Ili Tanzania iweze kupata maendeleo ni lazima makosa kama haya ya wazi wazi yaondoke ya kuwa na viongozi kwa maslahi yao binafsi na wasio kuwa na aibu hata punje moja. Mtu asiye na aibu kama inavyoonekana kwa Kawambwa ni hatari kwa taifa kwa kuwa malengo yake ni tofauti kabisa na matarajio ya wengi. Kinachoonekana hapa ni kwamba malengo la kawambwa siyo haya ambyo sisi wananchi wengi tunayatarajia na ndiyo maana anaweza kujitokeza hadharani kutetea matarajio yake kwa kuwa amefanikiwa kuhakikisha ameliangamiza taifa la Tanzania.
Haiwezekani katika hali ya kawaida Waziri, unatokea uharibifu mkubwa (janga) halafu yeye anenda kwenye media kuongea ujinga na hata dhamira yake haionyeshe kwamba kuna kitu kimeharibika. Huenda anataka kusikia wanafunzi wote waliomaliza kidato cha nne wamekufa wote ndiyo aweze kuona sasa hii ni hatari.
Hauwezi kwenda kwenye media kuongea kuwa wanafunzi wanafeli kwa sababu kuna shule nyingi za Serikali. Wakati sisi tuliposoma shule za Serikali zilikuwa bora kuliko hata Seminary, ajiulize what went wrong and why? siyo kwenda kuongea ujinga mtu na akili yake.
Kuna haja ya kuangalia uhalisia wa hiyo PhD yake maana pia anaidhalilisha.
Siku zote ninaamini, kiongozi mzuri ni yule anayeangalia nje ya dirisha na kutoa credits kwa watu/vitu vingine vinavyowezesha mambo kwenda vizuri na kujiangalia kwenye kioo na kujipa lawama pale mambo yanapokuwa hayaendi vizuri ili kuweza kujisahihisha kuliko kutumia lawama watu na wewe kutaka sifa tu. Kawambwa anataka sifa tu siyo kuwajibika. Eti watoto hawasomi ndiyo maana wanafeli, je amejiuliza kwa nini hawasomi. Wameandika kwenye karatasi za mitihani kuwa kuna masomo hawajawahi kuona mwalimu kwa miaka 4, hakuna vitabu hakuna maabara, walimu hawalipwi n.k yeye hayo hayaoni. Bajeti ya Wizara ya elimu imekuwa ikiongezeka mwaka hadi mwaka, lakini maendeleo ya elimu yamekuwa hakididimia mwaka hadi mwaka yeye haoni hilo.
Siku za karibuni hapa ilisemekana walimu wapo kwenye mgomo baridi yeye hataki kutumia elimu yake na muda kuangalia undani ili kupata ukweli na kutafuta suluhisho badala yake analaumi vitu ambavyo havina kabisa uhusiano wa moja kwa moja na elimu ya mtoto shuleni.
Jamani tupige kelele Kawambwa ajiuzulu kabla hayafanikisha kuliangamiza taifa kabisa. Mimi ninaamini hilo ndilo lengo lake.