Bemendazole
JF-Expert Member
- Nov 14, 2020
- 2,649
- 6,680
Yamepungua kuanzia eneo gani? mwanzoni mwa oktoba nimepita barabara ya Iringa -Mikumi kupita milima ya udzungwa maji yanatiririka kwa kasi utafikiri ni wakati wa masika. Labda kama waliyafungulia kwa makusudi huko mtera.Mto Ruaha maji yamepungua sana
Nilikuwa Ruaha National park Mto una maji machache sanaYamepungua kuanzia eneo gani? mwanzoni mwa oktoba nimepita barabara ya Iringa -Mikumi kupita milima ya udzungwa maji yanatiririka kwa kasi utafikiri ni wakati wa masika. Labda kama waliyafungulia kwa makusudi huko mtera.
Mto unajaza bwawa lipi? Maana kule udzungwa ni maji yaliyotoka mtera kuelekea KidatuNilikuwa Ruaha National park Mto una maji machache sana
Acha kujitoa ufahamu, kwani mvua hunyesha kwa kificho kusema watu watajua kuwa mvua zipo za kutosha ama la? UnashangazaHakuna Cha ukame hii ni Ile staili ya kugungulia mabwawa ili watu wapige ela hapa naona harufu ya iptl kurudi nakumbuka magu alisema kulikua na wajanja wachache wanaotengeneza ukame Kwa faida yao hatujasahau hayo bado
Kwa miaka 60 unatumia hydropower plant...kusingekuwa na uchepushwaji na hujuma maji yanatosha sana. Nyerere dam bado ni mradi sahihi na litakuwa na reserve kubwa sana kukabiliana na ukama kuanzia kuutunza umeme mpaka maji.Kama hakuna mvua waziri aseme nini? Walipoanza mradi wa bwawa la Nyerere viongozi walijua kabisa kuwa mabadiliko ya tabia nchi yapo, na mvua hazitabiliki- wao hawakuamini wataalamu ila wakatumia utashi wao.
Kama kutakuwa na Ukame mgao utakuwepoNimeona vigogo wa TANESCO wakitutahadharisha watanzania kuwa kutokana na ukame uliolikumba Taifa letu, kutokana na mabadiliko ya tabia nchi, wamelazimika wao TANESCO kuanzisha mgao wa umeme nchi nzima, kutokana na mabwawa ya Kihansi, Mtera na Kidatu, kupungukiwa maji ya kuyajaza mabwawa hayo kutokana na ukame na hivyo kulazimika kuizima mitambo hiyo uliosababishwa na tabia nchi.
Ndipo hapo ninapojiuliza, hivi pamoja na kutumia matrillioni kadhaa ya pesa, kwa ajili ya kujenga bwawa la Nyerere, ambalo watawala wetu wamekuwa wakilipigia "promo" kubwa Sana, kuwa ndilo litakalokuwa "muarobaini" wa tatizo letu la umeme nchini, kwani litakuwa linazalisha umeme usiopungua Megawatts 2,000 hivi kwa mwenendo tunaokwenda nao wa ukame unaosababishwa na kile kinachoitwa mabadiliko ya tabia nchi, ambapo inategemea kudra ya Mwenyezi Mungu kuendelea kuileta mvua itayojaza mabwawa hayo, je mgao huu wa umeme utaendelea kuwepo nchini, hata pale tutakapoufungua mradi huo mkubwa wa umeme wa bwawa la Nyerere?
Swali lingine ambalo ningependa kuwauliza hao TANESCO, hivi hii miradi ya uzalishaji umeme kwa kutumia gesi asilia yetu tuliyoivumbua huko Mtwara, ambayo nayo imeligharimu Taifa letu matrillioni ya pesa, ina maana nayo ni white elephant projects?
Kama kawaida ya watawala wetu, kutuona watanzania wote ni wajinga wa kupitiliza, tunaoweza kudanganywa wakati wote!
Naomba hayo maswali machache nijibiwe na hao wataalamu wetu wa TANESCO
Ni vyema tukaelezwa ukweli.Hiv hawa Wafanyakazi wa Tanesco hakuna mzalendo hata mmoja akatoa siri nn kinafanyika huko? Kweli maji yamekauka au watu wanafungua mabwawa ili upigaji uendelee?