Mh. Mwigulu Nchemba kutikisa Marekani na Uingereza mwezi mzima

Mh. Mwigulu Nchemba kutikisa Marekani na Uingereza mwezi mzima

Taswira

JF-Expert Member
Joined
Sep 23, 2012
Posts
1,198
Reaction score
447

MWIGULU NCHEMBA APASUA ANGA KIMATAIFA,SASA KUTIKISA MAREKANI NA UINGEREZA ZAIDI YA MWEZI MMOJA ---KUIMARISHA CCM KIMATAIFA,KUZUNGUMZA NA WATANZANIA KWENYE MATAIFA HAYO MAKUBWA DUNIANI.
CHADEMA WAWEWESEKA,YEYE AAHIDI KUKAZA KAMBA MWANZO MWISHO NDANI NA NJE YA NCHI.
nchemba.jpg
Ni kweli,ni uhakika,ni dalili za wazi kuwa Mh.Mwigulu Nchemba sasa hakamatiki,ni moto wa kuotea mbali katika siasa za nchi hii.Akabidhiwa beji ya kuimarisha chama kimataifa.Camera yetu imenasa habari za uhakika kuwa ,Mbunge wa Iramba Mgharibi na Naibu katibu Mkuu wa CCM-TANZANIA BARA Mh.Mwigulu Nchemba anaanza rasmi ziara yake ya kikazi,ziara ya kujenga na kuimarisha chama cha mapinduzi kimataifa,Ziara ya kuzungumza na vyama rafiki wa CCM ndani ya Marekani na Uingereza, ziara ya kuzungumza na watanzania kule kule waliko "MAREKANI NA UINGEREZA".

Mwigulu Nchemba anategema kuanza ziara yake siku ya kesho katika majimbo mbali mbali ndani ya Marekani na baadae kuelekea Uingereza katika miji ya West London,Birmigham,Reading Na Manchester kwa kazi maalum zifuatazo.

1.Mbunge huyo mwiba mkali kwa CHADEMA anategemea kuzunguka zaidi ya Mwezi Mzima Marekani na uingereza kufungua matawi mbalimbali na kuzungumza na wanachama wa CCM Katika Mataifa hayo makubwa mawili Duniani.


2.Pia Mh.Mwigulu Nchemba anategema kwenda kukutana na viongozi wa juu wa vyama vikubwa na vikongwe vya mataifa hayo mawili,Vyama rafiki vya CCM ndani ya Marekani na Uingereza.Hii ni fusa ambayo itatumika kujenga uimara wa CCM kidiplomasia hasa kwenye siasa za kimataifa.


3.Mbunge huyo anategemea kushiriki mkutano wa UN unaotegemea kufanyika mwishoni mwa Mwezi huu ndani ya WASHINGTON D.C (Hapa anategemea kupata uzoefu wa kukaa na kujadili mambo na mataifa makubwa duniani na viongozi wenye beji za heshima mbalimbali katika ulimwengu huu).


4.Pia Mh.Mwigulu Nchemba anategemea kuzungumza na watanzania karibia wote wanaoishi ndani ya nchi hizo mbili.Katika mambo muhimu anayokwenda kuzungumza ni pamoja na Katiba mpya,Maendeleo ya kiuchumi ndani ya Taifa letu,ajira,Amani na mwenendo wa siasa ndani na nje ya Tanzania.Pia anakwenda kujadiliana na watanzania maisha yao nje ya nchi na changamoto wanazokutana nazo.Kubwa zaidi anakwenda kuzungumza uimara wa CCM na uhakika wa kuendelea kuongoza nchi na namna watakavyobwaga upinzani kwenye uchaguzi ujao kwa sababu Upinzani Watanzania haujitambui,hawana malengo,ni vyama vyenye ubinafsi na ufamilia ndani yake hivyo havifai kupewa nchi.

