Mfungwa akutwa uraiani na SMG

Mfungwa akutwa uraiani na SMG

Pragmatist

Member
Joined
Sep 21, 2012
Posts
18
Reaction score
1
Inatisha! Aliyefungwa miaka 15 kukutwa uraiani tena akiwa na silaha za kivita. Magereza wanafanya nini? Haya ndiyo makandokando ya rushwa. Kama kawaida yetu Watanzania hakuna atakayewajibika! Serikali mpo?

==========

MFUNGWA anayetumikia kifungo cha miaka 15 jela alichohukumiwa mwaka 2010, Masanja Maguzu (42), amekuwa akiishi uraiani baada ya kutoka gerezani katika mazingira ya kutatanisha.

Akisimulia mkasa huo jana, Kamanda wa Polisi mkoani Simiyu, Salum Msangi alisema awali wa Polisi ilikuwa ikimchunguza mke wa Maguzu, Holo Mabuga (30) ambaye alipatikana akimiliki silaha ya kivita kinyume cha sheria.

Mwanamke huyo kwa mujibu wa Kamanda Msangi, alikamatwa Novemba 6 mwaka huu akiwa na silaha ya kivita aina ya G 3 ikiwa na risasi zake 36 na risasi zingine 96 za bunduki aina ya SMG.

Baada ya kumkamata mwanamke huyo, Kamanda Msangi alisema waligundua kuwa hakuwa peke yake katika matumizi ya silaha nzito na ya kivita kama hiyo, bali nyuma yake kulikuwa na mtandao au kundi la watu waliokuwa wakishirikiana naye kuzitumia silaha hizo katika matukio ya ujangili na uporaji wa kutumia silaha bila kujua ni mumewe.

Kamanda Msangi alisema, kutokana na hali hiyo polisi waliandaa mtego ili kubaini mtu au watu waliokuwa kwenye mtandao huo wa uhalifu waliokuwa wakishirikiana na mwanamke huyo.

Kutokana na mtego huo, siku kumi baada ya kumkamata mke wa mfungwa huyo, polisi walimkamata Maguzu akiwa nyumbani kwake katika Kijiji cha Ng'wang'wali wilayani Itilima katika Mkoa wa Simiyu.

Maguzu alikutwa na silaha ya kivita aina ya SMG, risasi 31 na magazine tatu ambazo moja ya magazine hizo ni ya bunduki aina ya Uzi Gun ya Israel.

Kamanda Msangi alisema kupatika kwa magazine hiyo kunathibitisha kwamba kuna bunduki nyingine aina ya Uzi Gun ambayo matumizi yake ni sawa na SMG, iko mikononi mwa mtandao wa wahalifu na watu wabaya.

Alisema kama haitapatikana haraka, silaha hiyo itaendelea kusumbua na kuhatarisha usalama wa maisha ya wananchi na mali zao na hata wanyama katika hifadhi za wanyama pori.

Kutokana na utata huo, Kamanda Msangi alisema wanafanya uchunguzi wa kina ili kubaini sababu za kuachiwa na kuwa huru kwa mfungwa huyo hatari aliyepatikana na hatia ya kupatikana na silaha na kuhukumiwa na Mahakama adhabu ya kifungo cha miaka 15 jela mwaka 2010.

Maisha ya askari

''Mimi kinachonisikitisha zaidi ni jinsi baadhi ya watu wanavyohatarisha usalama kwa kuwaachia huru wahalifu sugu na hatari kama huyo. Wakati sisi polisi hatulali na tunauza roho zetu kupambana na uhalifu hasa wa kutumia silaha nzito kama hizo, baadhi ya watu wanakwamisha jitihada zetu kwa kuwaachia huru wahalifu hao katika mazingira ya kutatanisha.

"Lakini hili la safari hii hatutalifumbia macho mpaka wale wote walioshirikiana naye wabainike na kuwajibishwa kwa mujibu wa sheria, mimi nimekula kiapo sintakubali kurudi nyuma,'' alionya.
 
Funguka vizuri Pragmatist kwani Mi naona bado post yako ina mapungufu.

