chakii
JF-Expert Member
- Sep 15, 2013
- 20,834
- 26,217
MGAHAWA wa wasanii wa vichekesho wa Kundi la Orijino Komedi (OK), umejipatia umaarufu mkubwa na kujizolea idadi kubwa ya watu, wanaohudhuria Maonyesho ya Kimataifa ya Biashara ya Dar es Salaam ‘Sabasaba' yanayofanyika kwenye viwanja vya Mwalimu Nyerere, jijini Dar es Salaam.
Tanzania Daima ambalo lilitembelea katika viwanja hivyo, lilikuta watu wakipigana vikumbo kuingia katika mgahawa huo kupata huduma mbalimbali, huku watoto wakionekana kuvutiwa zaidi.
Akizungumza na Tanzania Daima, mmoja wa wasanii wanaounda kundi hilo, Lucas Mhuvile ‘Joti', alisema wamebuni biashara hiyo kama moja ya njia za kuliingizia kundi hilo kipato na kingine kuweza kukutana na mashabiki wao ambao wamekuwa wakiwaona tu kwenye runinga.
Katika shughuli hiyo, Joti alisema wamegawana majukumu ambapo yeye yupo upande wa kushika fedha (mhasibu), wakati upande wa mapokezi yupo Alex Chalamila ‘Mc Regan', huku Mjuni Silvery ‘Mpoki' na Emmanuel Mgaya ‘Masanja' wakiwa katika idara ya upishi.
Kwa mujibu wa Joti, wanajisikia faraja wananchi wanapokwenda katika mgahawa huo kupata huduma na kufurahi nao pamoja, jambo linalowafanya watambue kwamba bado wanakubalika na Watanzania, licha ya kuwepo kwa makundi mengi ya uchekeshaji nchini.
Joti alitumia fursa hiyo kuwataka mashabiki wake kumuunga mkono katika kununua filamu yake ya ‘Kapu la Babu' aliyoiachia sokoni mwezi uliopita, ambayo pia inapatikana katika mgahawa wao huo.
Kutokana na ubunifu mkubwa alioufanya katika kutengeneza filamu hiyo, alisema mtu atakayeinunua hatajutia hela yake.
Source:Tanzania Daima
Tanzania Daima ambalo lilitembelea katika viwanja hivyo, lilikuta watu wakipigana vikumbo kuingia katika mgahawa huo kupata huduma mbalimbali, huku watoto wakionekana kuvutiwa zaidi.
Akizungumza na Tanzania Daima, mmoja wa wasanii wanaounda kundi hilo, Lucas Mhuvile ‘Joti', alisema wamebuni biashara hiyo kama moja ya njia za kuliingizia kundi hilo kipato na kingine kuweza kukutana na mashabiki wao ambao wamekuwa wakiwaona tu kwenye runinga.
Katika shughuli hiyo, Joti alisema wamegawana majukumu ambapo yeye yupo upande wa kushika fedha (mhasibu), wakati upande wa mapokezi yupo Alex Chalamila ‘Mc Regan', huku Mjuni Silvery ‘Mpoki' na Emmanuel Mgaya ‘Masanja' wakiwa katika idara ya upishi.
Kwa mujibu wa Joti, wanajisikia faraja wananchi wanapokwenda katika mgahawa huo kupata huduma na kufurahi nao pamoja, jambo linalowafanya watambue kwamba bado wanakubalika na Watanzania, licha ya kuwepo kwa makundi mengi ya uchekeshaji nchini.
Joti alitumia fursa hiyo kuwataka mashabiki wake kumuunga mkono katika kununua filamu yake ya ‘Kapu la Babu' aliyoiachia sokoni mwezi uliopita, ambayo pia inapatikana katika mgahawa wao huo.
Kutokana na ubunifu mkubwa alioufanya katika kutengeneza filamu hiyo, alisema mtu atakayeinunua hatajutia hela yake.
Source:Tanzania Daima