KUWEWESEKA KWA CHADEMA,Paparazi wetu amenasa tetesi kuwa Viongozi wa juu wa CHADEMA wamesikia Taarifa za Mwigulu Nchemba kutua Marekani na Uingereza,jambo hilo linaonekana kuwapa wakati mgumu sana viongozi wa CHADEMA na kupelekea kufanya vikao vya ghafla vya hapa na pale na kufikia maamuzi ya kumwmbia Dr.slaa naye afunge ziara kwenda marekani siku tatu akajaribu kujibu mapigo ya Mh.Mwigulu Nchemba.
Kuweweseka huku kwa CHADEMA si mara ya kwanza,kila mmoja anakumbuka kuwa Mh.Mwigulu Nchemba aliporejea kutoka china baada ya kukutana na viongozi wa juu wa kikomunisti wa nchi ile,CHADEMA waliloa jasho,wamekuwa wakilia kila siku kuwa Mwigulu anawadhoofisha kisiasa na wamekuwa wakisema alikwenda china kwa lengo maalumu la kujifunza siasa za kisayansi.JE MWIGULU NCHEMBA AKIREJEA KUTOKA MAREKANI NA UINGEREZA CHADEMA MTAPONA KWELI???Mziki wa China tu imewafanya chadema wachuje kiasi kwamba inaonekana sio chama cha upinzani tena.Hii yote ni kazi ya mikono ya Mh.Mwigulu NChemba kuhakikisha upinzani hawafui dafu mbele ya CCM na kweli imewezekana.
Je ikirejea kutoka ziara ya Marekani tutegemee nini kama sio kifo cha chadema ama kusambaratika kabisa???
8E9U6377xx.JPG

Duru za habari zainaonesha wazi kuwa Mh.Mwigulu Nchemba ndiye kijana anayeandaliwa na watu wakubwa wanchi hii kuchukua nafasi ya Urais,Rejea kauli ya JK kuwa nchi hii hatamuachi mtu Mzee.BASI kaaa ukijua kuwa Mh.Mwigulu Nchemba anaandaliwa kiti cha kugombea Urais,na vijana wa CCM wanasubiria kwa hamu sana kuona Mbunge huyo anatajwa kuwa ndiye atapeperusha bendera ya CCM kwenye kiti cha Urais.
Hii ya Urais inaonekana kuwa mwiba sana Kwa CHADEMA kutokana na namna wanavyomuogopa Mbunge huyu,iwapo yeye ni mbunge tu amewashinda kisiasa kiasi hiki,Je akiwa Rais wanchi tutegemee kuiona chadema tena??Tusubiri macho yetu tu kuona chadema na vyama vya upinzani vikitafuta njia mbalimbali za kukimbilia.

Nilipojaribu kumtafuta Mh.Mwigulu Nchemba kuhusiana na ziara hii kama ni kwelu au la!!akaniambia "Ni kweli naeleka kikazi zaidi huko Marekani na Uingereza,napeperusha bendera ya nchi yangu na chama changu kimataifa,Nakwenda kukutana na viongozi mbalimbali wa vyama rafiki na CCM,nakwenda kuzungumza na Watanzania wenzangu,nakwenda kuimarisha chama na kufungua matawi ya CCM huko nje ya nchi,Nimezaliwa kwaajili ya kulitumikia Taifa langu na chama change CCM,Na furaha yangu ni kuona wale ninaopambana nao kwenye siasa wanakasirika kila siku kwani ni ishara ya wazi kuwa nawapiga kisawasawa na nitaendelea kufanya hivyo bila kukata tamaa." alidokeza.
7891139_orig.jpg

MY TAKE ::Mh.Mwigulu Nchemba anaziwezea sana siasa za nchi hii,na swaga zake za kijamaa "Chegua Vara,Fidel Castro n.k" atafika mbali sana.Na kwa Taifa hili lenye vyama vibovu vya upinzani tunahitaji mtu wa aina ya Mh.Mwigulu Nchemba.Huyu mbunge hana cha kulaza damu,yeye ni kazi kazi,ni MORINGE SOKOINE MWINGINE NDANI YA TAIFA LETU.
ASANTE.
 
viva CCM,VIVA MWIGULU NCHEMBA
 
kazi kwake chama kimemuamini sana afanye kazi aliyotumwa na chama tunataka vijana wenye bidii.
 
kazi kwake chama kimemuamini sana afanye kazi aliyotumwa na chama tunataka vijana wenye bidii.

kweli kabisa mkuu,kazi kwake kijana anaoneakana kuaminiwa sanaaaaaaaa na chama.safi sana
 
......
..........Hii kasi haizuiliki!!!!!!!

