Mfumo wa kuteua Mawaziri una kasoro unabagua makundi kama ya wafanyabiashara, wenye viwanda na wakulima, wafugaji na wavuvi

Mfumo wa kuteua Mawaziri una kasoro unabagua makundi kama ya wafanyabiashara, wenye viwanda na wakulima, wafugaji na wavuvi

Shotocan

JF-Expert Member
Joined
Nov 21, 2023
Posts
6,650
Reaction score
12,711
Wizara ndizo husimamia sera na mipango husika kwa ajili ya maendeleo.

Uteuzi wa mawaziri kwa sasa umejikita sana kuzingatia mikoa, makundi maalaumu kama vijana, wazee ,akina mama na walemavu na wasomi na watoto na ndugu wa vigogo waliopita au waliopo.

Wafanyabiashara wakubwa hawamo wakulima na wafugaji wakubwa hawano,wenye viwanda vikubwa hawamo hii haijakaa sawa.

Hizo sekta ndizo mhimili mkubwa wa uchumi wawepo hata mawaziri wadogo tu toka hizo sekta.

Ni ubaguzi wa hali ya juu. Na ndio maana kunakuwa na sintofahamu mara nyingi sababu washika nafasi hawaelewi hizo sekta vizuri kama walioko huko kwenye hiyo sekta.
 
Wafanyabiashara wakubwa si ndio hao akina Msukuma,Shabiby,Tabasamu,Kushimba na wengineo ambao elimu zao ni darasa la 7 na form 4.
Kwa hiyo unataka tuteue Mawaziri darasa la 7 au form 4??????
 
Mfumo wa uteuzi kiujumla umekaa kisiasa zaidi, hauangalii compitence ya mtu...hata kauli ya Prof Assad majuzi tu hapa inasadiki hivyo...60% ya viongozi serikalini HAWANA uwezo!.
Tungekuwa na jamii inayojielewa kama kule Kenya wananchi tusingekubaliana na upuuzi huo wa kikundi kdg cha watu (wanasiasa)!.
 
Wafanyabiashara wakubwa si ndio hao akina Msukuma,Shabiby,Tabasamu,Kushimba na wengineo ambao elimu zao ni darasa la 7 na form 4.
Kwa hiyo unataka tuteue Mawaziri darasa la 7 au form 4??????
Kama hawapo hamna shida kuna vile viti maalumu vya uteuzi Raisi aweza wateua wabunge halafu akawapa uwaziri wala hamna shida hata wasipogombea
Sasa kama hata wabunge wa kuteuliwa na Raisi hawatoki hayo makundi hiyo kitu sio sawa kabisa

Vile viti maalum raisi anapewa ateue ni kwa ajili ya kuteua watu potential hasa kuingia bungeni ili wasaidie nchi sio nafasi za fadhila kwa shangazi ,mjomba nk au ohh yule mwenzetu asibaki bila cheo nitakupa ubuunge viti maalumu nafasi anazopewa Raisi
 
Mfumo wa uteuzi kiujumla umekaa kisiasa zaidi, hauangalii compitence ya mtu...hata kauli ya Prof Assad majuzi tu hapa inasadiki hivyo...60% ya viongozi serikalini HAWANA uwezo!.
Tungekuwa na jamii inayojielewa kama kule Kenya wananchi tusingekubaliana na upuuzi huo wa kikundi kdg cha watu (wanasiasa)!.
Kenya walichelewa sana ndio wameamka sasa
 
Back
Top Bottom