Mgogoro wa Palestina na Israel: Chimbuko na Suluhu

Mgogoro wa Palestina na Israel: Chimbuko na Suluhu

Grand Canyon

JF-Expert Member
Joined
Jan 2, 2020
Posts
545
Reaction score
1,191
Jina Palestina linatokana na neno la Kilatini Palaestina na neno la Kigiriki Palaeistine. Maneno haya mawili yanatokana na neno la Kiebrania Pelesheth. Biblia inatumia neno Pelesheth linatafsiriwa Filistia kwa Kiswahili kwenye Biblia.

Linarejelea eneo la Pwani ya Mediterenia lililokaliwa na Wafilisti.

Katika Biblia majina Palestina, Kanaani, Israeli, Nchi ya Ahadi yana maana moja. Wayahudi walipotoka Misri Mungu aliwaahidi kuwapa Kanaani waimiliki. Wakati huo ilikuwa ikikaliwa na Wafilisti. Abrahamu, Isaka na Yakobo waliishi Kanaani/Palestina kabla ya Yakobo kuhamia Misri.

Waliporudi waliwatimua Wafilisti nao wakaimiliki nchi ya Kanaani/Palestina. Mwaka 1070 BC Daudi akafanya Yerusalemu kuwa mji wake mkuu. Sulemani akamjengea Mungu hekalu Yerusalemu.

Mwaka wa 70 AD Roman Empire iliteketeza Yerusalemu na hekalu lake na kuwapeleka Wayahudi uhamishoni katika maeneo mbali mbali ya milki hiyo.

AD 130 Emperor Adrian alilijenga upya Yerusalemu na kuliita Aelia Capitolina. Akawapiga marufuku Wayahudi kukanyaga katika jiji hilo kwa miaka 200. Kisha Mama ya Emperor Constantine aliyeitwa Hellen alitembelea Yerusalemu na akaanza kujenga maeneo matakatifu (Shrines) na Makanisa.

Katika karne ya 7 AD waislamu waliteka jiji la Yerusalemu na Caliph Abd al-Malik ibn Marwan akajenga Msikiti wa el Aqsa. Waarabu walihamia Palestina kipindi hiki hasa kuanzia mwaka wa 638 AD.

Baada ya Adolf Hitler kuwaua Wayahudi karibu milioni 6, Uingereza iliamua kuwarudisha kwao yaani Israeli/Kanaani/Palestina. Hivyo mgogoro ukazuka.

NB😛alestina ni Geographic location. Kuna wapalestina waarabu, Wapalestina Wayahudi, nk. Hata mimi nikipata uraia nitaitwa Mpalestina mwenye asili ya Tanzania.

MFANO: Tuseme ni mwaka 1967. Serikali inaanzisha vijiji vya Ujamaa. Watu wa Kijiji A wanapelekwa Kijiji B ambacho kina huduma zote za kijamii. Baada ya wanakijiji kuondoka watu wengine wanahamia Kijiji A. Wanajenga na kulima mashamba. Kisha mwaka 1985 sera ya ujamaa inakufa. Watu waliohamishwa wanarudi Kijiji A wanakuta tayari watu wengine wameshajenga na kuishi hapo. Mzozo unazuka. Nani atatatua mzozo huu?

Hiyo ndiyo hali ya Palestina. Wayahudi waliondoshwa mwaka 70 AD, Waarabu wakahamia 638 AD. Wayahudi wakarudi nyumbani 1947 AD. Waarabu wanawaona Wayahudi kuwa wavamizi, na Wayahudi wanawaona Waarabu kuwa wavamizi.
 
Wafilisti ni kina nani kwa sasa hivi?
Wanaongea lugha gani?
Kulingana na mwanahistoria Josephus, Alexander the Great atashambulia Gaza akawaua wafilisti kisha waliobaki aliwauza utumwani sehemu mbali mbali za miliki ya Ugiriki. Hivyo utambulisho wao haupo tena.
 
