Mgogoro wa wananchi na wafugaji wa Kimasai utafutiwe suluhu

Mgogoro wa wananchi na wafugaji wa Kimasai utafutiwe suluhu

Hismastersvoice

JF-Expert Member
Joined
Jan 26, 2013
Posts
21,741
Reaction score
26,735
Huko Morogoro umetokea mgogoro kati ya wananchi na wamaasai, chanzo cha mgogoro ni wamaasai walipeleka ng'ombe wao mtoni kunywa maji.

Maji ya mto husika hutumiwa kwa matumizi ya kila siku majumbani na wakazi wa eneo hilo, ipo sheria inayokataza mifugo kupelekwa ndani ya mto kunywa maji ili kuzuia uharibifu wa mtiririko wa maji japo wamaasai hukaidi wanavijiji wanapowazuia.

Ukaidi wa wamaasai hutokana na wao kuruhusiwa kutembea na silaha za jadi ambazo huzitumia kuwadhuru wananchi, ila kwenye tukio hilo wananchi waliwazidi nguvu wamaasai na kuishia kuwakata mapanga ng'ombe.

Jeshi la polisi litumie busara ya usuruhishi kwenye jambo hilo japo wao wanauita ni uhalifu, hayo makundi mawili yanaishi eneo hilo na wanategemea mto huohuo, hivyo jeshi halinabudi kuwaelimisha wamaasai wafuate sheria za nchi kuhusu mazingira kwa kutopeleka ng'ombe ndani ya mto.
 
Hao wamasai warudi ngorongoro wafukuze waarabu na sio kupambana na watanganyika wenzao
 
Hao wamasai warudi ngorongoro wafukuze waarabu na sio kupambana na watanganyika wenzao
Mgogoro wa wamaasai na wenyeji wa Morogoro ulianza miaka ya tisini wakati makundi makubwa ya ng'ombe yalipoanza kuswagwa kuelekea Morogoro na pwani kisha kusini, hata hivyo kutokana na nguvu ya pesa waliyonayo wamaasai hakuna juhudi zozote zenye tija walizochukuliwa wamaasai.
 
Mgogoro wa wamaasai na wenyeji wa Morogoro ulianza miaka ya tisini wakati makundi makubwa ya ng'ombe yalipoanza kuswagwa kuelekea Morogoro na pwani kisha kusini, hata hivyo kutokana na nguvu ya pesa waliyonayo wamaasai hakuna juhudi zozote zenye tija walizochukuliwa wamaasai.
Kuna mwaka wakati sumaye waziri mkuu, alimtumbua mtu alikuwa mkuu wa wilaya akarudi kufundisha sekondary, ilikuwa mgogoro wa wamasai na wakulima, ye alikuwa anapewa Ela na wamasai anachuna tu.
 
Hahaha [emoji1787] usiombe wamasai wakuletee rushwa huwezi kataa kwakua ilikua ndio ndoto yako. Kula Pension kabla huja stafu.
 
Mgogoro wa wamaasai na wenyeji wa Morogoro ulianza miaka ya tisini wakati makundi makubwa ya ng'ombe yalipoanza kuswagwa kuelekea Morogoro na pwani kisha kusini, hata hivyo kutokana na nguvu ya pesa waliyonayo wamaasai hakuna juhudi zozote zenye tija walizochukuliwa wamaasai.
Nafikiri mropokaji amepata somo la bure hapa. Inasikitisha hata mambo ya msingi na hatari kama hili watu wanaingiza stress zao
 
Siku hizi nyuzi zinazoonesha matatizo ya wananchi hazidumu humu asiee. .. Max siku hizi naye sijui kalambishwa maokoto? Hii ni asal ndo inafanya haya.

Sio beat ya nape.
 
Tulikubaliana kuwa kila mtu abaki sehemu yake ya asili!

Wazaramo tuna banwa na watu mikoani na kusababisha joto kuongezeka
 
Back
Top Bottom