Mgao wa umeme uliotangazwa na TANESCO kwa ajili ya ukame. Je, tutegemee mgao zaidi hata litakapokamilika bwawa la Nyerere?

Mgao wa umeme uliotangazwa na TANESCO kwa ajili ya ukame. Je, tutegemee mgao zaidi hata litakapokamilika bwawa la Nyerere?

Mystery

JF-Expert Member
Joined
Mar 8, 2012
Posts
15,843
Reaction score
31,057
Nimeona vigogo wa TANESCO wakitutahadharisha watanzania kuwa kutokana na ukame uliolikumba Taifa letu, kutokana na mabadiliko ya tabia nchi, wamelazimika wao TANESCO kuanzisha mgao wa umeme nchi nzima, kutokana na mabwawa ya Kihansi, Mtera na Kidatu, kupungukiwa maji ya kuyajaza mabwawa hayo kutokana na ukame na hivyo kulazimika kuizima mitambo hiyo uliosababishwa na tabia nchi.

Ndipo hapo ninapojiuliza, hivi pamoja na kutumia matrillioni kadhaa ya pesa, kwa ajili ya kujenga bwawa la Nyerere, ambalo watawala wetu wamekuwa wakilipigia "promo" kubwa Sana, kuwa ndilo litakalokuwa "muarobaini" wa tatizo letu la umeme nchini, kwani litakuwa linazalisha umeme usiopungua Megawatts 2,000 hivi kwa mwenendo tunaokwenda nao wa ukame unaosababishwa na kile kinachoitwa mabadiliko ya tabia nchi, ambapo inategemea kudra ya Mwenyezi Mungu kuendelea kuileta mvua itayojaza mabwawa hayo, je mgao huu wa umeme utaendelea kuwepo nchini, hata pale tutakapoufungua mradi huo mkubwa wa umeme wa bwawa la Nyerere?

Swali lingine ambalo ningependa kuwauliza hao TANESCO, hivi hii miradi ya uzalishaji umeme kwa kutumia gesi asilia yetu tuliyoivumbua huko Mtwara, ambayo nayo imeligharimu Taifa letu matrillioni ya pesa, ina maana nayo ni white elephant projects?

Kama kawaida ya watawala wetu, kutuona watanzania wote ni wajinga wa kupitiliza, tunaoweza kudanganywa wakati wote!

Naomba hayo maswali machache nijibiwe na hao wataalamu wetu wa TANESCO
 
Kiongozi hiyo miradi mikubwa, ndiyo upigaji ulimojificha. Kinachoshangaza sana vianzo muhim vikubwa ambavyo ni gesi na makaa ya mawe huji sikia Hata mule bungeni, wabunguaji wakivitetea kwa hali na mali. Hivi ujue mradi wa magenerator ndiyo watapiga pesa mpaka tulie moooo!!
 
Kiongozi hyo miradi mikubwa,ndyo upigaji ulimojificha.Kinachoshangaza sana vianzo muhim vikubwa ambavyo ni gesi na makaa ya mawe huji sikia Hata mule bungeni, wabunguaji wakivitetea kwa hali na mali . Hivi ujue mradi wa magenerator ndy watapiga pesa mpaka tulie moooo!!
Nchi hii imejaa washibishaji matumbo yao..............

Kwao wao, mradi wa kuuza majenereta ndiyo "deal" ya kujitajirisha.

Nchi hii ni viongozi wachache Sana, wanaojali maslahi mapana kwa Taifa
 
Nimeona vigogo wa TANESCO wakitutahadharisha watanzania kuwa kutokana na ukame uliolikumba Taifa letu, kutokana na mabadiliko ya tabia nchi...
Simple! Bwawa la Nyerere maji yatatoka wapi kama haya ya sasa yanakosa maji wakati wa ukame? Jibu unalo!
 
Hata huko China kwenye Yangtze three gorges dam ukame umekausha nao wameanza mgao.
 
Kwani waziri mwenye dhamana na nishati hapa nchini anasemaje!?
Kama hakuna mvua waziri aseme nini? Walipoanza mradi wa bwawa la Nyerere viongozi walijua kabisa kuwa mabadiliko ya tabia nchi yapo, na mvua hazitabiliki- wao hawakuamini wataalamu ila wakatumia utashi wao.
 
Hakuna Cha ukame hii ni Ile staili ya kugungulia mabwawa ili watu wapige ela hapa naona harufu ya iptl kurudi nakumbuka magu alisema kulikua na wajanja wachache wanaotengeneza ukame Kwa faida yao hatujasahau hayo bado
 
Wakulima wa Mchele kilombero , kilosa, na mbarali ndo wanasababisha bwawa liishe maji. Wasipodhibitiwa hata mradi wa stiglers ukikamilika maji hayatatisha, nashauri wafukuzwe
 
Nimeona vigogo wa TANESCO wakitutahadharisha watanzania kuwa kutokana na ukame uliolikumba Taifa letu, kutokana na mabadiliko ya tabia nchi...
Mtamkumbuka Prof Muhongo kwa kumchafua kuwa ni mwongo.moja kati ya michango yake ktk bunge aliwahi kusema kuwa umeme wa maji si wa kuaminika na tufute vyanzo vya kuaminika.wabunge wenzake wakambeza leo hii tuko wapi?

Tusipowatumia watalaamu wetu vzr hali itakuwa mbaya zaidi huko mbeleni.hata mwaka huu dalili zinaonyesha hakutakuwa na mvua za kutosha hivyo tutegemee mgao huu utakuwa endelevu na unakwenda kuathiri moja kwa moja uzalishaji wa bidhaa na huduma hivyo kupandisha bei ya bidhaa na huduma hizo.
 
Wakulima wa Mchele kilombero , kilosa, na mbarali ndo wanasababisha bwawa liishe maji. Wasipodhibitiwa hata mradi wa stiglers ukikamilika maji hayatatisha, nashauri wafukuzwe
Unasema wakulima wafukuzwe, mchele ukipanda bei sana utakuja hapa kusema bwawa lifungwe maji tumwagilie mpunga.

Kifupi watanzania hatujui tunataka nini,
Ndio maana watawala wetu wanatudharau.
 
Back
Top Bottom