Mgogoro wa Russia Vs Ukraine: Tuache Ushabiki; Athari ya Vita mara nyingi huwa ni ya dunia nzima Tuombe mgogoro huu utafutiwe ufumbuzi wa haraka

Mgogoro wa Russia Vs Ukraine: Tuache Ushabiki; Athari ya Vita mara nyingi huwa ni ya dunia nzima Tuombe mgogoro huu utafutiwe ufumbuzi wa haraka

Peter Madukwa

JF-Expert Member
Joined
Sep 20, 2012
Posts
3,139
Reaction score
2,488
Habari ndugu wana JF

Kama inavyoonekana katika vyombo vya habari kwa muda mrefu sasa kumekuwa na mgogoro kati ya Urusi na Ukraine.

Mgogoro huu chanzo chake kikubwa ni dhamira ya UKRAINE Kujiunga na Mkataba wa NATO ambao pia unahusisha MAREKANI.

Kwa mujibu wa madai ya Urusi wanasema kuwa hawapendezwi kuona Ukraine inajiunga na NATO kwa sababu wana hofu ya usalama wa mipaka yake ambapo endapo UKRAINE ikijiunga na NATO basi Urusi wanaamini kuwa MAREKANI itaweka millitary base UKRAINE ambayo ipo mpakani na URUSI na hivyo kwa maelezo ya Rais Viladmir Putin wa Urusi ni kuwa kiusalama itakuwa hatari zaidi ktk nchi yake jasa ukizingatia nchi hizi ni mahasimu ktk masuala ya kijeshi na uchumi kwa kuwa zote zina nguvu kubwa ya kiuchumi (RUSSIA VS USA).

Kwa sasa hivi imekuwa siyo mgogoro tena ambapo imeripotiwa mapema leo asubuhi majeshi ya URUSI yamezingira karibu eneo lote la mipaka ya UKRAINE kupitia nchi jirani ikiwemo Belarus.

Kwa mujibu wa vyanzo mbalimbali vya habari tayari Urusi imeaanza mashambulizi dhdi ya Ukraine na hivyo kusababisha madhara ya vifo vya watu 6 huku wananchi wengi wa UKRAINE wakionekana kukimbia nchi kuelekea nchi za jirani.

Mapema leo Rais wa Urusi amewataka wanajeshi wa Ukraine kusalimu amri na kuweka silaha chini kabla hawajasambaratishwa huku akitamba kuwa nchi yoyote itakayojaribu kuingilia mgogoro huo atakiona cha mtema kuni.

Hapa nchini kwetu ukiingia ktk mitandao watu wengi wanaaonekana kuleta ushabiki wa kivita.. wapo ambao wapo upande wa Urusi na wapo ambao wapo upande wa Ukraine wakiamini kuwa NATO hasa marekani inaweza kuingilia vita hiyo ili wazichape na Urusi.

Kimsingi ndugu zangu watanzania VITA siyo jambo la kushabikia; ktk ulimwengu wa sasa ambao uchumi ni wa kutegemeana ukiacha athari ya moja kwa moja kama vile mauaji ya raia wasio na hatia, uharibifu wa miundombinu ktk eneo la vita lakini VITA huleta athari ya uchumi wa dunia ikiwemo mfumuko wa bei ya bidhaa muhimu kama mafuta ya petrol na diesel ambayo kupanda kwake huleta athari kubwa ktk uchumi wa dunia hasa ktk NCHI MASKINI/ZINAZOENDELEA ambapo uchumi wetu ni wa kusuasua.

Shime ndugu zangu vita siyo jambo la kushabikia badala yake tunatakiwa kuomba mgogoro huu uishe salama na kwa muda mfupi tuombe mashirika ya kimataifa ikiwemo UN watafute suluhu ya haraka ya vita hii kati ya UKRAINE na URUSI ili kunusuru athari zinazoweza kujitokeza.

Mapema leo Papa wa Kanisa Katoliki amesema kuwa siku ya Jumatano ya majivu ni siku maalum ya maombi kwa ajili ya kumwomba Mungu kumaliza mgogoro wa Ukraine na Urusi ili dunia iendelee kubaki kuwa sehemu salama ya kuishi

Mungi ibariki Tanzania, Mungu Ubariki ulimwengu kuwa sehemu ya amani badala ya vita.

Pichani: RAIA WA UKRAINE WAKIKIMBIA NCHI YAO BAADA YA URUSI KUANZA MASHAMBULIZI YA MABOVU.

