka mfuko wenye sera nzuri,utawala bora,ukokotoaji mzuri na mengineo.Wadau tusijiunge na mfuko kwa kufuata mkumbo.

Mfuko unaopendwa zaid kwa kuwa na formula bora mshahara wa mwisho, huduma bila foleni, mafao mengi ni LAPFna hauja filisika.
 
Mkuu ci kubaliani na wewe kwani mpaka sasa pspf uhai wake hatihati unapungukiwa tirion 6 kulipa wafanyakaz waliopo kazini cag, sasa anae jiunga leo atalipwa nini baadae, take care
 
Yap naungana na Mr2hr mfuko wenye mafao bora ni LAPF,kwanza angalia uwezo wa kulipa kwa miaka ijayo wanao? Na pia suppose wanachama wanastaafu leo ni 100 wanaweza kulipa? Jibu ni ndiyo kulingana na actuarial valuation iliyofanyika wana uwezo wa kulipa miaka 30 ijayo bila kuterereka tofauti na PSPF maana wanadaiwa sana,LAPF idumuuuuuuu!! Tujiunga jamani walimu wenzangu.
 
Mimi ni mwanachama wa LAPF na ndio naona mfuko bora wa mafao. Vikokotoa vyao vya fao la pensheni ni vizuri sana wana mafao mengine na habari niliyopata wanaanzishwa fao la elimu na mkopo wa elimu wanasubiri tu go ahead ya actuary ambaye amepewa kazi ya kutest. PSPF wako mahututi na wanaendelea on negative return yaani liabilities zao ni zaidi ya mapato so wameanza kule akiba yao ya siku nyingi so watakuwa hawana uwezo wa kulipa karibuni. Kuhusu formula kuwa sawa hiyo ni hadithi maana hata wazee wa serikalini hawataki hilo zaidi ya SSRA Wenyewe ambao hawana backing ya actuarial studies maana hata ile waliofanya wenyewe bado LAPF iko juu. Hiyo mifuko mingine ni mateso tu.
 
Kama ndio kwanza unaanza kazi haijalishi ni mfuko upi mzuri kwsbu serikali iko mbioni kuharmonize fomula ya mafao kwa mifuko yote na hatimaye kumerge kuwa na mfuko 1 tuu. Chance ni kubwa km unaanza kazi leo ukaingia katika hii new plan!

Hakuna kitu kama hicho mkuu, hizo ni ndoto kama mji wa kisasa wa Kigamboni. Mifuko inatakiwa ishindane na mfuko wenye afya ndio utakaolipa mafao bora zaidi. NSSF na PPF wana mafao kiduchu ajabu kiasi kwamba Manager anayechangia huko anapata vijisent kiduchu ukilinganisha na secretary wake anayechangia LAPF wakati mshahara wa secretary haufiki hata robo ya meneja. LAPF The best, wako fasta kulipa na unatoka na mfuko umetuna tofauti na kwengine
 
Back
Top Bottom