Mgonjwa aliyetibiwa kifua kikuu anaweza rudia hali yake ya mwanzo au lah?

Juru

Senior Member
Joined
Jul 25, 2016
Posts
136
Reaction score
38
Hello member nimepata hamu ya kufaham ukweli kuhusu ugonjwa wa kifua kikuu maana una shambulia sehem nyeti za miili yutu hasa mapafu n.k, je kwa MTU ambae aliugua na kutibiwa anaweza kulud katika hari yake kama mwanzo au anaweza kushirikiichezo kama football au riadha nikiwa na maana ya kutoweza kupata shida ingine. Asanteni sana
 
Depends on how TB affect the patient, hata fungus zinaweza kuleta complications mtu akawa hata kichaa

Ila kama hakukuwa na complication yeyote anaweza kupona na kurudi kama zamani.
 
Depends on how TB affect the patient, hata fungus zinaweza kuleta complications mtu akawa hata kichaa

Ila kama hakukuwa na complication yeyote anaweza kupona na kurudi kama zamani.
Thank you v.much
 
La msingi pia ni mgonjwa kumaliza dose zake 6months Tb ni rahisi sana kutengeneza usugu endapo mgonjwa atacheza na dawa.

Kuna hatua nne za kutibu Tb
stage 1
stage 2
stage 3
stage 4...hii ni mbaya na hutokea pale Mgonjwa anaposhindwa kutumia dawa vizuri.

uwezekano wa kupona na kurudi kawaida upo kabisa
 
Asante sana mkuu nmekuelewa
 
Kuongezea waliyosema wadau hapo juu pia azingatie masharti atakayoshauriwa na doctor,mzee wangu mdogo Mungu amlaze pema aliumwa maradhi haya 2012 akatumia dose vizuri akamaliza akiwa na afya njema doc akamuamuru asivute sigara wala kunywa pombe{akitumia hizi pombe viroba}akapuuzia 2014 Mwananyamala Hospital aliiaga dunia huku akijiona.
 
Daaah pole sana broo
 
Majibu sahihi umepata. Jaribu kusafisha kiswahili chako basi. Maneno 'ludia' na 'hari' siyo sahihi!
 
TB ugonjwa hatari aisee eti nasikia mtu akishaanza dozi ni vigumu kuambukiz mtu mwingine?
 
Inawezekana. Mimi pia niliwahi kuugua. Na sasa Niko fit, na naweza kukimbia km 14 km. Cha muhimu ni kufuata masharti. Wacha pombe, sigara na pia sex kwa kipindi chote cha dawa. Pia chakula kizuri kama proteins ni muhimu
 
Inawezekana. Mimi pia niliwahi kuugua. Na sasa Niko fit, na naweza kukimbia km 14 km. Cha muhimu ni kufuata masharti. Wacha pombe, sigara na pia sex kwa kipindi chote cha dawa. Pia chakula kizuri kama proteins ni muhimu
Bigup sana broo
 
Umeshauliwa vizuri
Lakini lazima tuichambue huyo alikuwa na TB ipi
Ya mapafu ( pulmonary TB )
Or extra pulmonary TB

Maana causes zake ziko tofauti
.

Mwisho ,,, uwezekano wa TB kurudia ni upo,
 
Huu ugonjwa sikuwah kuzani kama ntaumwa maishani mwangu lakini bila kutegemea niliumwa mnamo mwaka 2011 nikiwa kijana mdogo kabisa nipo form 5 tabora boys. Ni ugonjw mbaya sana kwa dalili za awali unaweza sema ni mtu anayeumwa ukimwi. Watu wakawa wananiogopa na kuzani kuwa ntakufa siku yoyote na ukichanganya kuwa nilikua mbali na familia yangu. Nlbahatka kuhama shule, na kurudi kwa wazazi wangu Dar na kwenda hospital na kugundulika kuwa nina ugonjwa wa TB. Nikaanza dose mara moja na kupata msosi uliokamilika, DK akashauri kuwa naweza kuendelea na masomo hvyo nikahamia shule nyingine ipo morogoro. Nikiwa form 6.nilifuatisha mashart ya daktari kwa kumeza vidonge bila kukosa ndani ya miezi 6..
Namshukuru mungu nilimaliza dose nikapona nikiwa shule.
Sasa hivi ni Engineer.
TB inatibika kama ukifata mashart ya daktari.
 
Kuna mtu aliniambia TB ni dalili mojawapo kuna mtu ana ukimwi au watu wenye ukimwi wanashambuliwa sana na TB .... je kuna ukweli hapo?
 
Dogo, ondoa woga.Mm mwenyewe victim niliyetibiwa na kupo.a since April 2004.Nipo na shughuli zangu kawaida bila upungufu wowote ule.Muhimu zingatia masharti ya dr.Asilimia kubwa niliokuwa nipo nao kwenye trend waliishia njiani kwa kutifuata mashariti ya dr.usifanye kazi ngumu, fanya mazoezi mepesi,chakula ya kutosha.Ondoa wasiwasi.
 
Kuna mtu aliniambia TB ni dalili mojawapo kuna mtu ana ukimwi au watu wenye ukimwi wanashambuliwa sana na TB .... je kuna ukweli hapo?
Hapana unaeza kua na Tb na usiwe na ukimwi ni ugonjwa tu kama yalivyo magonjwa mengine, ila ninawajua watu wawili walikua na TB walipima na ukimwi wakakutwa nao.
 
Inawezekana. Mimi pia niliwahi kuugua. Na sasa Niko fit, na naweza kukimbia km 14 km. Cha muhimu ni kufuata masharti. Wacha pombe, sigara na pia sex kwa kipindi chote cha dawa. Pia chakula kizuri kama proteins ni muhimu
Hongera sana broo

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Inatibika fuata masharti ya dawa 2013 ilinipata nikanywa dawa for 6 months now nimepona na nimeingia gym vizuri tu ya kwangu ilisababishwa na matumizi ya AC kali
 
Mkuu mm niliugua hii kitu nikatumia dawa kwa kufuata utaratibu wa madakitari na sasa hivi nipo Mzimaaaa. Yaani hata ule mchezo wetu pendwa uleee na umudu tena zaidi ya awali [emoji1] [emoji1] [emoji1]

Kukimbia na kimbia tu kma zamani mkuu. Kuhusu kucheza football hapo sijui maana sijawahi cheza hata before. ila nmepona ka.bsa hivyo kma upo ktk hali hiyo usiogope kunywa dawa mkuu utapona kabsa
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…