Pre GE2025 Mgombea huyu apewe onyo au Kuchukuliwa hatua kali ikibidi afungiwe kushiriki uchaguzi mkuu 2025 kwa kuanza Kampeni kabla ya muda

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)

Abraham Lincolnn

JF-Expert Member
Joined
Apr 12, 2018
Posts
2,754
Reaction score
4,975
Kwa Mujibu wa sheria za Uchaguzi ni kosa kubwa kwa Mgombea kuanza kufanya kampeni kabla ya muda maalum uliopangwa na Tume.

Kwa zaidi ya miezi miwili sasa, Bidhaa mbalimbali zenye nembo na chapa ya mgombea huyu zimekuwa zikionekana sehemu mbalimbali, Hii pia inaashiria dalili mbaya ya Rushwa ya Uchaguzi,

Pia TAKUKURU wanapaswa waingilie na kuchukua hatua kali. Ushahidi huu unatosha kabisa kwa TUME kuchukua hatua kwa mujibu wa sheria zilizopo.
 
Nina tatizo la kufananisha maneno...

Umesema 'afungwe au afungiwe'?

Keshateua mgombea mwenza ambaye anazunguka nchi nzima kueneza ilani😄😄😄

Wengine wanasubiri pazia lifunguliwe...wanajadili Tume na Katiba kwenye majukwaa ya vyombo vya KICHAWA.

Endeleeni na ujuaji mwingi.....
 
“Locuta causa finita” !
Hamna kesi hapo 😳🙄😀😅 !
Hata watoto wa wakulima wanajua hivyo !
 
Wapi omeandikwa "Mgombea Urais"?
 
Mbwa hawezi kuuma mkia wake. Halafu kuna mbweha wanataka wapinzani washiriki chaguzi hizi za kiini macho.
 
 
Mimi sielewi kama kweli tupo serios na hili suala la uchaguzi na sheria zake na miko yake. Huyu anayetajwa kufungiwa ni uonevu tu. Hebu angalia television zetu za channel 10 na clouds zinakampeni wazi wazi bila kificho nani achaguliwe. Kuna mtangazaji mmoja leo alikuwa anajinasibu jinsi anavyofaidi kuongozana na msafara wa Rais huko Tanga na pia alishaenda nae India mwisho anapiga kampeni achaguliwe. Angalia piki piki zilizosambazwa nchi nzima huku zimeandikwa initials za mgombea na rangi ya chama chake. Hivi kweli kuna upinzani hapa nchini? Mbona hawajafungua kesi. Kulikuwa na sababu gani kuzuia kuandikishwa chama fulani kipya cha siasa? Vinginevyo hakuna haja ya uchaguzi kwani mshindi anaeleweka na ameshajulikana
 
Ni ngumu sana kwa tume anayoichagua kumchukulia hatua kwa kuanza kampeni kabla ya wakati. Aidha, katiba yetu inasema huwezi kumshtaki rais aliyeko madarakani kwa kosa lolote analofanya. Inamlinda mkosaji!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…