.....wakufyonza Karibu tena Arusha.....
 
MWIGULU NCHEMBA APASUA ANGA KIMATAIFA,SASA KUTIKISA MAREKANI NA UINGEREZA ZAIDI YA MWEZI MMOJA ---KUIMARISHA CCM KIMATAIFA,KUZUNGUMZA NA WATANZANIA KWENYE MATAIFA HAYO MAKUBWA DUNIANI.
CHADEMA WAWEWESEKA,YEYE AAHIDI KUKAZA KAMBA MWANZO MWISHO NDANI NA NJE YA NCHI.​


Upuuzi usio na tija wa kujijibu.
 
siasa kama za akina Mwigulu Nchemba zinahitajika sana hapa tanzania
 
Atatikisa marekani na U.K ataweza mfu huyo!
 
VIVA Mwengulu, Viva Sii Sii Eeeeem, Ukirudi uwasaidie CDM kwenda kujisajili upya. Ama kweli si lazima uokote makopo ndipo tukupeleke Mirembe. Ukiwaza kwa kupiga kelele tunaweza pia kukupeleka huko. Kama unapiga yowe kuwa unaenda kuiba na unapitia Police Central lazima wakukamate.
Si, Nape kasema CDM walipewa mchango wa mshiko kuja kuharibu mchakato wa katiba na nchi hizo hizo anakoenda Mchemba jamani au nilisikia vibaya?
Mwingulu, sema unataka kutakatisha fedha flani flani ulizoleta China juzi kati hapa. Ukianza kuzimwaga useme ulipewa Marekani na UK. Sawa mkuu tumekusikia, tumeona matangazo yako kuwa unasafiri kwa wakubwa huko kuomba msaada wa kuibomoa na kuiteketeza kabisa CDM. Sisi CDM hatutishwi na fedha haramu ambazo ni lazima zikatakatishwe kwa safari ya USA na UK.
Ati kiboko ya CDM, naona huyo ndiye aliyeandaliwa na Mungu kuimaliza kabisa CCM. Just mark ma words. Mlianza kushambulia kuwa CDM wamepewa fedha nyingi sana huko ugaibuni ili nyie mpate huu mlango wa kutakatishia hizo fedha haramu lakini tunalijua hilo. Akirudi na neti za mbu za matundu makubwa sawa. Huo ndio msaada mnaoweza kupewa huko. Lakini akirudi na uwezo mkubwa kifedha, twajua hiyo ni Janja tuuu.
Mataifa hayo wameshajua moto wa CDM. Haufunikikiiiiiii. 2015 inavyozidi kukaribia mtaweweseka saana tu.
 
Huyu mtu mara ya kwanza kutoka nje ya Tanzania ni pale alipoenda juzi China. Nasikia kila kitu alikuwa anashangaa. Sasa leo wanampeleka Amerika atajinyea atatangazia wanyiramba wote kila kona. Asijue kwamba wenzake walishawahi kuishi huku na wengine hadi leo wapo huku. Ulimbukeni kitu cha hatari sana.

Ajitahidi ajifunze Kiingereza kidogo!!
 
Safari yake asiwasahau wapendwa wake (Mtela na Juliana)!!!!!!
 
Jembe jembe jembe...
Hilo ndilo Jembe la tanzania bhana.
Naamini huko atatakata sana tu.
 
Wapiga kura wako wanalalamika njaa kali sana mwaka huu hadi wanalazimika kuuza Vindege, ujugu, ukwaju na ubuyu kuendesha maisha yao ya kila siku, ukikaa huko mwezi mzima utakuwa huwatendei haki.

