Mfungo wa Ramadhani katika Mji wa Harare Zimbabwe

Mfungo wa Ramadhani katika Mji wa Harare Zimbabwe

Mohamed Said

JF-Expert Member
Joined
Nov 2, 2008
Posts
21,967
Reaction score
32,074
MFUNGO WA RAMADHANI KATIKA MJI WA HARARE ZIMBABWE

Zamani ilikuwa ukiwa na safari unahitaji vibali kadhaa ili uweze kusafiri, iwe safari ya kikazi au vinginevyo.

Kwanza utahitaji kibali cha Benki Kuu ili uweze kupata fedha za kigeni.

Naamini kuna wasomaji wangu hawajapatapo kusikia kitu kinaitwa Thomas Cooke Travellers Cheque.

Hii ni hundi ambayo msafiri alikuwa anapewa na afikapo safari yake atavunja kupata dollars, pounds nk.

Kulikuwa na kibali cha Wizara husika, kibali cha Ikulu nk. nk. kiasi kuwa hadi umemaliza kupata vibali vyote hivyo mtu unakuwa taaban kwa kuchoka.

Ukiingia tu kwenye ndege hata kabla haijaruka umeshalala kwa uchovu na si kama natia chumvi mimi mwenyewe yamenitokea mara nyingi tu.

Kusafiri ilikuwa shughuli pevu.

Nasafiri kwenda Harare Mwezi Mtukufu wa Ramadhani ndege Air Tanzania Corporation (ATC) wenyewe ndege hii tukiipa majina kadha wa kadha lakini mimi nililipenda jina la Twiga.

Ndege ya alfajir saa 12 kwa hiyo nimefika uwanjani kumi ya usiku.

Tumetua Harare na haukupita muda niko nje ya uwanja na ndani ya teksi inanipeleka mjini.

Madereva wa taxi wanajua mengi sana kuanzia ''rate,'' ya ''dollar black market,'' hadi hoteli nzuri kwa malazi na chakula.

Dereva wa taxi namuuliza kuhusu msikiti uliopo mjini jirani na hoteli yangu ''Ambassador Hotel.''

Mimi na dereva wa taxi tunazungumza Kiingereza na natumia neno. ''mosque,'' neno hili halipo katika msamiati wake wa Kiingereza.

Nimejitahidi sana kumuelewesha lakini hakunielewa.
Mwisho nikamwambia, ''the place where Muslims pray.''

''Oh! You mean Muslim church I will show you!''

Nikapumua na kweli akanipitisha kwenye huo msikiti nikauona.

Niko Ambassador Hotel, katikati ya mji.

Tarweh nikawa nasali kwenye huu msikiti lakini wengi wa waumini ni Wahindi na Waafrika wachache kutoka kabila la Wayao.

Meneja wa hoteli akawa hanioni kwenye chai asubuhi akanitafuta kutaka kujua kwa nini siendi kunywa chai kwenye dining room ya hoteli.

Kaniuliza tena kwa masikitiko.
Nikamfahamisha kuwa nimefunga Mwezi wa Ramadhani.

Yule Bwana Meneja wala hajui Ramadhani ni kitu gani lakini akaniambia kuwa kuanzia siku hiyo atamfahamisha ''Chef,'' yaani mpishi wa hoteli anitayarishie futari jioni kama fidia ya ya chai ya asubuhi na itakuwa, ''Room Service,'' futari italetwa chumbani kwangu tena, "on the house,'' yaani hawatanitoza chochote.

Furaha yangu haisemeki.

Jioni ile ulipotimu muda wa kufungua nikapiga simu,''Room Service,'' na haukupita muda mlango ukagongwa na futari ikaletwa imefunikwa vizuri sana.

Ikafunuliwa na kwa hakika ule muonekano wake ulinivutia kupita kiasi.

Chakula na vinjywaji vilikuwa vimepangika vyema.

