A
Anonymous
Guest
Mfumo wa Ajira Portal wa Secretariat ya Ajira ambao unapatikana katika tovuti ya Public Service Recruitment Secretariat | PSRS una changamoto kadhaa ambazo zimekuwa kikwazo kwa sisi Watumiaji wengi.
Mfumo huo hauruhusu kwa Watu wenye level ya elimu zaidi ya moja kujisajili na kuomba ajira katika nafasi tofauti na zile ambazo walijiandikisha mwanzo wakati wanajiunga kwenye mfumo.
Mfano ukiwa na Digrii au Diploma ukijisajili kwa moja kati ya hizo inamaanisha huwezi kuomba kazi kwa kutumia nafasi nyingine ya elimu hata kama umebadilisha vyeti kwenye mfumo.
Mfano ukijiandikisha Diploma kisha baadaye ukapata Digrii, mfumo hautatambua hayo mabadiliko kwa kuwa ile namba ya NIDA iliyotumika awali ilisoma wewe ni mtu wa Diploma, hivyo huwezi kuomba nafasi ya Digrii.
Hivyohivyo ukijiandikisha kuwa wewe una Digrii, zikitokea nafasi za Diploma, mfumo haukuruhusu kuomba kwa kuwa tayari namba yako ya NIDA inasoma wewe umesajiliwa katika qualification nyingine.
Tunaomba TAMISEMI washughulikie changamoto hii kwa kuwa imekuwa kikwao kwa watu wengi.
Mfumo huo hauruhusu kwa Watu wenye level ya elimu zaidi ya moja kujisajili na kuomba ajira katika nafasi tofauti na zile ambazo walijiandikisha mwanzo wakati wanajiunga kwenye mfumo.
Mfano ukiwa na Digrii au Diploma ukijisajili kwa moja kati ya hizo inamaanisha huwezi kuomba kazi kwa kutumia nafasi nyingine ya elimu hata kama umebadilisha vyeti kwenye mfumo.
Mfano ukijiandikisha Diploma kisha baadaye ukapata Digrii, mfumo hautatambua hayo mabadiliko kwa kuwa ile namba ya NIDA iliyotumika awali ilisoma wewe ni mtu wa Diploma, hivyo huwezi kuomba nafasi ya Digrii.
Hivyohivyo ukijiandikisha kuwa wewe una Digrii, zikitokea nafasi za Diploma, mfumo haukuruhusu kuomba kwa kuwa tayari namba yako ya NIDA inasoma wewe umesajiliwa katika qualification nyingine.
Tunaomba TAMISEMI washughulikie changamoto hii kwa kuwa imekuwa kikwao kwa watu wengi.