Allen Kilewella
JF-Expert Member
- Sep 30, 2011
- 21,470
- 40,593
Ujasiriamali siyo kitu rahisi hata kidogo na ndiyo maana uchumi kama wa Marekani unadhibitiwa na watu wasiofikia kumi. Kama ni kusoma ama kuona fursa unajiuliza hivi mtu wa Marekani na Tanzania kwa uwiano kupi kuna wasomi na waona fursa wengi!?
Ni kweli ni lazima vijana wajifunze kufanya kazi ili wajitegemee lakini si kweli kwamba kila mtu kwenye kila jamii atafanikiwa kuwa sawa na wengine waliofanikiwa. Tatizo hao "Motivational/Inspirational speakers" huwa mafundisho yao yanaonesha kufanikiwa kupo kwa kila mtu na wasiofanikiwa ni kwa kuwa hawajajaribu ama kuthubu.
Kuwa na mali na kufanya kile unachokipenda na kukiamini ni vitu viwili tofauti. Tatizo kwenye jamii yetu maskini ni wengi sana kiasi kwamba akitokea mtu na porojo za kufanikiwa wengi hupata kichaa cha kujilamu kuchelewa au kujiona wana ujinga wa kutokujuja mambo na kuamini kuwa wana hofu ya kuthubutu kuyatafuta mafanikio.
Hao magwiji wa kuhamasisha wenyewe ukiwachunguza sana ni wakwepaji wakubwa sana wa kodi. Hivi yale makongamano na semina wanazoziendesha huwa wanalipa kodi kweli??
Ni kweli ni lazima vijana wajifunze kufanya kazi ili wajitegemee lakini si kweli kwamba kila mtu kwenye kila jamii atafanikiwa kuwa sawa na wengine waliofanikiwa. Tatizo hao "Motivational/Inspirational speakers" huwa mafundisho yao yanaonesha kufanikiwa kupo kwa kila mtu na wasiofanikiwa ni kwa kuwa hawajajaribu ama kuthubu.
Kuwa na mali na kufanya kile unachokipenda na kukiamini ni vitu viwili tofauti. Tatizo kwenye jamii yetu maskini ni wengi sana kiasi kwamba akitokea mtu na porojo za kufanikiwa wengi hupata kichaa cha kujilamu kuchelewa au kujiona wana ujinga wa kutokujuja mambo na kuamini kuwa wana hofu ya kuthubutu kuyatafuta mafanikio.
Hao magwiji wa kuhamasisha wenyewe ukiwachunguza sana ni wakwepaji wakubwa sana wa kodi. Hivi yale makongamano na semina wanazoziendesha huwa wanalipa kodi kweli??