Lakini katika kutupa jicho nikaona kuna nyama ina rangi nyeupe inayokwenda kwenye wekundu na imekatwa ''slice,'' nyembamba iliyoviringika.

Yule bint aliyeleta futari ile alikuwa bado hajatoka mle chumbani kasimama ananiangalia ninavyokitazama chakula kile.

Nikamuuliza kuhusu ile nyama kuwa ni nyama gani?

Jibu alilonipa lilinishtua.

''This is pork sir.''

Kanifahamisha kuwa ile nyama ilikuwa nguruwe.

Futari ya nguruwe.

Kwa utaratibu nilimuomba aondoe chakula chote kile akirudishe jikoni.

Nilihama siku ya pili nikahamia hoteli nyingine inaitwa Holiday Inn.

Kusafiri hakika ni elimu tosha.
 
Kuna siku nilimtania FF kwamba napenda Sana futari hasa ya nguruwe..aisee nikikula ban! Pole Sana!
 
Siku hizi mambo yamebadilika sana duniani na neno "Halal" limekuwa maarufu kwa kila ndege na baadhi ya hotels
Neno halal linaandikwa sehemu nyingi kuliko vegetarian
Lakini sikushangaa sana kwa ftari ya pork kwani hukuwatahadharisha kuwa wewe huli huyo mdudu
 
MFUNGO WA RAMADHANI KATIKA MJI WA HARARE ZIMBABWE

Zamani ilikuwa ukiwa na safari unahitaji vibali kadhaa ili uweze kusafiri, iwe safari ya kikazi au vinginevyo.

Kwanza utahitaji kibali cha Benki Kuu ili uweze kupata fedha za kigeni.

Naamini kuna wasomaji wangu hawajapatapo kusikia kitu kinaitwa Thomas Cooke Travellers Cheque.

Hii ni hundi ambayo msafiri alikuwa anapewa na afikapo safari yake atavunja kupata dollars, pounds nk.

Kulikuwa na kibali cha Wizara husika, kibali cha Ikulu nk. nk. kiasi kuwa hadi umemaliza kupata vibali vyote hivyo mtu unakuwa taaban kwa kuchoka.

Ukiingia tu kwenye ndege hata kabla haijaruka umeshalala kwa uchovu na si kama natia chumvi mimi mwenyewe yamenitokea mara nyingi tu.

Kusafiri ilikuwa shughuli pevu.

Nasafiri kwenda Harare Mwezi Mtukufu wa Ramadhani ndege Air Tanzania Corporation (ATC) wenyewe ndege hii tukiipa majina kadha wa kadha lakini mimi nililipenda jina la Twiga.

Ndege ya alfajir saa 12 kwa hiyo nimefika uwanjani kumi ya usiku.

Tumetua Harare na haukupita muda niko nje ya uwanja na ndani ya teksi inanipeleka mjini.

Madereva wa taxi wanajua mengi sana kuanzia ''rate,'' ya ''dollar black market,'' hadi hoteli nzuri kwa malazi na chakula.

Dereva wa taxi namuuliza kuhusu msikiti uliopo mjini jirani na hoteli yangu ''Ambassador Hotel.''

Mimi na dereva wa taxi tunazungumza Kiingereza na natumia neno. ''mosque,'' neno hili halipo katika msamiati wake wa Kiingereza.

Nimejitahidi sana kumuelewesha lakini hakunielewa.
Mwisho nikamwambia, ''the place where Muslims pray.''

''Oh! You mean Muslim church I will show you!''

Nikapumua na kweli akanipitisha kwenye huo msikiti nikauona.

Niko Ambassador Hotel, katikati ya mji.

Tarweh nikawa nasali kwenye huu msikiti lakini wengi wa waumini ni Wahindi na Waafrika wachache kutoka kabila la Wayao.

Meneja wa hoteli akawa hanioni kwenye chai asubuhi akanitafuta kutaka kujua kwa nini siendi kunywa chai kwenye dining room ya hoteli.

