Mfumuko wa bei Zanzibar sasa imekuwa gumzo. Ni wakati sasa Rais Dkt. Mwinyi kujitafakari

Mfumuko wa bei Zanzibar sasa imekuwa gumzo. Ni wakati sasa Rais Dkt. Mwinyi kujitafakari

5525

JF-Expert Member
Joined
Apr 6, 2014
Posts
5,412
Reaction score
6,279
Ndivyo hali ilivyo Zanzibar, watu walianza kuvimilia vumilia sasa kila mzanzibar analia na vitu vya chakula kupanda bei tena kwa speedi ya kutisha sana.

1. Mkate wa Boflo ambao ndio mkate kila mzanzibar anakula sasa ni Tshs 250/- badala ya 200/=

2. Mchele ambao ndio chakula kikuu kwa maisha ya Wazanzibari Rais Mwinyi alivyoingia madarakani ilikuwa 1kg ni Tshs 1600 wa bei ya chini wanaita mapembe mchele mbovu sana huu sasa umepanda hadi ni Tshs 2000/= per kilo

3. Mchele wa mbeya ambao ni standard kule bara hauzidi Tshs 2000/- per kilogram, Lakini ukiuliza mchelewa mbeya zanzibar utakuta bei zinaanzia 2200/- per kg ambao huu ni chenga tupu, unafuata mchele mwengine wa kawaida 2400/- per kg., unafuata mwengine hadi 2800/- per kg ni tofauti sana maisha haya na awamu iliyopita ya Dr. Ali Mohamed Shein.

4. Sukari ilikuwa Tshs 2000/- per kg sasa wanauza 2400/-

5. Mafuta ya kupikia nusu lita ilikuwa 1000/- sasa ni Tshs 2000/=

6. Sahani ya chips plain ikiuzwa 1500/- sasa wamelazimika kupandisha hadi 2000, ambapo chips mayai ikiuzwa 2500/- sasa ni Tshs 3000/=

Huu ni mfano wa bidhaa kwa vyakula fulani fulani lakini takriban hali ni hiyo hiyo kwa vyakula vilivyobakia kama maharage, kunde nk.

Lakini kama haitoshi adha ya maji imerudi ambapo sasa unaweza kukaa mwezi mieizi miwili ama wiki 3 kwa kiwango cha chini maji hayatoki kwenye mabomba watu inabidi wayafuate maji maeneo ya mbali sana tofauti na awamu ilyopita ya Dr. Mohammed Ali Mohamed Shein ambaye kwa kiasi kikubwa aliweza kuondoa kero ya maji visiwa vya Zanzibar.

Lakini kama haitoshi mahospitali dawa hamna inabidi ununua hadi bomba ya sindano baadae urudi kwa daktari akuchome sindano. nadhan haileti picha nzuri sana kwa Mhe, Rais wetu mpendwa hali imekuwa ni tete sana Zanzibar katika maisha ya watu

Nimeona niilete hapa hii kwenu wadau na labda Mhe. anaweza kulijua hili na kujitathmini kwa muda ambao sasa ameingia madarakani

Wazanzibar walikuwa na matumaini sana baada ya kuunganisha tofauti zilizokuwepo na kumpa mioyo yao Dr. Mwinyi lakini sasa hali imeanza kuwa tete kutokana na maisha ya watu.

Wazanziri wamekuwa wakepewa maneno laini laini lakini sidhani kama hii hali itawapeleka mbele zaidi.

Kwenu wadau katika hili.
 