Asante kwa ilimu, nadhani middle east iko hivyo ili kufanya dunia ”isipoe”
 
Huu ugomvi hayupo mtu / nchi ya kuamua kwasababu wanajua historia. Baada ya kujiita Warabu wanajiita Wapelestina.
Katika karne ya 7 AD waislamu waliteka jiji la Yerusalemu na Caliph Abd al-Malik ibn Marwan akajenga Msikiti wa el Aqsa. Waarabu walihamia Palestina kipindi hiki hasa kuanzia mwaka wa 638 AD.
 
Kulingana na mwanahistoria Josephus, Alexander the Great atashambulia Gaza akawaua wafilisti kisha waliobaki aliwauza utumwani sehemu mbali mbali za miliki ya Ugiriki. Hivyo utambulisho wao haupo tena.
Hehe ....
Haya mkuu.
 
Hehe ....
Haya mkuu.

Kulingana na mwanahistoria Josephus, Alexander the Great "alishambulia" Gaza akawaua wafilisti kisha waliobaki aliwauza utumwani sehemu mbali mbali za miliki ya Ugiriki. Hivyo utambulisho wao haupo tena.
 
Kulingana na mwanahistoria Josephus, Alexander the Great "alishambulia" Gaza akawaua wafilisti kisha waliobaki aliwauza utumwani sehemu mbali mbali za miliki ya Ugiriki. Hivyo utambulisho wao haupo tena.
Sawa.
 
Swali langu ni hili!?? Je kabla ya kwenda utumwani Misri wayahudi kwao kulikua ni wapi!?? Nitajie jina!!
Pili, hivi hizo nchi hawawezi kugawana kila mtu aende kwake!?? Nisaidie ndugu
 
Swali langu ni hili!?? Je kabla ya kwenda utumwani Misri wayahudi kwao kulikua ni wapi!?? Nitajie jina!!
Pili, hivi hizo nchi hawawezi kugawana kila mtu aende kwake!?? Nisaidie ndugu
Kuna ushahidi wowote kuwa wayahudi walikwenda utumwani Misri?
Lini?
 
Swali langu ni hili!?? Je kabla ya kwenda utumwani Misri wayahudi kwao kulikua ni wapi!?? Nitajie jina!!
Pili, hivi hizo nchi hawawezi kugawana kila mtu aende kwake!?? Nisaidie ndugu
Tatizo wanataka kusolve tatizo kwa kutumia dini... Na vitabu vyake.
Kiasili wale wote pale sio Kwao ndo maana vurugu ni nyingi. Kama ukisoma vzr historia utajua ya kuwa mwanzoni hao USA na UK walitaka kuwa peleka hao Jews converts to UGANDA.... Kwamba ndio iwe nchi yao..... So unaona kabisa hawa jamaa hawajulikani ni wa wapi. Why Uganda??? If kama pale Israel ni kwao hili wazo la kuwa peleka Uganda lisingekuwepo in the first place.
Kama. Mleta uzi alivyosema kweli waarabu walihamia na akina macalif wao.
Na hao Jews pia wamehamia tu hapo wakiletwa na westerners... Walitumia story ya bibble kuwalazimishia kukaa hapo. Ndo maana wanawalinda kwa kila hali na Mali. Sababu wamewakweka hapo kimkakati
 
Swali langu ni hili!?? Je kabla ya kwenda utumwani Misri wayahudi kwao kulikua ni wapi!?? Nitajie jina!!
Pili, hivi hizo nchi hawawezi kugawana kila mtu aende kwake!?? Nisaidie ndugu
Kwa sababu ya njaa Yakobo aliondoka Palestina/Kanaani na kuelekea Misri na familia yake ambako yeye na wazao wake waliishi kwa miaka 215. Wakiacha ukabila, udini wanaweza kuishi kama sisi watu wa makabila mengi na dini nyingi tunavyoishi.
 