1)Wapi?
2)Ilikuwaje?
 
Last edited by a moderator:
Weka basi nyama za kutosha ili habari yako ieleweke mkuu
 
Hueleweki japo ilitokea indonesia miaka ya nyuma, wakasema(mafisadi) huyo tajiri aliyefungwa alipewa likizo kidogo
 
Wapi na alifungwa gereza gan? Ni nani huyo? Funguka mkuu!
 
Mambo gani sasa haya ya kuweka habari nusu nusu? Nani huyo mtu?alifungwa kwa kosa gani?gereza gani na wapi? na amekutwa na silaha sehemu gani? baada ya kukutwa amechukuliwa hatua gani? Na alikuwa anafanya nini na hiyo silaha hapo alipokutwa nayo?
 
Labda ameshinda kwa rufaa maana ushahidi wa polisi huwa haufiki mbali watuhumiwa wengi sana wa makosa makubwa huwa wanashinda rufaa zao!!
 
chunguza kwanza habari hiyo ina kasoro,
 
ndio uzuri wa rushwa. Rushwa huvunja mapingu na makufuli ya gerezani
 
Ukiwa na hela gerezani mbona unaingia na kutoka kama 'lodge?
 
huyu jamaa ni hatari sana. kwa mtandao huo wengi wanatoka kwa staili hii ya rushwa
 
Jeshi la Polisi mkoani Simiyu, linamshikilia mkazi wa kijiji cha Ng’wang’wali, Wilaya ya Itilima, aliyekuwa akitumikia kifungo cha miaka 15 gerezani akiwa na silaha ya kivita.

Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Simiyu, Salum Msangi, alimtaja mfungwa huyo aliyekamatwa juzi na silaha hiyo kuwa ni Masanja Maguzu (42).

Kwa mujibu wa Kamanda Msangi, Maguzu alikamatwa na bunduki aina ya Sub Machine Gun (SMG) ikiwa na risasi 31 nyumbani kwake.

Kamanda Msangi alisema hayo alipozungumza na waandishi wa habari kwa njia ya simu jana kutoka wilayani Bariadi.

Alisema kwa mara ya kwanza Maguzu alikamatwa na bunduki aina ya SMG na risasi 622 mwaka 2010 na kufikishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi mkoani Shinyanga na kuhukumiwa adhabu ya kifungo cha miaka 15 gerezani baada ya kupatikana na hatia.

Hata hivyo, alisema katika hali isiyokuwa ya kawaida, jeshi hilo tena limemkamata mfungwa huyo akiwa uraiani.

Kamanda Msangi alisema mbali na bunduki, pia alikamatwa na magazini tatu na risasi 31 za SMG kinyume cha sheria.

Alisema bunduki hiyo anatuhumiwa kuifanyia vitendo vya kihalifu na ujangili katika Hifadhi ya Taifa ya Serengeti na Pori la Akiba la Maswa.

Kamanda Msangi alisema jeshi lake linaendesha uchunguzi wa kina ili kufahamu mazingira yaliyosababisha mfungwa huyo kuwa nje ya gereza baada ya kuhukumiwa adhabu hiyo.

Alisema Novemba 6, mwaka huu, polisi walimkamata mke wa mfungwa huyo aliyetambuliwa kwa jina la Holo Mabuga (30), akiwa na silaha nyingine ya kivita aina ya G3.

Kamanda Msangi alisema silaha hiyo ilikamatwa ikiwa na risasi zake 36 pamoja na risasi nyingine zinazotumika katika bunduki aina ya SMG.

Siku 10 baada ya kukamatwa kwa mwanamke huyo, polisi walifanikiwa kumnasa mumewe, ambaye ni mfungwa aliyeaminika yumo gerezani akitumikia adhabu yake ya kifungo cha miaka 15 akiwa na silaha hiyo ya SMG na risasi 31 na magazini tatu; moja hutumika katika bunduki aina ya Uzi gun ya Kiisraeli.

