Mfumo wetu wa elimu ni takataka, unatulazimisha tuwe watu wa kukariri zaidi kuliko kuelewa. Kukariri hakuwezi kuleta ubunifu

Mfumo wetu wa elimu ni takataka, unatulazimisha tuwe watu wa kukariri zaidi kuliko kuelewa. Kukariri hakuwezi kuleta ubunifu

NetMaster

JF-Expert Member
Joined
Sep 12, 2022
Posts
1,454
Reaction score
4,925
Naomba nisieleweke vibaya nashare tu mtazamo wangu ili kuboresha na kuwa na taifa bora zaidi lenye uwezo wa kutatua matatizo yake kwa kutumia wataalamu wake.

Mfumo wetu wa elimu huko hivi unamchukua samaki na ndege aina ya tai alafu unawapa mtihani mmoja. Yaani unampima samaki kwa kupaa juu na tai unamuingiza baharini ili aogelee. Mwisho wa siku wote wanafeli alafu unahisi hawana akili kumbe umetumia vipimo visivyo sahihi.

Mfumo wetu wa elimu unatulazimisha tuwe watu wa kukariri zaidi kuliko kuelewa.

Tunapokuwa watu wa kukariri tunajikuta tunasoma kwa ajili ya kufaulu mitihani na sio kuelewa. Ukishafanya mtihani kila ulichokariri kinafutika.

Mtihani mwingine ukija inakubidi ukariri tena. Basi huo mzunguko unaendelea tena na tena na tena.

Tuna uwezo wa kuwa wavumbuzi lakini sasa unakuwaje mvumbuzi wakati elimu yako yote toka msingi mpaka ngazi uliyopo sasa umefaulu vema sio kwa sababu ulikuwa ukielewa sana lakini kwa sababu ulikuwa unakariri vema.

Kukariri kunakuwezesha kutoa copy ya ulichofundishwa.

Kuelewa kunakuwezesha kutumia ulichofundishwa kuleta mabadiliko. Huwezi kuapply kile ambacho hujaelewa.

Huwezi kufanya innovation kwa maarifa uliyokariri. Innovation inafanywa na maarifa uliyoyaelewa.

Huwezi kuwa creative wakati elimu yako ni elimu kariri.

Creativity inazaliwa kutoka kwenye elimu uliyoelewa.

Mungu tusaidie tuelewe sio tukariri. Mungu ibariki Tanzania.
 
Naomba nisieleweke vibaya nashare tu mtazamo wangu ili kuboresha na kuwa na taifa bora zaidi lenye uwezo wa kutatua matatizo yake kwa kutumia wataalamu wake .
.
Mfumo wetu wa elimu huko hivi unamchukua samaki na ndege aina ya tai alafu unawapa mtihani mmoja. Yaani unampima samaki kwa kupaa juu na tai unamuingiza baharini ili aogelee. Mwisho wa siku wote wanafeli alafu unahisi hawana akili kumbe umetumia vipimo visivyo sahihi.
.

Mfumo wetu wa elimu unatulazimisha tuwe watu wa kukariri zaidi kuliko kuelewa.

Tunapokuwa watu wa kukariri tunajikuta tunasoma kwa ajili ya kufaulu mitihani na sio kuelewa.

Ukishafanya mtihani kila ulichokariri kinafutika.

Mtihani mwingine ukija inakubidi ukariri tena.

Basi huo mzunguko unaendelea tena na tena na tena.
Tuna uwezo wa kuwa wavumbuzi lakini sasa unakuwaje mvumbuzi wakati elimu yako yote toka msingi mpaka ngazi uliyopo sasa umefaulu vema sio kwa sababu ulikuwa ukielewa sana lakini kwa sababu ulikuwa unakariri vema.

Kukariri kunakuwezesha kutoa copy ya ulichofundishwa.

Kuelewa kunakuwezesha kutumia ulichofundishwa kuleta mabadiliko.

Huwezi kuapply kile ambacho hujaelewa.

Huwezi kufanya innovation kwa maarifa uliyokariri.

Innovation inafanywa na maarifa uliyoyaelewa.

Huwezi kuwa creative wakati elimu yako ni elimu kariri.

Creativity inazaliwa kutoka kwenye elimu uliyoelewa.

Mungu tusaidie tuelewe sio tukariri. Mungu ibariki tanzania.
Elimu ya Tanzania ni UTAPELI

Elimu ya Tanzania ni ya MCHONGO

Elimu ya Tanzania ni BIASHARA.

I think education is expensive now I'm trying ignorance.
 
Wazungu walileta
1. Elimu
2. Dini
Hivyo vyote vimekuwa mzigo kwa mtu mweusi badala ya kuwa mkombozi
 
inashangaza sana mtoto wa darasa la nne hafahamu jinsi ya kuanda tuta la bustani lakini nyimbo ya kwikwi imemkaa kichwani kama BABA YETU ULIE MBINGUNI .....
 
Wenye mamlaka na uwezo wa kubadirisha mitaala wapo, wanajua, wanaelewa na wanasoma sana haya maandiko humu, ila hawawezi kubadirisha muwe kama wao.

Elimu ya nchi yetu ninkwa ajili yetu wenyewe na inafanywa hivi ili walioshika mpini waendelee kuwatawala.

Kadiri unavyotoka gizani ndivyo unazidi kuona na kujua ulivyokuwa uoni na hujui.
 
Kila siku tunasema humu kuwa hakuna elimu bali mtoto anachapwa akariri tu
Wanapewa shahada zisiweza kumpatia kazi hata Nairobi tu
 
Back
Top Bottom