Kaniuliza tena kwa masikitiko.
Nikamfahamisha kuwa nimefunga Mwezi wa Ramadhani.

Yule Bwana Meneja wala hajui Ramadhani ni kitu gani lakini akaniambia kuwa kuanzia siku hiyo atamfahamisha ''Chef,'' yaani mpishi wa hoteli anitayarishie futari jioni kama fidia ya ya chai ya asubuhi na itakuwa, ''Room Service,'' futari italetwa chumbani kwangu tena, "on the house,'' yaani hawatanitoza chochote.

Furaha yangu haisemeki.

Jioni ile ulipotimu muda wa kufungua nikapiga simu,''Room Service,'' na haukupita muda mlango ukagongwa na futari ikaletwa imefunikwa vizuri sana.

Ikafunuliwa na kwa hakika ule muonekano wake ulinivutia kupita kiasi.

Chakula na vinjywaji vilikuwa vimepangika vyema.

Lakini katika kutupa jicho nikaona kuna nyama ina rangi nyeupe inayokwenda kwenye wekundu na imekatwa ''slice,'' nyembamba iliyoviringika.

Yule bint aliyeleta futari ile alikuwa bado hajatoka mle chumbani kasimama ananiangalia ninavyokitazama chakula kile.

Nikamuuliza kuhusu ile nyama kuwa ni nyama gani?

Jibu alilonipa lilinishtua.

''This is pork sir.''

Kanifahamisha kuwa ile nyama ilikuwa nguruwe.

Futari ya nguruwe.

Kwa utaratibu nilimuomba aondoe chakula chote kile akirudishe jikoni.

Nilihama siku ya pili nikahamia hoteli nyingine inaitwa Holiday Inn.

Kusafiri hakika ni elimu tosha.
Waislam wenzako wa huko wanakula ndo maana wakukuletea.ulitakiwa useme wewe hutumii km wenzako!
 
Siku hizi mambo yamebadilika sana duniani na neno "Halal" limekuwa maarufu kwa kila ndege na baadhi ya hotels
Neno halal linaandikwa sehemu nyingi kuliko vegetarian
Lakini sikushangaa sana kwa ftari ya pork kwani hukuwatahadharisha kuwa wewe huli huyo mdudu
hata vyombo vinavyotumika kupikia pork at same time vyakula vingine basi vyote ni haram
 
hata vyombo vinavyotumika kupikia pork at same time vyakula vingine basi vyote ni haram
Ni haram ndio, hilo halina mjadala huwezi kuwa na nguruwe haram na mafuta yake halali come on lets be honest
 
MFUNGO WA RAMADHANI KATIKA MJI WA HARARE ZIMBABWE

Zamani ilikuwa ukiwa na safari unahitaji vibali kadhaa ili uweze kusafiri, iwe safari ya kikazi au vinginevyo.

Kwanza utahitaji kibali cha Benki Kuu ili uweze kupata fedha za kigeni.

Naamini kuna wasomaji wangu hawajapatapo kusikia kitu kinaitwa Thomas Cooke Travellers Cheque.

Hii ni hundi ambayo msafiri alikuwa anapewa na afikapo safari yake atavunja kupata dollars, pounds nk.

Kulikuwa na kibali cha Wizara husika, kibali cha Ikulu nk. nk. kiasi kuwa hadi umemaliza kupata vibali vyote hivyo mtu unakuwa taaban kwa kuchoka.

Ukiingia tu kwenye ndege hata kabla haijaruka umeshalala kwa uchovu na si kama natia chumvi mimi mwenyewe yamenitokea mara nyingi tu.

Kusafiri ilikuwa shughuli pevu.

Nasafiri kwenda Harare Mwezi Mtukufu wa Ramadhani ndege Air Tanzania Corporation (ATC) wenyewe ndege hii tukiipa majina kadha wa kadha lakini mimi nililipenda jina la Twiga.

Ndege ya alfajir saa 12 kwa hiyo nimefika uwanjani kumi ya usiku.