Ndivyo hali ilivyo Zanzibar, watu walianza kuvimilia vumilia sasa kila mzanzibar analia na vitu vya chakula kupanda bei tena kwa speedi ya kutisha sana.,
1. Mkate wa Boflo ambao ndio mkate kila mzanzibar anakula sasa ni Tshs 250/- badala ya 200/=
2. Mchele ambao ndio chakula kikuu kwa maisha ya Wazanzibari Rais Mwinyi alivyoingia madarakani ilikuwa 1kg ni Tshs 1800 wa bei ya chini sasa ni Tshs 2400/= per kilo
3. Sukari ilikuwa Tshs 2000/- per kg sasa wanauza 2400/-
3. Mafuta ya kupikia nusu lita ilikuwa 1000/- sasa ni Tshs 2000/=
3. Sahani ya chips plain ikiuzwa 1500/- sasa wamelazimika kupandisha hadi 2000, ambapo chips mayai ikiuzwa 2500/- sasa ni Tshs 3000/=

Huu ni mfano wa bidhaa kwa vyakula fulani fulani lakini takriban hali ni hiyo hiyo kwa vyakula vilivyobakia kama maharage, kunde nk.

Lakini kama haitoshi adha ya maji imerudi ambapo sasa unaweza kukaa mwezi mieizi miwili ama wiki 3 kwa kiwango cha chini maji hayatoki kwenye mabomba watu inabidi wayafuate maji maeneo ya mbali sana tofauti na awamu ilyopita ya Dr. Mohammed Ali Mohamed Shein ambaye kwa kiasi kikubwa aliweza kuondoa kero ya maji visiwa vya Zanzibar.

Lakini kama haitoshi mahospitali dawa hamna inabidi ununua hadi bomba ya sindano baadae urudi kwa daktari akuchome sindano. nadhan haileti picha nzuri sana kwa Mhe, Rais wetu mpendwa hali imekuwa ni tete sana Zanzibar katika maisha ya watu

Nimeona niilete hapa hii kwenu wadau na labda Mhe. anaweza kulijua hili na kujitathmini kwa muda ambao sasa ameingia madarakani

Wazanzibar walikuwa na matumaini sana baada ya kuunganisha tofauti zilizokuwepo na kumpa mioyo yao Dr. Mwinyi lakini sasa hali imeanza kuwa tete kutokana na maisha ya watu.

Wazanziri wamekuwa wakepewa maneno laini laini lakini sidhani kama hii hali itawapeleka mbele zaidi.

Kwenu wadau katika hili.
mwandish wa habar hii ni mgen sana kwa maisha ya zanzibar kwa miaka yote chakula zanzibar ni ghali sana aswa kwa mchele viaz unga uwez kuona ulojo ukiwa bei juu vyaula vyote ambavyo vinaletwa kutoka morogoro mbeya shinyanga unategemea bei iwe chini wakat dar mchele nzur ni 2000 nk

Sent from my SM-G965U using JamiiForums mobile app
 
Lakini kama haitoshi adha ya maji imerudi ambapo sasa unaweza kukaa mwezi mieizi miwili ama wiki 3 kwa kiwango cha chini maji hayatoki kwenye mabomba watu inabidi wayafuate maji maeneo ya mbali sana tofauti na awamu ilyopita ya Dr. Mohammed Ali Mohamed Shein ambaye kwa kiasi kikubwa aliweza kuondoa kero ya maji visiwa vya Zanzibar.
hii shehia ya uswahilini kwetu huduma ya maji ya ZAWA inapatikana kila baada ya siku 3 au 4, na walivyo wahuni wanaweza kutufungulia maji majira ya saa 7 usiku, hapo tena utachagua usingizi au maji.

kwa sasa tumekuwa tukitegemea zaidi huduma ya maji tuliounga kwa michango ya wanakijiji kuliko maji ya serikali.
serikali za manigga hazijawahi kuwa na huduma zenye uhakika.
siku mbili kabla ya sherehe za mapinduzi walitoa huduma ya maji mchana kutwa

ngoja tusubirie huu mradi mpya wa maji walioanza kuchimbia mabomba, pengine tunaweza kupata unafuu.
 
... wale kwa urefu wa kamba zao wasivimbiwe wakachafua hewa!
 
Back
Top Bottom