“Jamani, tukio hili limetushitua na kutusikitisha sana. Maana wakati tukipambana na kukabiliana na vitendo vya uhalifu na wahalifu, bado kuna watu wengine wanakwamisha juhudi zetu sisi polisi. Mfungwa huyu kila mmoja hapa mkoani anaelewa kuwa yuko gerezani anatumikia adhabu yake. Ajabu leo amekutwa tena uraiani akiendelea na vitendo vyake vile vile. Je, tutashindwa kulaumiwa kuwa tunakula na wahalifu?” Alihoji Kamanda Msangi na kuongeza:

“Haiwezekani mfungwa aliyehukumiwa kutumikia jela miaka 15 kwa muda mfupi hivi akawa nje hata kama ni kwa msamaha. Ni muda mfupi sana na hasa ikilinganishwa na kosa lenyewe. Maana ni la kupatikana na silaha tena ya kivita. Na iliyokuwa ikitumika kwa vitendo vya kijambazi na ujangili ndani ya hifadhi, hii inaonyesha kuna namna imefanyika. Na sisi tunaendelea kuchunguza kujua ukweli wa jambo hili.”

Alisema inawezekana mfungwa huyo alitoka gerezani katika mazingira ya kutatanisha, lakini bado aliendelea kujihusisha na vitendo vya uhalifu kwa kutumia silaha za kivita, kinyume cha sheria na mitego ya polisi ilifanikiwa kumnasa baada ya kumkamata mkewe, ambaye pia alikutwa akiwa na silaha nzito za kivita.

Alisema uchunguzi wa awali wa polisi ulibaini kuwa mke wa mfungwa huyo, Holo Mabuga, pamoja na kupatikana akiwa na silaha hizo za kivita kinyume cha sheria, hakuwa peke yake katika matumizi ya silaha hizo, bali nyuma yake kulikuwa na kundi la watu aliokuwa akishirikiana nao.

Kamanda Msangi alisema kupatikana kwa magazini ya Uzi gun, kunathibitisha kwamba, bunduki yake, ambayo matumizi yake ni sawa ya SMG, bado iko mikononi mwa mtandao wa wahalifu na watu wabaya.

Alisema kama haitapatikana haraka itaendelea kusumbua wananchi na kuhatarisha usalama wa maisha na mali zao na hata wanyama katika hifadhi za wanyamapori.

NIPASHE iliwasiliana kwa njia ya simu jana na Msemaji wa Jeshi la Magereza nchini, Omary Mtiga, kutaka aeleze mfungwa huyo aliondokaje gerezani na kurudi uraiani lakini alisema hakuwa na taarifa hizo.

“Mimi sina taarifa. Niandikie meseji (ujumbe mfupi wa simu ya mkononi (sms) ili nifuatilie huko Simiyu kujua ni gereza gani alilokuwa akitumikia kifungo hicho,” alisema Mtiga.

Naye Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Isaac Nantanga, aliomba apewe kufuatilia suala hilo.

“Nami nitafuatilia kesho (leo) kujua kulikoni,” alisema Nantanga.

MWENYEKITI CCM MATATANI

Kikosi maalum cha Mali Asili na Misitu cha kukusanya maduhuli ya serikali kwa kushirikiana na Jeshi la Polisi mkoani Geita, kimekamata magogo na mbao yakiwa yamepakizwa kwenye gari la abiria linalodaiwa kuwa mali ya Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Geita, Joseph Kasheku maarufu kama Msukuma.

Mbao na magogo vilikamatwa Novemba 16, mwaka huu vikiwa vimepakizwa katika gari la abiria lenye namba za usajili T 517 BBJ.

Kiongozi wa kikosi cha ukusanyaji wa maduhuli katika mikoa ya Mwanza na Mara, Ngatara Kimaro, alisema magogo na mbao hizo vilikuwa vikisafirishwa kutoka Runzewe katika Wilaya ya Bukombe kwenda jijini Mwanza.

Alisema kikosi hicho kilipata taarifa kutoka kwa wenzao kwamba kulikuwa na mbao na magogo vikisafirishwa kinyemela.

Alisema dereva wa basi hilo aliposimamishwa njiani alikataa hadi kwenye karakana ya mabasi hayo iliyopo eneo la Natta jijini Mwanza.