Tumetua Harare na haukupita muda niko nje ya uwanja na ndani ya teksi inanipeleka mjini.

Madereva wa taxi wanajua mengi sana kuanzia ''rate,'' ya ''dollar black market,'' hadi hoteli nzuri kwa malazi na chakula.

Dereva wa taxi namuuliza kuhusu msikiti uliopo mjini jirani na hoteli yangu ''Ambassador Hotel.''

Mimi na dereva wa taxi tunazungumza Kiingereza na natumia neno. ''mosque,'' neno hili halipo katika msamiati wake wa Kiingereza.

Nimejitahidi sana kumuelewesha lakini hakunielewa.
Mwisho nikamwambia, ''the place where Muslims pray.''

''Oh! You mean Muslim church I will show you!''

Nikapumua na kweli akanipitisha kwenye huo msikiti nikauona.

Niko Ambassador Hotel, katikati ya mji.

Tarweh nikawa nasali kwenye huu msikiti lakini wengi wa waumini ni Wahindi na Waafrika wachache kutoka kabila la Wayao.

Meneja wa hoteli akawa hanioni kwenye chai asubuhi akanitafuta kutaka kujua kwa nini siendi kunywa chai kwenye dining room ya hoteli.

Kaniuliza tena kwa masikitiko.
Nikamfahamisha kuwa nimefunga Mwezi wa Ramadhani.

Yule Bwana Meneja wala hajui Ramadhani ni kitu gani lakini akaniambia kuwa kuanzia siku hiyo atamfahamisha ''Chef,'' yaani mpishi wa hoteli anitayarishie futari jioni kama fidia ya ya chai ya asubuhi na itakuwa, ''Room Service,'' futari italetwa chumbani kwangu tena, "on the house,'' yaani hawatanitoza chochote.

Furaha yangu haisemeki.

Jioni ile ulipotimu muda wa kufungua nikapiga simu,''Room Service,'' na haukupita muda mlango ukagongwa na futari ikaletwa imefunikwa vizuri sana.

Ikafunuliwa na kwa hakika ule muonekano wake ulinivutia kupita kiasi.

Chakula na vinjywaji vilikuwa vimepangika vyema.

Lakini katika kutupa jicho nikaona kuna nyama ina rangi nyeupe inayokwenda kwenye wekundu na imekatwa ''slice,'' nyembamba iliyoviringika.

Yule bint aliyeleta futari ile alikuwa bado hajatoka mle chumbani kasimama ananiangalia ninavyokitazama chakula kile.

Nikamuuliza kuhusu ile nyama kuwa ni nyama gani?

Jibu alilonipa lilinishtua.

''This is pork sir.''

Kanifahamisha kuwa ile nyama ilikuwa nguruwe.

Futari ya nguruwe.

Kwa utaratibu nilimuomba aondoe chakula chote kile akirudishe jikoni.

Nilihama siku ya pili nikahamia hoteli nyingine inaitwa Holiday Inn.

Kusafiri hakika ni elimu tosha.
Pole kwa changamoto mkuu!
 
Wahenga walinena. MSAFIRI KAKILI {KATILI} TEMBEA UJIONEE...
YUTILIBU LIELIMU WALA BISWIIN FAINNAL ELIM FARADHII ALA KUL MUSLIM...
 
Mohamed Said uliwakosea fadhila. Kama ulivyomvumilia dereva taxi hadi akasema ''muslim church'' ndivyo hivyo ungewaambia waondoe chakula na kuwaeleza ni kwanini

Kufanya hivyo kungemsaidia Meneja siku nyingine ya ugeni aelewe nini cha kufanya au kuuliza

Nia na dhamira yao ilikuwa njema kabisa, mapungufu ya uelewa hayawafanyi wawe na makosa

Hiyo ilikuwa fursa ya kutoa darsa na si kuhamia hoteli nyingine
 
Back
Top Bottom