heaven on desert
JF-Expert Member
- Jan 25, 2013
- 1,025
- 393
We Diamond, usijifanye chizi! wasanii wooote hutegemea tunguri kuvuta nyota lakini huu ndio mwisho wako!
Si ndo hapo.
Mganga hajui hata ethics za kuweka siri za wateja wake?
Basically kawaambia wengine wote waliokuwa wanafikiria kwenda kwake kwamba wakiingia kwenye database anaweza kuwaumbua muda wowote.
Kama kamfukizia mvuto Diamond mbona yeye hana mvuto kwa Diamond.
MGANGA WA DIAMOND AJITOKEZA
by Teen Newz
1 hour ago
Ustadhi Yahya Michael, mkazi wa
Dar, hivi karibuni amejitokeza na
kudai kuwa yeye ndiye mganga
aliyempaisha mwanamuziki Nasibu
Abdu Diamond Platnumz ambaye
kwa sasa ni kinara wa Bongo Fleva,
Risasi Jumamosi lina mkanda
kamili.
MH! SIKU HIZI ANAJIFANYA
SUPASTAA
Akizungumza na gazeti hili katika
mahojiano maalum maeneo ya
Magomeni, Dar, mganga huyo
alidai kuwa pamoja na jitihada
kubwa alizofanya kumpaisha
Diamond lakini anamshangaa kwa
kuwa amesahau alikotoka na
anajifanya supastaa.
Alidai kuwa siku hizi akimpigia
simu, Diamond huwa hapokei,
tofauti na zamani alipokuwa
akihangaika kuchomoka kisanii.
Mganga huyo alifunguka kuwa
sababu ya kufanya hivyo ni baada
ya kuchukuliwa na watu
waliompeleka kwa waganga wa
Kigoma ambako anajidanganya
kuwa ndiyo wanampaisha kumbe
walimchukua akiwa
ameshampandisha kwa kumpa
dawa kali za mvuto.
ALIMPA DAWA GANI?
Alizitaja dawa alizompatia
Diamond kuwa ni mitishamba aina
ya Dubi, Ntajamasala (hii humfanya
watu wamuogope na
kumheshimu), Italigula,
Nkangacharo na Kalila Lila (ambayo
huichoma na kuoga kwa ajili ya
kuwavutia watu).
ANGUKO LA DIAMOND
Alidai kuwa Diamond amejisahau
na hajui kama anguko lake linakuja
kufuatia ahadi aliyoiweka wakati
anaanza kuimba baada ya
kumpatia dawa hivyo atapotea
kwenye muziki.
Akielezea historia ya kukutana
kwao, Ustadhi Yahya alisema yeye
na staa huyo walikutana miaka ya
2000 nyumbani kwa Papaa Misifa
ambaye alikuwa meneja wa
Diamond.
Alidai kuwa kubadilika kwa
Diamond kulikuja baada ya kutwaa
tuzo tatu za Kili mwaka 2010 ndipo
akawa anahusudu wanawake
tofauti na masharti ya dawa
japokuwa alimkanya lakini
hakumsikia.
DIAMOND ANASEMAJE?
Kama ilivyo desturi ya gazeti hili,
lilimgeukia Diamond ili kupata
mzani wa habari hiyo ambapo
alipopatikana kwa njia ya simu
alisomewa maelezo yake yote.
AMKANA
Katika maelezo yake, Diamond
alikataa kata kata kuwa
hamfahamu mtu huyo kisha
akakata simu.
Sina msikiti nitakuwaje na
Ustadhi? Huyo mganga nasema
simfahamu, alisema kisha akakata
simu.
source : GLOBAL PUBLISHERS
WEBSITE
We Diamond, usijifanye chizi! wasanii wooote hutegemea tunguri kuvuta nyota lakini huu ndio mwisho wako!
Kumbe Ustaadh inatumika hata kwenye uganga...
Mi mwenyewe huwa natatizwa ninapokutana na waganga wa kienyeji wanaojitanabaisha kuwa maustaadhi
Kama ni kweli ulimshirikisha huyo jamaa basi Diamond unahitaji kutubu na kumrudia Mungu kwani huo ni ukosefu wa akili na kutojiamini. Pili ninachojiuliza hivi mchango wa huyo bwana kwa muziki wa Diamond ni upi ? Kuandika mashairi ? Kuboresha sauti ? Kutengeneza beat nzuri ? ama ? Huyu bwana anatafuta promo kupitia Diamond kama ni kweli Diamond amewahi kumshirikisha kwenye shughuli zake basi iwe ni fundisho kwa wengine. Na yeyote atakayeenda kwa huyu bwana ajue imekula kwake atakuja kudhalilishwa. Na je katika ufanyaji wake wa hizo kazi amewasaidia wangapi ambao wamefanikiwa kufikia level ya Diamond ? Ni kumaanisha kuwa amebahatisha ? Sitaki kuamoni ujinga wa aina hii. Ila Diamond hili liwe ni fundisho, Muamini Mungu na mambo yako yatakuwa sawa daima hakuna zaidi ya Mungu.(ungelikuwa mkristu ningekuambia yesu ndiye njia ya kweli na uzima)
tofaut ipo kbwa 2 mungu ni 1 na ukmuamini atkusaidia,lkni wganga ni wengi utaamini wangapi?
mkuu usianzishe ligi ya izo vitu na Kiranga...maana haoni vibaya kumtusi Mungu wetu kipenzi,akaturushia stimu waamini.
Mungu ni deal la watu kuwakandamiza wengine, kuwafariji pale faraja inapokosekana (kama kwenye msiba) etc.
Lakini habari za mungu hazina uthibitisho na ukichunguza sana utaona uzushi tu.
All things supernatural are characterized by human ignorance, intentional obfuscation or wishful thinking. Possibly all combined.
Kasema nani? Unajuaje kama mungu ni mmoja? Ushawauliza Wahindu? Kwa nini wewe na imani yako muwe sawa na Wahindu wanaoamini miungu wengi wasiwe sahihi? Kwa sababu wewe umeikuta dini yako kwenu tu?
Na kama wewe unaamini mungu, na Diamond anaamini mganga, wote wawili mnaamini, kimsingi tofauti ni nini kama wote mnaamini?
Kama kuamini kuna tatizo kuna tofauti gani kati ya anayeamini mungu na anayeamini mganga?
Mungu huyo mmoja unayesema unamuamini unamjua historia yake? Kafikaje mpaka ukapata kumuamini wewe? Na kabla yake kiliaminiwa nini na mababu zako?
Anayeamini mganga anaweza kuwa afadhali hata ya anayeamini mungu, maana anayeamini mgamnga anamuona mganga, na dawa isipofanya kazi anaweza kwenda kumdai mganga.
Wewe unayeamini mungu usiyemuona je?
mkuu usitafute ban, jf hairuhusu plagarism..........
sasa wewe mpagani kamawe unaamini ma-theory yaliyobuniwa na wazungu...acha kudhiaki iman za watu,wewe si umetokana na evolution basi endelea kumdhiaki aliyehasisi evolution eti sababu haumuoni kuna siku utaipata flesh.