Kimaro alisema walipofika kwenye karakana, walijitambulisha na wakawaomba watumishi wa gari hilo wafungue buti ili wafanye ukaguzi, lakini walikataa kwa madai kuwa mhusika mwenye funguo hakuwapo.

Alisema baadhi ya wafanyakazi walifungua tairi moja na kuondoa laini za breki wakati maofisa hao wakitafuta namna ya kufanya huku wakiwasiliana na Jeshi la Polisi kwa ajili ya kupata askari.

Kimaro alisema wakati wakisubiri askari wafike, ghafla lango la kuingia ndani ya karakana lilifunguliwa kisha gari hilo likaingizwa ndani na askari polisi walifika eneo hilo saa 11:00 jioni kusimamia ukaguzi huo.

“Askari walipofika mmoja wa wafanyakazi alikubali kufungua buti ya gari, tukakuta mbao na magogo yamepangwa kwa ustadi mkubwa, mbao nyingine ziliwekwa ndani ya basi chini ya uvungu wa viti vya abiria na kwenye juu ya basi,” alisema Kimaro.

Alisema mbao hizo hazikuwa na nyaraka zozote za uhalali wa usafirishaji wake na walipozikagua, zilionekana kuvunwa kinyume cha sheria na hazikuwa na alama ya misitu.

Alisema kwa kushirikiana na polisi, waliingia ndani ya karakana hiyo kupitia lango dogo na kufanya upekuzi na kuzikuta mbao zikiwa katikati ya viti vya abiria.

“Tulifanikiwa kuchukua baadhi ya mbao ambazo tuliondoka nazo kama kielelezo. Gari hatukuondoka nalo lilibaki kwenye karakana kwa sababu tuliambiwa dereva hayupo,” alisema.

Mmiliki wa basi hilo, Msukuma, alithibitisha gari lake kukamatwa likiwa na mbao, lakini akawatuhumu maofisa misitu kwamba walichukua hatua hiyo ya kukamata gari hilo baada ya kushinikiza wapewe rushwa.

Msukuma alisema kwa mujibu wa sheria za usafirishaji, gari lake linaruhusiwa kusafirisha mizigo na abiria inayoshindikana kupakiwa kwenye buti inapakiwa kwenye lori.

“Ni kweli nina taarifa kama hizo, lakini wao wamekamata mbao siyo gari, kazi ya gari langu ni kusafirisha abiria na mizigo yao, lakini kikubwa ni kwamba polisi walipiga simu kwa maafisa wa maliasili baada ya kunyimwa rushwa kutokana na njaa njaa zao,” alidai.

Msukuma alisema suala la kutokuwa na nyaraka linahusu kitengo kingine na kupakia mbao ni suala lingine na kuhoji kuwa kwa nini walishindwa kulikamata basi hilo kutoka Ushirombo hadi liingie jijini Mwanza ambapo kuna vituo tisa vya ukaguzi?”

Alisema anajiandaa kufungua kesi dhidi ya polisi ambao walivunja lango kuu la kuingilia kwa ajili ya kufanya upekuzi na kisha wakafanya uporaji nyumbani kwake.

Alipotakiwa kutoa ufafanuzi wa kupakia mbao chini ya uvungu wa viti vya abiria wakati sheria inakataza, alisema ni kosa na uzembe wa askari wa Kikosi cha Usalama Barabarani.

Kuhusu vibali vya kumruhusu kusafirisha mbao na magogo, alidai suala hilo si lake bali mteja mwenye mbao.

Kaimu Kamanda wa Polisi mkoani Mwanza, Lilian Matola, alisema hakuwa na taarifa hizo.

Imeandaliwa na Stephen Wang’anyi, Simiyu, Juma Ng’oko, Mwanza na Muhib Said, Dar.




CHANZO: NIPASHE

 
Hilo ni dili la bwana jela na wakuu wa magereza wanaotumia wafungwa kufanya uhalifu uraiani,haiwezekani mfungwa aliyehukumiwa kuwa huru then anaendelea kufanya uhalifu, kunahaja ya kuchunguza uadilifu wa maofisa wa magereza!
 
Back
Top Bottom