Mganga wa kienyeji ahukumiwa miaka 20 jela na viboko 12 kwa kosa la kufuga fisi.

Mganga wa kienyeji ahukumiwa miaka 20 jela na viboko 12 kwa kosa la kufuga fisi.

Nani anaikumbuka hii kesi ya yule mganga wa kienyeji aliyekamatwa na fisi? amehukumiwa leo.

View attachment 3267716

Mahakama ya Wilaya Bariadi mkoani Simiyu imemhukumu kifungo cha miaka 20 jela pamoja na kuchapwa viboko 12 Emmanuel John (31), maarufu kama Chief wa Kilulu, kwa kosa la kukutwa na nyara za serikali aina ya fisi akiwa hai na akiishi naye nyumbani kwake.

Mshtakiwa huyo, ambaye ni mkazi wa kijiji cha Kilulu kilichopo kata ya Bunhamala, wilayani Bariadi, na mganga wa kienyeji, alipewa adhabu hiyo katika kesi namba 2458/2025 iliyokuwa ikimkabili kwenye mahakama hiyo.

Awali, akisoma kosa la mshtakiwa, Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mashtaka Mkoa, Lupiana Mahenge, alieleza mahakama kuwa mtuhumiwa huyo alikutwa na nyara ya serikali, fisi akiwa hai, akimfuga nyumbani kwake kinyume cha sheria.

Mtuhumiwa aliishi na fisi huyo kama mnyama wa kufuga kinyume na kifungu cha 86 (1) na kifungu kidogo cha (2)(C)(III) cha Sheria ya Kuhifadhi Wanyamapori sura ya 283, kama ilivyofanyiwa marejeo mwaka 2022.

Mtuhumiwa alipopewa nafasi ya kujitetea aliomba mahakama imsamehe kwa kuwa anategemewa na familia ya watoto wanne, wakiwemo mapacha, ndipo hakimu akatoa adhabu ya kifungo cha miaka 20 jela na viboko 12 ili iwe fundisho kwake na kwa watu wengine.
20 haitoshi angetakiwa afugwe miaka 50 pamoja na kulipa fidia. Ili iwe fundisho hasa huko kanda ya ziwa ndiyo wanapenda sana.
 
Nani anaikumbuka hii kesi ya mganga wa kienyeji aliyekamatwa na fisi? amehukumiwa leo.

View attachment 3267716

Mahakama ya Wilaya Bariadi mkoani Simiyu imemhukumu kifungo cha miaka 20 jela pamoja na kuchapwa viboko 12 Emmanuel John (31), maarufu kama Chief wa Kilulu, kwa kosa la kukutwa na nyara za serikali aina ya fisi akiwa hai na akiishi naye nyumbani kwake.

Mshtakiwa huyo, ambaye ni mkazi wa kijiji cha Kilulu kilichopo kata ya Bunhamala, wilayani Bariadi, na mganga wa kienyeji, alipewa adhabu hiyo katika kesi namba 2458/2025 iliyokuwa ikimkabili kwenye mahakama hiyo.

Awali, akisoma kosa la mshtakiwa, Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mashtaka Mkoa, Lupiana Mahenge, alieleza mahakama kuwa mtuhumiwa huyo alikutwa na nyara ya serikali, fisi akiwa hai, akimfuga nyumbani kwake kinyume cha sheria.

Mtuhumiwa aliishi na fisi huyo kama mnyama wa kufuga kinyume na kifungu cha 86 (1) na kifungu kidogo cha (2)(C)(III) cha Sheria ya Kuhifadhi Wanyamapori sura ya 283, kama ilivyofanyiwa marejeo mwaka 2022.

Mtuhumiwa alipopewa nafasi ya kujitetea aliomba mahakama imsamehe kwa kuwa anategemewa na familia ya watoto wanne, wakiwemo mapacha, ndipo hakimu akatoa adhabu ya kifungo cha miaka 20 jela na viboko 12 ili iwe fundisho kwake na kwa watu wengine.
Watanzania hatupendani tuna chuki binafsi mioyoni mwetu,miaka20 jela na viboko juu kumfuga fisi, ukute alikaokota kakiwa kadogo
 
Mwafrika badala afuge kuku,bata,kanga au mbuzi ambao atauzs apate faida ndani kwake kafungia fisi.Fisi anamsaidia nini haijulikani na faida anayopata kwa kumiliki fisi pia haijulikani
 
Adhabu kubwa kuliko kosa, angemuua angeitwa muwindaji haramu, angalau inge make sense, ila kumfuga tu pasipo kumdhuru sioni kama anastahili adhabu kubwa kiasi hicho, mbona kuna hawa wanaotembea na mijoka mikubwa kwenye maonyesho yao hawakamatwi?
Wataalamu wa Wildlife Act wakuje watupe dondoo tujazie nyama kuhusu hii hukumu
 
Lakini unafuga li fisi la kazi gani wajameni..kwanza ni nyara ya serikali pili likidhuru watu kesi kwako, tatu huna uhuru nalo kutembea nalo mtaani ,nne ni gharama kulihudumia. Ila kudumisha uafrika ni kazi sana
 
Sasa mbona fisi anacheka hivyoo? 😂😂😂😂😂 Au anafurahia kifungo cha boss wake! Wangemfunga nao ili awe anawatunza ha ha ha
 
Nani anaikumbuka hii kesi ya mganga wa kienyeji aliyekamatwa na fisi? amehukumiwa leo.

View attachment 3267716

Mahakama ya Wilaya Bariadi mkoani Simiyu imemhukumu kifungo cha miaka 20 jela pamoja na kuchapwa viboko 12 Emmanuel John (31), maarufu kama Chief wa Kilulu, kwa kosa la kukutwa na nyara za serikali aina ya fisi akiwa hai na akiishi naye nyumbani kwake.

Mshtakiwa huyo, ambaye ni mkazi wa kijiji cha Kilulu kilichopo kata ya Bunhamala, wilayani Bariadi, na mganga wa kienyeji, alipewa adhabu hiyo katika kesi namba 2458/2025 iliyokuwa ikimkabili kwenye mahakama hiyo.

Awali, akisoma kosa la mshtakiwa, Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mashtaka Mkoa, Lupiana Mahenge, alieleza mahakama kuwa mtuhumiwa huyo alikutwa na nyara ya serikali, fisi akiwa hai, akimfuga nyumbani kwake kinyume cha sheria.

Mtuhumiwa aliishi na fisi huyo kama mnyama wa kufuga kinyume na kifungu cha 86 (1) na kifungu kidogo cha (2)(C)(III) cha Sheria ya Kuhifadhi Wanyamapori sura ya 283, kama ilivyofanyiwa marejeo mwaka 2022.

Mtuhumiwa alipopewa nafasi ya kujitetea aliomba mahakama imsamehe kwa kuwa anategemewa na familia ya watoto wanne, wakiwemo mapacha, ndipo hakimu akatoa adhabu ya kifungo cha miaka 20 jela na viboko 12 ili iwe fundisho kwake na kwa watu wengine.
Y viboko tena kwa baba wa watu 😅😅😅😅😅😅
 
Ni tapeli, sio mganga, angekuwa mganga wa kweli fisi hangeonekana. Wengi wanafuga ila hayaonekani kwa macho.
 
Waganga wanaowachinjia watoto au kutaka viungo vya albino kwa nafasi zao awakamatwi.
 
Back
Top Bottom