FB_IMG_1645707661926.jpg


20220224_170300.jpg


20220224_170311.jpg


20220224_170333.jpg


20220224_170338.jpg


20220224_170346.jpg


20220224_170400.jpg




20220224_170419.jpg

20220224_205320.jpg

Wanaoumia ni raia wasio na hatia

20220225_121940.jpg


20220225_112027.jpg


Updates: 1.3.2022

Bei ya mafuta imepanda ktk soko la dunia

Updates: Tarehe 5.4.2022

Bei ya mafuta ya petroli yazidi kupaa kufuatia kuadimika kwa bidhaa hiyo inayochangiwa na athari ya vita ya Ukraine na Russia ambao unakwenda sambamba na vita ya kiuchumi
 
Kanisa Katoliki lina desturi na historia ya kufumbia macho migogoro na viongozi dhalimu, na kuibuka baada ya madhara ya migogoro na udhalimu huo kuanza kuathiri jamii.

Huwa ninaichukia sana hii tabia
 
Anachokifanya sasa Rusia kuivamia Ukraine,huko nyuma U.S na NATO walishafanya kwa nchi kadhaa kama Iraq,Syria,Afghan na Libya.
Wrong is Wrong hata kama itafanywa na kila mtu. Ukweli utabaki palepale kuwa vita siyo jambo la kishabiki na haipaswi kuvumiliwa. Hatua lazima zuchukuliwe ili dunia ibaki kuwa sehemu salama
 
Anachokifanya sasa Rusia kuivamia Ukraine,huko nyuma U.S na NATO walishafanya kwa nchi kadhaa kama Iraq,Syria,Afghan na Libya.
kunusuru UCHUMI wa dunia na kuiacha DUNIA kuwa na AFYA njema inapaswa NATO na US iachane na VITA hii isiyo na FAIDA yoyote Zaidi ya hasara kubwa wasioitegemea
Hakuna anaekubaliana na UVAMIZI wa URUSI Ukraine ila anachofanya URUSI ni kujilinda kwa namna yoyote ambapo hata yeye US asingekubali MEXICO iingie uhusiano wa kijeshi na URUSI kisha urusi ikadai kuilinda MEXICO kijeshi
wote tuliona URUSI kwa mwaka mmoja nyuma hakuwa na NIA ya kuivamia UKRAINE na hata kwa miaka ya nyuma kabla uvamizi CRIMEA walikuwa na uhusiano mzuri tu
ila CHOKOCHOKO za US ndio zilizopelekea URUSI kufikia hatua hiyo iliyopo sasa

Inachopaswa US na washirika wake waache ubwanyenye 7bu URUSI sio lelemama ipo Vizuri hata kma wataamini wakiingiza majeshi yao watashinda VITA
Ni sawa ila ATHARI zitakazojitokeza HAZITATIBIKA mpk DUNIA itakapofikia ukingoni 7bu siraha walizonazo wote NATO na URUSI ni za hatari mno
 
Tanzania kila kitu ni Yanga vs Simba, hiyo duality inatawala maisha yetu, usipokuwa CCM basi unalazimishwa kuwa chadema, usipopendezwa na Samia wewe ni unalazimishwa
team Magu ( RIP), Tanzania hakuna grey area, kila kitu ni black or white.

Hii jamii inaumwa!
 
Ingawaje Ukraine wana haki ya kuheshimiwa sovereignty yake na hivyo kuwa na haki na uhuru wa kujiunga na jumuiya yoyote ile lakini bado, kwa kuzingatia jicho la NATO dhidi ya Russia, napata taabu kuilamu Russia!

Hata nami ningekuwa ndo Putin... I'd do whatever it takes to make sure NATO isn't anywhere near my door!

Kama ambavyo Ukraine walivyo na haki ya kujiunga na NATO na ndivyo Russia walivyo na haki ya kuchukua tahadhali mapema dhidi ya chochote kile kinachoweza kuikaribisha NATO barazani pa Russia!
 
They are clearly already prepared for any sanction they could face, they wouldn't have invaded if sanctions would bring them down
 
Russian FM Lavrov says Moscow wants:

  • Our expectations of Kyiv remain the same, Russia doesn’t change its position “like a girl”
  • We want to 'free Ukraine from oppression'
  • President Putin will hold several int phone calls
  • We want to ensure demilitarisation of Ukraine https://t.co/AT8CWuePp8
 
Back
Top Bottom