Mgunda amenishangaza leo Mapinduzi Cup

Bila bila

JF-Expert Member
Joined
Dec 20, 2016
Posts
22,168
Reaction score
39,118
Akihojiwa na mtangazaji wa Azam TV baada ya kupoteza mechi dhidi ya Mlandege 0-1 amesema bado ana matumaini ya kushinda mechi 2 zilizobaki katika kundi lao C na kutinga hatua ya nusu fainali kutetea ubingwa wao.

Tangu ratiba inatolewa kundi C lilikuwa na timu 3 tu yaani;

1. Simba
2. Mlandege
3. KVZ

Mechi ya kwanza kwenye kundi hili ilikuwa baina ya Mlandege na KVZ iliyomalizika kwa sare ya 1-1 na Leo mechi ya pili Simba vs Mlandege.

Kwa maana nyingine Kundi limebakiza mechi moja tu Simba vs KVZ ambayo hata Simba akishinda anapata point 3 ambazo hazitamsaidia kuongoza kundi maana tayari Mlandege ana pwenti 4 na anahtajika mshindi mmoja tu.

Labda uelewa wangu kuhusu kanuni za mashindano haya siyo mzuri kiasi kwamba Simba kweli bado ana mechi 2?
 
Dah hata mimi nimeshangaa, duuh bonge la mbumbumbu!
 
Nipo Yanga lakini hili kombe wala si la kulichukulia serious, ni kama kombe la bonanza tu na lina nuksi ya timu kujikuta inabweteka wakati ndio kwanza lgi kuu ipo kati imepamba moto na FA bado mbichi...

Kama vipi wabebe wazenji tu wafurahie, hata Yanga hatuna kipaumbele nalo
 
Uko sahihi, Mgunda alikuwa na mhaho.
 
Swala la Mgunda kunyang'anywa majukumu kwa kupitia tweet ya Mo limemfedhehesha sana na mechi ya Leo ilikuwa lazima apoteze ili ionekane ni sahihi kuwa na kocha mpya
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…