Uchaguzi 2020 Mgombea Urais kupitia SAU, Muttamwega Mgaywa na mgombea mwenza wamewasili Ofisi za NEC peku kuchukua fomu

Hii inamaanisha nini kuenda peku peku?
Wamesema eti watanzania wao ni wakulima na wakulima wanalima peku, pia watanzania wengi hawana viatu so ni Kama kuwatia moyo wasio na viatu.
 
Bahati yao Niko mbali na hapo ningewatandazia mbigiri iwachome miguu
 
Walivua viatu kwa sababu za kidini na kuviacha kwenye gari. Hakuna lingine.
 
Muttamwega Bhati Mugaywa leo tarehe 7/8/2020 amechukua fomu ya kugombea uraisi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa tiketi ya chama cha Sauti ya Umma (SAU)
Katika Tukio hilo Mh Muttamwega aliongozana na Mgombea Mwambata wake Bi Satia Musa sambamba na viongozi wengine wa chama hicho akiwemo katibu mkuu wa chama hicho Majalio Paul Kyara na Mkurugenzi wa Propaganda wa chama hicho Kunje Ngombale Mwiru.

Tukio hilo la kusisimua na la kihistoria liliandamana na kubusu ardhi kabla ya kuingia katika ofisi za tume ya uchaguzi na kuingia katika ofisi hizo wakiwa wamevua viatu.
Msafara wa Mgombe

WAKATI MSAFARA UNAINGIA





MGOMBEA NA VIONGOZI WA SAU WAKIBUSU ARDHI

MARA BAADA YA KUBUSU ARDHI


vIONGOZI WA SAU WAKIINGIA OFISI ZA NEC MIGUU PEKU
kulia Mgombea Uraisi Mh Muttamega Bhati Mugaywa katikati Mgombea Mwambata Bi Satia Mussa na kushoto ni katibu mkuu wa SAU ndugu Majalio Paul Kyara



KATIBU MKUU AKIPEANA MKONO NA MWENYEKITI WA TUME YA UCHAGUZI WAKATI WA KUMTAMBULISHA MGOMBEA




BAADA YA KUKABIDHIWA FOMU


 
Hahaha vyama vya msajili, kwa kusherehesha na kutetea asiyeshinda.

Vyama havisimamishi mbunge, wala diwani kwanini urais?@
 
Watu ni wanafiki balaaaa hakiyanan njaa inauwa watu wazima
Fanyeni kazi achen tabia za shortcut
 
Mwaka huu tutashudia viroja sana, kubusu ardhi,kutembea pekupeku,kupiga push-up, kuruka kichura,kukata mauno .........yaani ni vibweka mwanzo mwisho. Ila mwisho wa siku CCM chaliiiiiiiii !!!!!!!

Sent from my Nokia 5.1 Plus using JamiiForums mobile app
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…