Mfumo wa Muungano ni JANGA LA KITAIFA ?

Mfumo wa Muungano ni JANGA LA KITAIFA ?

battawi

JF-Expert Member
Joined
Mar 29, 2014
Posts
2,712
Reaction score
2,577
Mimi nadhani ni Mfumo wa MUUNGANO waliojiwekea hauruhusu mabadiliko, kwahiyo CCM wamekwama.
Nadhani sasa ni wakati muafaka kabla ya kuandika kwa katiba mpya Pajadiliwe mfumo muafaka wa Muungano kwanza .
Kuna hatari kuwa endapo chama kingine kisichokuwa CCM kukamata upande mmoja wa Muungano na upande wa pili kuwepo CCM hali itakuwa ni ya Minyukano zaidi. Zanzibar wanataka MAMLAKA KAMILI
Natoa tahadhari. MUUNGANO WETU NI TUNU, LAKINI UNAPASWA UENDANE NA MATAKWA YA WAKATI NA MBADILIKO YA KIFIKRA ZA WADAU NA MAHITAJI.
Nawakilisha
 
Aidha Huku bara kuna Mashirika hayahusuani kabisa na Muungano, lakini Huitwa ya Muungano, na yanapata ruzuku toka kwenye serikali ya Muungano
 
idha Huku bara kuna Mashirika hayahusuani kabisa na Muungano, lakini Huitwa ya Muungano, na yanapata ruzuku toka kwenye serikali ya Muungano
Mmh!!
Nabii mvivu: Daudi kwenye Msafara waliamrishwa wabebe jiwe moja kila mmoja wao
Daudi kwa uvivu wake akabeba kajiwe kadogo walipofika mbele walipumzka Nabii Issa akawaambia: kila mmoja wetu jiwe litabadlika kuwa Mkate tupate kula Daud alibeba Jiwe dogo Mkate wake ulikuwa mdogo hakushiba wenzake wote walishiba kisha wakaamrishwa wabebe tena jiwe na kuanza safar Daudi kwa hasira zake hakushiba Mkate na akaamin kwamba safar hii jiwe tena litabadilika kuwa Mkate akabeba Jiwe kubwa mno kuwazid wote. walipofika mbele wakapmzka tena Nabii Issa akasema: kila mwenye jiwe arushe umbali ambao utakuwa na uwezo nao ndio itakuwa urefu wa maisha yako weng walirusha umbali mkubwa sana sasa kaz kwa ndugu yangu Daudi aliyebeba jiwe kubwa akiamin litabadlika kuwa Mkate ili afaid zaid alirusha hatua 3 tu aliposimama yeye ndio alikuwa mtu wa kwanza kufa kwenye ule Msafara..!!
 
