Mgambo wavamia Majumbani Kimara Mavurunza na Kutishia,Kukamata watu na Kuomba Rushwa

Mgambo wavamia Majumbani Kimara Mavurunza na Kutishia,Kukamata watu na Kuomba Rushwa

MR.NOMA

JF-Expert Member
Joined
Feb 1, 2014
Posts
339
Reaction score
505
Habari za Leo ndugu zangu, Nimeumizwa na kusononeshwa Sana na tukio lililotokea Leo Majira ya saa 5-6 mchana Jijini Dar - Mtaa wa Kimara Mavurunza, mita chache tu ukitoka kimara DAWASCO kuelekea Kimara Mavurunza.

Vijana wapatao watano wakiwa wamevalia magwanda ya kijani ambapo inasadikiwa kuwa ni migambo waliotumwa na Serikali ya mtaa walivamia nyumba kadhaa katika mtaa huo na kuwaeleza wenye nyumba kuwa wanakagua usafi wa mazingira badae walikuwa wakali Huku wakitishia kuwapeleka watu polisi na waliwaambia watu kuwa Bora watoe Hela elf 50 la sivyo wakienda polisi watatoa zaidi ya laki 2 ili kuwa huru.

Bahati nzuri hakuna mtu aliyetoa pesa yeyote baada ya hapo mgambo hao walikamata watu kadhaaa wasio na hatia ambao pia walishindwa kuwakimbia wakimwemo Ma house girl.

Taarifa nilizonazo ni kuwa watu hawa walienda wakafungiwa katika ofic za mtaa huo na mashahidi wakiwemo vijana waliokamatwa wanasema Wanasema kuwa Walipokuwa kwenye chumba walichohifadhiwa walisikia mgambo na viongozi wa mtaa wakizozana juu ya kuwa wamekamata watu wasio na maana hivyo hawataweza fanikisha Nia Yao. Kiukweli na laani sana tukio hili na nimekwazika sana kwa kilichotokea.

Naomba uongozi wa kata ya saranga Kimara na wilaya ya Ubungo hasa Mkuu wa wilaya utusaidie kufatilia na kuwawajibisha kikundi hiki haramu ambacho kimeleta tafrani na usumbufu kwa raia kwa kutaka kujipatia fedha isivyo halali.

Mgambo Gani Hana kitambulisho na Wala hajaongozana na uongozi wa mtaa.Anatofauti Gani na jambazi?
 
Kama ni kweli ni upuuzi wa hali ya juu. Mjiunge wote mwende panoja kwenye ofisi zao kudai wawajibishwe ili wasifanye mambo kama hayo tena.

Serikali ipo kwa ajiri ya kuwalinda na kuwasaidia wananchi.

Nguvu kubwa sana kwa swala dogo la usafi, labda hujaeleza kila kitu, kwanini nyumba hizo tu, kuna uchafu unaoathiri wengi sana?
 
Sasa hivi wamepewa makombati mapyaaaaa tena ya kijani,KWA Sasa Wana KAZI ya kufanya maana JPM aliwastaafisha KWA lazima na in short hawakua na KAZI tena.Mambo yaleee ya awamu ile yamerudi
 
Huku juzi wamevamia na polisi mmoja na hio kamata kamata inaendelea mpaka leo hii
Ukifikishwa wanataka 50 na makosa sio hayo tu ni jambo tu lolote wakijiskia yani kwakweli ni huzuni sana

Sent from
 
Huku juzi wamevamia na polisi mmoja na hio kamata kamata inaendelea mpaka leo hii
Ukifikishwa wanataka 50 na makosa sio hayo tu ni jambo tu lolote wakijiskia yani kwakweli ni huzuni sana

Sent from
Hahahahha waje walete ungese kitaani watajua hawajui yani😅
 
Ila wanachokifanya ni kitu hatari Kwa usalama wao na Raia pia maana wanatumia nguvu nyingi na ubabe kuliko akili,nashauri mamlaka zinazohusika na Hawa migambo zione namna nzuri ya kuwatumia kwa uzuri sio kuwatuma wenyewe TU. Kwanza migambo wananjaa sana, wanaomba rushwa bila aibu, wanaweza wakaanzia elf 50 ila ukiwambia una elf 5 wanachukua.
 
Niliwahi kumdindia mgambo kipindi niko Mwanza,amekuja na pingu kabisa nikamuuliza kitambulisho kwanza kabla ya mambo yote akawa hana nikamwambia umevaa kiraia na unasema we ni mgambo m nikuamini vipi,bahati nzuri nilikua kitaa kabisa na karibu na kijiwe cha boda...aliondoka kanyong'onyea sana (Ningemtaja hadi jina na mahali sema sheria za JF haziruhusu),ila ni moja wa migambo wanaosemwa kwa ubaya sana eneo hilo
 
Back
Top Bottom