Mgeni Siku ya Kwanza (Ni wapi Chimbuko la hili Shairi la Kale)

Mgeni Siku ya Kwanza (Ni wapi Chimbuko la hili Shairi la Kale)

Logikos

JF-Expert Member
Joined
Feb 26, 2014
Posts
15,460
Reaction score
24,233
Mgeni siku ya kwanza
mpe mchele na panza;
mtilie kifuani,
mkaribishe mgeni.

Mgeni siku ya pili
mpe ziwa na samli;
mahaba yakizidia,
mzidishie mgeni.

Mgeni siku ya tatu
jumbani hamuna kitu.
mna zibaba zitatu,
pika ule na mgeni.

Mgeni siku ya nne
mpe jembe akalime.
akirudi muagane,
aende kwao mgeni,

Mgeni siku ya tano
mwembamba kama sindano,
hayeshi masengenyano,
asengenywayo mgeni.

Mgeni siku ya sita;
mkila mnajificha;
mwaingia vipembeni
afichwaye ni mgeni.

Mgeni siku ya saba,
si mgeni ana baa.
hata moto mapaani
katia yeye mgeni,

Mgeni siku ya nane;
njoo ndani tuonane.
atapotokea nje,
natuagane mgeni,

Mgeni siku ya kenda;
enenda mwana kwenenda!
usirudi nyuma nenda,
utokomee mgeni.

Mgeni siku ya kumi
kwa mateke na magumi.
hapana afukuzwaye,
Ila ni yeye mgeni.​
 
Hakuna ajuaye ?
Au hamjawahi kuwa wageni wasioondoka mpaka kwa mateke na magumi ?
 
Mgeni siku ya kwanza
mpe mchele na panza;
mtilie kifuani,
mkaribishe mgeni.

Mgeni siku ya pili
mpe ziwa na samli;
mahaba yakizidia,
mzidishie mgeni.

Mgeni siku ya tatu
jumbani hamuna kitu.
mna zibaba zitatu,
pika ule na mgeni.

Mgeni siku ya nne
mpe jembe akalime.
akirudi muagane,
aende kwao mgeni,

Mgeni siku ya tano
mwembamba kama sindano,
hayeshi masengenyano,
asengenywayo mgeni.

Mgeni siku ya sita;
mkila mnajificha;
mwaingia vipembeni
afichwaye ni mgeni.

Mgeni siku ya saba,
si mgeni ana baa.
hata moto mapaani
katia yeye mgeni,

Mgeni siku ya nane;
njoo ndani tuonane.
atapotokea nje,
natuagane mgeni,

Mgeni siku ya kenda;
enenda mwana kwenenda!
usirudi nyuma nenda,
utokomee mgeni.

Mgeni siku ya kumi
kwa mateke na magumi.
hapana afukuzwaye,
Ila ni yeye mgeni.​
Hatari Sana!
 
Hatari Sana!
Najaribu kujua Chimbuko lake, Sikumbuki kama upo kwenye kitabu cha Bulicheka..., ila huu hata Kenya wanao pia..., na Kwa ukarimu wa Watanzania Kipindi kile nadhani / sichelei kusema huenda ulitoka huko..., ila sijui Ngoja Nimuulize huyu Muhenga wa Kale huenda anajua...

Mohamed Said
 
Pia naona Ukarimu huu sio Huku tu..., Hata wenzetu huko India wana Msemo

The first day a guest, the second day a guest, the third day a calamity.


Au toka kitambo kulikuwa na misemo kama hii

The first day one is a guest, the second a burden, and the third a pest. Aidha kuna Ushauri unatolewa Don't Overstay your Welcome..., Kwahio sichelei kusema huenda world over Binadamu ni Wachoyo....
 
Ugeni ugeni ugeni, hadi nakoswa usemi
wasikuzoe machoni, maneno ninenayo mimi
watakusema chumbani, jikoni had sebreni
Watakutia majaribuni, kwa mishale itokayo vinywani
UGENINI SIO NYUMBANI, WASIKUZOE MACHONI.

Nilikuwa najaribu tu kujidai Shabani Robert
 
Mgeni siku ya kwanza
mpe mchele na panza;
mtilie kifuani,
mkaribishe mgeni.

Mgeni siku ya pili
mpe ziwa na samli;
mahaba yakizidia,
mzidishie mgeni.

Mgeni siku ya tatu
jumbani hamuna kitu.
mna zibaba zitatu,
pika ule na mgeni.

Mgeni siku ya nne
mpe jembe akalime.
akirudi muagane,
aende kwao mgeni,

Mgeni siku ya tano
mwembamba kama sindano,
hayeshi masengenyano,
asengenywayo mgeni.

Mgeni siku ya sita;
mkila mnajificha;
mwaingia vipembeni
afichwaye ni mgeni.

Mgeni siku ya saba,
si mgeni ana baa.
hata moto mapaani
katia yeye mgeni,

Mgeni siku ya nane;
njoo ndani tuonane.
atapotokea nje,
natuagane mgeni,

Mgeni siku ya kenda;
enenda mwana kwenenda!
usirudi nyuma nenda,
utokomee mgeni.

Mgeni siku ya kumi
kwa mateke na magumi.
hapana afukuzwaye,
Ila ni yeye mgeni.​
Nakumbuka na vipicha vya watu vinavyoendana na kila fungu la shairi, Ila sikumbuki ni kitabu gani.
 
Ugeni ugeni ugeni, hadi nakoswa usemi
wasikuzoe machoni, maneno ninenayo mimi
watakusema chumbani, jikoni had sebreni
Watakutia majaribuni, kwa mishale itokayo vinywani
UGENINI SIO NYUMBANI, WASIKUZOE MACHONI.

Nilikuwa najaribu tu kujidai Shabani Robert

Shaaban Robert anajua mwanangu.
Nachosikitika kazi zake nyingi hazikuchapishwa, angechapisha jamaa angekiwa ana vitabu vingi kama James Hardley Chase
 
Hizo kazi zipo wapi ni rahisi sana kama bado zipo ndugu zake wakazichukua na kuzichapisha (hapo watapata pesa kwa kutumia fame yake)

Tangu 1960 hadi leo?
Zitakuwa zimechoka sana pengine ndugu wamezichoma moto au kuzitupa.
Jaribu kutembelea nyumbani kwake ukaonane na wake zake
 
Shaaban Robert anajua mwanangu.
Nachosikitika kazi zake nyingi hazikuchapishwa, angechapisha jamaa angekiwa ana vitabu vingi kama James Hardley Chase
Wewe ushaona ngapi ambazo hazikuchapishwa ?

Unajua mara nyingi Legend inakuwa kubwa kuliko hata uhalisia...
 
Back
Top Bottom