Lycaon pictus
JF-Expert Member
- Jan 31, 2021
- 9,189
- 16,128
Kila siku demokrasia inazidi kujithibitisha kama mfumo wa hovyo sana na haufai kutumika kama mfumo wa utawala.
Zamani nchi zilipoongozwa na wafalme nchi ilikuwa ni mali ya mfalme na vizazi vyake. Nchi ilikuwa kama mali yao binafsi na waliitunza kama mali binafsi.
Wafalme wengi walikuwa makini sana kuhakikisha kuwa mali yao haipotei. Walijitahidi kukopa kwa makini ili wasifilisike na wahakikishe wanarithisha wana wao mali ikiwa vyema. Hata wana wafalme wangeweza kumuua mfalme iwapo wangeona anataka kufuja urithi wao.
Pia kwenye mfumo wa kifalme mfalme hakuwa anawajibika kuwahudumia wananchi wake. Mfalme akiwafanyia kitu watu wake ilikuwa ni hisani tu. Mkimpa mfalme kodi yake ni yake kuitumia atakavyo.
Mfumo huu wa mtu mmoja kumiliki nchi si mzuri na wa kinyonyaji, lakini kwenye suala la kusimamia fedha ulikuwa mzuri kuliko wa kidemokrasia.
Kwenye mfumo wa kidemokrasia rais si mmiliki wa nchi, yeye ni msimamizi tu wa mali. Ni mpitaji tu. Hana uchungu wowote na mali ya nchi(Hana sababu ya kuwa na uchungu). Kuna uwezekano mkubwa madhara ya kukopa na kutapanya mali za umma yasimguse hata kidogo.
Pia serikali za kidemokrasia huwa na maafisa wengi sana ukilinganisha na zile za kifalme. Kuna wabunge, mawaziri, makatibu. . . Vyeo kibao. Wote hawa ni watumia pesa za nchi. Gharama za kulipa maafisa kwenye serikali za kidemokrasia ni kubwa mno.
Kingine ni kuwa kwenye mfumo wa kidemokrasia wananchi hutaka kuhudumiwa na serikali. Wananchi wana sauti juu ya matumizi ya pesa, na mara nyingi wanataka huduma zaidi na zaidi. Pia wana sauti juu ya kodi kiasi gani walipe
Matokeo yake ni kuwa serikali za kidemokrasia zinakuwa na matumizi mengi, zina uongozi usio na uchungu na mali ya umma na wananchi wasiotaka kulipa kodi.
Serikali nyingi za kidemokrasia zinaamua kukopa na kukopa. Serikali hizo zinajaa madeni hadi zinaishia kuanguka. Kila Rais ili abaki madarakani analazimika kukopa ili kuwafurahisha wananchi na maafisa wake. Kwanza mali siyo yake, na pili madeni atakomaa nayo anayekuja. Anayekuja naye amambambikia ajaye. Wakati wa ufalme alikuwa anaweza tokea mfalme mpya akaamua kufunga mkanda kufuta madeni ya baba zake. Rais wa kidemokrasia akisema afunge mkanda kufuta madeni ya watangulizi wake hawezi kaa madarakani hata mwaka. Basi anaamua kuendelea kukopa mambo yaende kipindi chake kama mdhamini kiishe.
Nchi inayoendeshwa kidemokrasia kufilisika sababu ya madeni ni suala la muda tu, halikwepeki.
Zamani nchi zilipoongozwa na wafalme nchi ilikuwa ni mali ya mfalme na vizazi vyake. Nchi ilikuwa kama mali yao binafsi na waliitunza kama mali binafsi.
Wafalme wengi walikuwa makini sana kuhakikisha kuwa mali yao haipotei. Walijitahidi kukopa kwa makini ili wasifilisike na wahakikishe wanarithisha wana wao mali ikiwa vyema. Hata wana wafalme wangeweza kumuua mfalme iwapo wangeona anataka kufuja urithi wao.
Pia kwenye mfumo wa kifalme mfalme hakuwa anawajibika kuwahudumia wananchi wake. Mfalme akiwafanyia kitu watu wake ilikuwa ni hisani tu. Mkimpa mfalme kodi yake ni yake kuitumia atakavyo.
Mfumo huu wa mtu mmoja kumiliki nchi si mzuri na wa kinyonyaji, lakini kwenye suala la kusimamia fedha ulikuwa mzuri kuliko wa kidemokrasia.
Kwenye mfumo wa kidemokrasia rais si mmiliki wa nchi, yeye ni msimamizi tu wa mali. Ni mpitaji tu. Hana uchungu wowote na mali ya nchi(Hana sababu ya kuwa na uchungu). Kuna uwezekano mkubwa madhara ya kukopa na kutapanya mali za umma yasimguse hata kidogo.
Pia serikali za kidemokrasia huwa na maafisa wengi sana ukilinganisha na zile za kifalme. Kuna wabunge, mawaziri, makatibu. . . Vyeo kibao. Wote hawa ni watumia pesa za nchi. Gharama za kulipa maafisa kwenye serikali za kidemokrasia ni kubwa mno.
Kingine ni kuwa kwenye mfumo wa kidemokrasia wananchi hutaka kuhudumiwa na serikali. Wananchi wana sauti juu ya matumizi ya pesa, na mara nyingi wanataka huduma zaidi na zaidi. Pia wana sauti juu ya kodi kiasi gani walipe
Matokeo yake ni kuwa serikali za kidemokrasia zinakuwa na matumizi mengi, zina uongozi usio na uchungu na mali ya umma na wananchi wasiotaka kulipa kodi.
Serikali nyingi za kidemokrasia zinaamua kukopa na kukopa. Serikali hizo zinajaa madeni hadi zinaishia kuanguka. Kila Rais ili abaki madarakani analazimika kukopa ili kuwafurahisha wananchi na maafisa wake. Kwanza mali siyo yake, na pili madeni atakomaa nayo anayekuja. Anayekuja naye amambambikia ajaye. Wakati wa ufalme alikuwa anaweza tokea mfalme mpya akaamua kufunga mkanda kufuta madeni ya baba zake. Rais wa kidemokrasia akisema afunge mkanda kufuta madeni ya watangulizi wake hawezi kaa madarakani hata mwaka. Basi anaamua kuendelea kukopa mambo yaende kipindi chake kama mdhamini kiishe.
Nchi inayoendeshwa kidemokrasia kufilisika sababu ya madeni ni suala la muda tu, halikwepeki.