Ndugu wana JF habari za sku.
Imenilazimu kuandika Mada hi baada ya kuona mengi yanayojitokeza nchini kwetu.
Raisi wetu mama Samia Suluh Hassan anapofanya teuzi zake hutuhumiwa na baadhi ya watu kuwa anaupendeleo kwa Zanzibar wenzake.
Uteuzi wa Mkurugenzi wa TPDC inatuhumiwa eti ni mzanzibari na inaonekana haistahiki kwa shirika la Muungano.
ilitakiwa amchague Mtanganyika. kwakuwa Zanzibar eti wanashirika lao linaitwa ZPDC.
Mitafaruku ya aina hii ya mambo ya kimuungano imeshajitokeza sana kwa maraisi waliotangulia.
OIC ilifika kuleta mtafaruku wa kuvunjika Muungano.
Suala la Benki kuu na A/C ya pamoja bado ni kitendawili tokea miaka ya 80 HAKIJATEGULIWA.
Kuna tume kadhaa zimeundwa na kutumia fedha nyingi za Watanzania hatimae mapendekezo yao yametupwa.
Moja ya mapendekezo ni lile la serikali 3. liiwa limependekezwa na tume zaidi ya 3.
Kuna vikao vya mawaziri wakuu na waziri kiongozi(Makamu wa pili wa raisi kwa sasa) Zanzibar kuhusu kujadili,na kuyatatua machangamoto ya kimuungano. Lakini ukweli hadi leo bado ni kioja , na fedha zinaliwa katika kamati na vikao mbali mbali.
Zanzibar ilitaka Kujenga Bandari ya Mpiga duri ,Mkopo wa pesa umezuiwa na waziri wa Mungano na kufanya mradi ule ufe.
Zazibar walianza mchakato wa kuchimba mafuta na Gesi wakati wa Dr.Sheni, lakini Wataalamu walipewa masa 24 kuondoka Tanzania na mchakato wa kampuni ya Ras el khema petroleum, ukafia pale nungwi.
Takriban Miradi mingi ya Zanzibar imelalamikiwa kukwamishwa na Muungano kwa zanzibar kuzuiwa kukopa fedha nje.
Leo Zanzibar wana ZRB ambayo ni mbadala wa TRA ambayo ni ya Muungano. Kuna ZBS ambayo ni mbadala wa TBS na
SUMATRA ya Muungano na Zanzibar wana Sumatra ya kwao.
Hii ni kuonesha kuwa Kuna mvutano ya kimuungano ambayo CCM wenyewe wameshindwa kuitatua.

Munajua sababu nini?

Mimi nadhani ni Mfumo wa MUUNGANO waliojiwekea hauruhusu mabadiliko, kwahiyo CCM wamekwama.
Nadhani sasa ni wakati muafaka kabla ya kuandika kwa katiba mpya Pajadiliwe mfumo muafaka wa Muungano kwanza.

Kuna hatari kuwa endapo chama kingine kisichokuwa CCM kukamata upande mmoja wa Muungano na upande wa pili kuwepo CCM hali itakuwa ni ya Minyukano zaidi. Zanzibar wanataka MAMLAKA KAMILI
Natoa tahadhari. MUUNGANO WETU NI TUNU, LAKINI UNAPASWA UENDANE NA MATAKWA YA WAKATI NA MBADILIKO YA KIFIKRA ZA WADAU NA MAHITAJI.

Nawakilisha
karibuni kwa mjadala
 
You are very right ndugu battawi. Muungano huu una exist kwa nguvu ya dola tu na si kwa ridhaa ya wananchi..

Na jambo lihusulo utawala wa nchi linapolazimishwa pasipo utashi wa wananchi, hilo huwa halina MWISHO mwema siku zote..

Huu muungano uko Kwa sababu kuu mbili tu;

1. CCM kuwa madarakani ktk pande zote za muungano..

2. CCM kulinda maslahi yake ya kiutawala..

Lakini haya yote MWISHO wake ni siku ambayo CCM imetoweka duniani na siku hiyo haiko mbali..
 
Muungano bado upo na Utaendelea kuwepo, Lakini Mfumo wa Kinyerere nim lazima ufikie mwisho.
Wazee hawa walianzisha jambo kwa nia safi ,lakni misingi yake ni ya Kizamani zamani ,ya kuaminiana tuu.
Hata Mababu zetu zamani walikuwa wanauziana vitu kwa maneno tuu bila ya Risiti wala Nyaraka,.
Kwa dunia leo kila kitu ni Documents na Mashariti na vipengele vya kutatulia migogoro kwa pale kwenye Ushirika.
Kwa Muungano huu hauna yote hayo.
 
Sasa naona kila kukicha hali ya Muungano inazidi kuwa tete.
Zamani ilikuwa nadra sana kuwasikia watanganyika wakiitaja Tanganyika yao,
Lakini sasa naona Imeanza kuw midomono mwao kwa sana tuu.
Kaeni sawa Tanganyika yaja very soon au Muungano inafikia ukingoni endapo wazenji wataamua kutafuna jongoo kwa meno.
 
Back
Top Bottom