Mgonjwa wa 14 apona Selimundu Hospitali ya Benjamin Mkapa

Mgonjwa wa 14 apona Selimundu Hospitali ya Benjamin Mkapa

Nehemia Kilave

JF-Expert Member
Joined
Jan 9, 2022
Posts
1,414
Reaction score
3,118
Haya ni maendeleo makubwa katika sekta ya Afya.

IMG-20240905-WA0032.jpg

Hospitali ya Benjamin Mkapa (BMH) imemuaga Faith Mwinula (9), ambaye ni mtoto wa kumi na nne kupona ugonjwa wa selimundu baada ya kupandikizwa uloto.

Ugonjwa wa Selimundu ni ugonjwa wa kuzaliwa nao kutokana na kuurithi kutoka kwa wazazi wa mtoto kupitia vinasaba.

Akiongea na Kitengo cha Mawasiliano na Uhusiano kwa Umma cha Hospitali, Mama mzazi wa mtoto, Pendo Luteja, amesema alipata taarifa kuwa BMH wanatoa huduma hiyo kupitia chombo Cha habari Cha televisheni (TV).

"Niliona kwenye TV wakati Mhe. Ummy (Waziri wa zamani wa Afya) anamtambulisha mtoto wa kwanza kupona sikoseli Bungeni baada ya kupata matibabu katika Hospitali ya Benjamin Mkapa," amesema mama mzazi wa Faith, ambaye ni mkazi wa Musoma, mkoani Mara.

Pendo amemshukuru Mkurugenzi Mtendaji wa Hospitali, madaktari na wauguzi kwa kuanzisha huduma hiyo, kwani imesaidia kuokoa uhai wa binti yake.

Soma Pia: Rais Dkt. Samia ametoa fedha shilingi bilioni 1 kwa ajili ya kutibu watoto 20 wenye ugonjwa wa Selimundu

"Namshukuru Mkurugenzi Mtendaji wa Hospitali kwa kufikiri na hatimaye kuanzisha huduma. Kwa kweli, imesaidia kuok
 
kwa Africa Tanzania ni namba mbili kwa madaktari bora
1-south Africa
2-tanzania
3-egypt
 
haya ni matunda chini ya uongozi makini wa chama cha mapinduzi ndugu
 
Nina swali huu ugonjwa niwakurithi vipi sasa huyo mtoto akija kupata watoto, watoto wake pia hawatakuja kuwa na huo ugonjwa..?
kwa maana nifahamuvyo urithi huu hutoka moja kwa moja kwenye Genetic! ama hiyo tiba inaondoa huo urith kwa offsprings wajao ufafanuzi tafadhari.
 
Nina swali huu ugonjwa niwakurithi vipi sasa huyo mtoto akija kupata watoto, watoto wake pia hawatakuja kuwa na huo ugonjwa..?
kwa maana nifahamuvyo urithi huu hutoka moja kwa moja kwenye Genetic! ama hiyo tiba inaondoa huo urith kwa offsprings wajao ufafanuzi tafadhari.
According to Okazaki fragments, zipping and unzipping of DNA double helix under polymerase chain reaction (PCR) oyaaa mwana mtafute Prof Janabi akupe majibu ya hivi vitu vya kitoto toto
 
According to Okazaki fragments, zipping and unzipping of DNA double helix under polymerase chain reaction (PCR) oyaaa mwana mtafute Prof Janabi akupe majibu ya hivi vitu vya kitoto toto
😂 umeanza vyema maharage uliyoleta mwishoni sijui ya nchi gani
 
Back
Top Bottom