Mgombea wa ACT Wazalendo kata ya Mbagala Kuu akamatwa na kupigwa na Polisi akiwa kituo cha kupigia kura

Mgombea wa ACT Wazalendo kata ya Mbagala Kuu akamatwa na kupigwa na Polisi akiwa kituo cha kupigia kura

Mgombea wa Udiwani wa ACT Wazalendo Kata ya Mbagala Kuu, Shaweji Mketo amekamatwa na Polisi akiwa kituo Cha Kupigia kura ambako alikwenda kuzuia watu wasioandikishwa kupiga kura.Amejuruhiwa mguuni na Polisi akiwa mikononi mwao na sasa anapelekwa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa yaTemeke.

View attachment 1858888
View attachment 1858889
View attachment 1858889
Huyu Mgombea wa ACT- Wazalendo ni nini kilichomsukuma mpaka aende kituoni kuwazuia Wapiga Kura wasitekeleze haki yao ya msingi na kikatiba kuchagua vkiongozi wao. yeye alikuwa na ushahidi gani hawakuandikishwa wakati yeye si Msimamizi wa Uchaguzi? Kwani Mawakala wake alikuwa hawaamini kuwa wanaweza kutambua watu ambao hawajaandikishwa kwenye Daftari? Maana Mpiga Kura akiingia kwenye Kituo anatoa jina lake, halafu Msimamizi wa Kituo Namba Mbili anasoma jina lake kwa sauti ili Mawakala wasikie na kufuatia kwenye Daftari walilo nalo. Kama jina lake halipo kituoni hapo hawezi kuruhusiwa kupiga kura
 
Back
Top Bottom