Mgunda ni muhamasishaji mzuri ila siyo kocha mzuri

Mgunda ni muhamasishaji mzuri ila siyo kocha mzuri

ToniXrated

JF-Expert Member
Joined
Sep 21, 2022
Posts
1,134
Reaction score
2,993
Nimeiangalia Simba toka Kocha Mgunda anakabidhiwa timu msimu huu nikagundua kuwa ni muhamasishaji mzuri ila sio kocha mzuri. Tuwe wakweli, Simba inabebwa sana na uwezo binafsi wa wachezaji watatu kupata matokeo msimu huu, nao si wengine bali ni Chama, Phiri na Okra.

Mgunda amekuwa akihusika na kupanga kikosi cha timu kishikaji huku akiendekeza kitu kinachoitwa "Uzawa". Kwamba lazima wachezaji wazawa wacheze huku wale wenye viwango vya kimataifa tena waliosajiliwa kwa pesa nyingi kama kina Sakho, Banda, Okwa, Ouatara wakiendelea kulitumikia benchi wakati huo huo wachezaji ma-flopp kama kina Mkude, Nyoni na Bocco wakiendelea kupata namba.

Amekuwa akichezesha wachezaji nje ya position zao halisi. Hivi Phiri ni wa kumchezesha kama winga? Mgunda anahusika katika kufanya subs za ovyo kabisa. Anaona timu imezidiwa kati anamuingiza Bocco, anamuacha Mkude amalize dakika 90, ili hali hata kukimbia hawezi. anamuanzisha Nyoni mchezaji ambae hastahili kabisa kuvaa uzi wa Simba.

Wito wangu kwa uongozi wa Simba ni kuwa tutafute kocha wa maana, mwenye ujuzi na uzoefu wa kutosha tena atoke nje ya Tanzania, pia aje na benchi lake zima la ufundi ili kuja kuepusha upendeleo na yoendelea kwa jina la "Uzawa".
 
Ha ha ha ha haaaa.. dk 5 zilizopita nilikua naongea na Mdogo wangu namwambia tukifika home ukaingia JF au insta utakuta lawama za Mgunda tayari!!

Sasa game ijayo mkidraw au kufungwa Mgunda hana kazi, yaani Mikia hamnaga uvumilivu kabisa!
 
Sema wewe mtoa mada unaendeshwa na mihemko na unaonekana kabisa hujui mpira ina unaushabiki wa kijinga tu tangu lini Phiri akawa striker mzee? Phiri kiasilia ni winger ila alifanya vizuri kwa nafasi ya striker ndio maana simba walimuweka katika nafasi hio hivyo haikua mbaya kumuweka Kyombo ambae kiasilia ni Mshambuliaji na kakosa nafasi za wazi.
 
Nimeiangalia Simba toka Kocha Mgunda anakabidhiwa Timu msimu huu nikagundua kuwa ni muhamasishaji mzuri ila sio kocha mzuri.

Tuwe wakweli, Simba inabebwa sana na uwezo binafsi wa wachezaji watatu kupata matokeo msimu huu, nao si wengine bali ni Chama,Phiri na Okra. Mgunda amekuwa akihusika na kupanga kikosi cha timu kishikaji huku akiendekeza kitu kinachoitwa "Uzawa" .Kwamba lazima wachezaji wazawa wacheze huku wale wenye viwango vya kimataifa tena waliosajiliwa kwa pesa nyingi kama kina Sakho,Banda,Okwa,Ouatara wakiendelea kulitumikia benchi wakati huo huo wachezaji ma-flopp kama kina Mkude, Nyoni na Bocco wakiendelea kupata namba .

Amekuwa akichezesha wachezaji nje ya position zao halisi. Hivi Phiri ni wa kumchezesha kama winga??

Mgunda anahusika katika kufanya Subs za ovyo kabisa, anaona timu imezidiwa kati anamuingiza Bocco, anamuacha Mkude amalize dakika 90, ili hali hata kukimbia hawezi, anamuanzisha Nyoni mchezaji ambae hastahili kabisa kuvaa uzi wa Simba.

Wito wangu kwa uongozi wa Simba ni kuwa tutafute kocha wa maana, mwenye ujuzi na experience ya kutosha tena atoke nje ya Tanzania pia aje na benchi lake zima la ufundi ili kuja kuepusha favouritism nayoendelea kwa jina la "Uzawa".
Naunga Mkono Hoja.Simba itafute kocha Mkuu haraka mgunda abaki kuwa kocha msaidizi.Mgunda ni mhamasishaji na anaendekeza 'uzawa' bila kuangalia capacity ya mchezaji husika
 
Mgunda kocha hamna humo,,

Nikishazungumza mda mrefu sn,
Simba inabebwa na uwezo binafsi wa wachezaji kadhaa na sio uwezo wa kocha.

Tukija kishtuka ni too late.


Simba tafuteni kocha wa maana na sio kutuletea suruali kubwa uwanjani badala ya kocha.
 
Nakubali mzee wa za ndaaaaani kabisa, ulistahili ulipwe kutokana na hizi exclusive contents.Kwa hakika unalijua soka la bongo hasa katika figisu zake nje ya uwanja🤣🤣🤣🤣

Simba mmeuza mechi
 
Mgunda kufungwa mechi moja tuu makelele, mpeni ushauri na pia apewe muda. Tusiwe wepesi wakufukuza makocha
Nabi unbeaten mechi 44 na bado anataka kufungashiwa virago.

Kwenye ulimwengu wa soka la kibepari hakuna muda wa kusikilizia ni either u-perform au you go home.

Simba sio klabu ya kocha kuja kufanya majaribio.
 
Back
Top Bottom