Jina Palestina linatokana na neno la Kilatini Palaestina na neno la Kigiriki Palaeistine. Maneno haya mawili yanatokana na neno la Kiebrania Pelesheth. Biblia inatumia neno Pelesheth linatafsiriwa Filistia kwa Kiswahili kwenye Biblia.

Linarejelea eneo la Pwani ya Mediterenia lililokaliwa na Wafilisti.

Katika Biblia majina Palestina, Kanaani, Israeli, Nchi ya Ahadi yana maana moja. Wayahudi walipotoka Misri Mungu aliwaahidi kuwapa Kanaani waimiliki. Wakati huo ilikuwa ikikaliwa na Wafilisti. Abrahamu, Isaka na Yakobo waliishi Kanaani/Palestina kabla ya Yakobo kuhamia Misri.

Waliporudi waliwatimua Wafilisti nao wakaimiliki nchi ya Kanaani/Palestina. Mwaka 1070 BC Daudi akafanya Yerusalemu kuwa mji wake mkuu. Sulemani akamjengea Mungu hekalu Yerusalemu.

Mwaka wa 70 AD Roman Empire iliteketeza Yerusalemu na hekalu lake na kuwapeleka Wayahudi uhamishoni katika maeneo mbali mbali ya milki hiyo.

AD 130 Emperor Adrian alilijenga upya Yerusalemu na kuliita Aelia Capitolina. Akawapiga marufuku Wayahudi kukanyaga katika jiji hilo kwa miaka 200. Kisha Mama ya Emperor Constantine aliyeitwa Hellen alitembelea Yerusalemu na akaanza kujenga maeneo matakatifu (Shrines) na Makanisa.

Katika karne ya 7 AD waislamu waliteka jiji la Yerusalemu na Caliph Abd al-Malik ibn Marwan akajenga Msikiti wa el Aqsa. Waarabu walihamia Palestina kipindi hiki hasa kuanzia mwaka wa 638 AD.

Baada ya Adolf Hitler kuwaua Wayahudi karibu milioni 6, Uingereza iliamua kuwarudisha kwao yaani Israeli/Kanaani/Palestina. Hivyo mgogoro ukazuka.

NB😛alestina ni Geographic location. Kuna wapalestina waarabu, Wapalestina Wayahudi, nk. Hata mimi nikipata uraia nitaitwa Mpalestina mwenye asili ya Tanzania.

MFANO: Tuseme ni mwaka 1967. Serikali inaanzisha vijiji vya Ujamaa. Watu wa Kijiji A wanapelekwa Kijiji B ambacho kina huduma zote za kijamii. Baada ya wanakijiji kuondoka watu wengine wanahamia Kijiji A. Wanajenga na kulima mashamba. Kisha mwaka 1985 sera ya ujamaa inakufa. Watu waliohamishwa wanarudi Kijiji A wanakuta tayari watu wengine wameshajenga na kuishi hapo. Mzozo unazuka. Nani atatatua mzozo huu?

Hiyo ndiyo hali ya Palestina. Wayahudi waliondoshwa mwaka 70 AD, Waarabu wakahamia 638 AD. Wayahudi wakarudi nyumbani 1947 AD. Waarabu wanawaona Wayahudi kuwa wavamizi, na Wayahudi wanawaona Waarabu kuwa wavamizi.
Ibrahimu ndo aliahidiwa inchi kipindi anaishi Urdu ya kaldayo, na nchi hiyo tayari walikua wanaishi watu mfano yerusalemu walikuwa wanaishi wayebusi na ulikua unaitwa yebusi, na wenyeji wengine ni wakaanani
 
Tunafanya kosa kubwa kiutazama mgogoro huu kuwa chanzo chake ni Kidini. Hii ni suala la siasa za kimaeneo. Dini imetumika tu kama kigezo. Pitia hapa:

 
Back
Top Bottom