By the way sijawahi kumsikia Mwigulu akiongea kidhungu sa sijui anaenda na mkalimani....
 
Ushamba mbaya sana wajamani,sasa mlughalugha kama huyu atazungumza nini mbele ya watu ambao wana smart brains na ni watetezi wazuri wa human rights?Je na ile cap yake atavaa?

Sent from my BlackBerry 9300 using JamiiForums
 
IRAMBA magharibi wamlilia mbunge wao Mwigulu Mnchemba.



Wanasema ukistaajabu ya Mussa utaona ya Mwigulu,
Wakati mbunge wa Singida magharibi Mhe. Mwigulu Mnchemba anapasua masafa ya nchi wapiga kura wake wanamlilia kweli aende akawasikilize matatizo yao kwani shida zimewakaba hadi shingoni. Wanamstaajabu mbunge wao ambae wakati rais wake anachanja mbuga duniani yeye mbunge anachanja mbuga inchini akiwawakilisha wanainchi ambao hawakumchagua akiwaacha wao katikati ya lindi la matatizo. Nimepita jimboni mwa huyo mbunge wapiga kura wake wakanieleza yafuatayo kwa mdomo wao:-
Shida zinazowakabili-


1. Njaa kali.



Wana uhaba mkubwa wa chakula mvua zilikuwa haba sana ukitilia maanani wenywe wako kwenye bonde la ufa inabidi kupata mvua za kutosha ili wavune mtama (lugugu) wacha mahindi, kwa hiyo wanauhaba mkubwa wa chakula familia nyingi karibu % 90 katika jimbo la Mwigulu wanakula mlo mmoja na huo mlo mmoja hawashibi. Watoto wa shule wanashindwa kwenda shule shauri ya njaa, pia wakirudi nyumbani saa 6 wanalala inje ya nyumba shauri ya njaa kali ndani hamna kitu na wazazi wao hawapo wamekwenda kutafuta vibarua, wengine wanazirahi.


2. Umasikini wa kipato.



Wanaumaskini mkubwa wa kipato wachilia mbali njaa inayowakabili, hawana zao lolote la maana la biashara,ajira wanayoitegemea ingalao kupata kipato ili kutatua matatizo yao ni ombaomba kwenye treni, na biashara za ovyoovyo kwenye treni yakati biashara kama kuuza ujugu, vikapo , vindege, vifilimbi vya miti, ukwaju na ubuyu, ni vibiashara vya kijinga jinga tu, vijana wengi wamekimbia jimbo wasichana kwa wavulana wameenda kutafuta ajira mjini na wengine wameenda kutafuta vibarua vya kulima tumbaku katika vijiji kata ya Igwisi urambo.


3. Ukame mkali.



Kuna ukame wa hali ya juu, ukame unawakabili watu na mifugo, mifugo kuanzia vijiji vya Kintinku, Igose, Makutupora Kirimatinde Salanda, Ulyampiti, Msigili hadi Sherui mifugo wanakunywa mgwao, yaani wanakunywa leo siku inayofuata hawanywi maji.Maji yenyewe wanayapata kwa kuesea kwa kutumia Nkosi,wanadamka usiku kwenda kwenye visima walivyochimba wenyewe ili kuchotelea maji kwa kutumia nkosi na kujaza mrambo ili mchana mifugo waje wanywe, kazi hiyo ni ngumu sana inawafanya vijana wengi kukimbia makazi yao au kuwa ni ajira kwa wenye uwezo, mtu unafanya kazi hiyo ngumu halafu anaishia kupewa chakula tu jioni.


4. Wizi wa mifugo.


Kuna wizi wa mifugo wa hali ya juu, hii ni kutokana na njaa kali, mifugo inaibiwa nyumbani usiku au mchungaji ananyang`anywa mchana kweupe machungani, mifugo inaibiwa kiasi kuna tishio la mifugo kwisha kwa wizi, wengine huiba mbuzi na kwenda kuchinja polini na kuishia kula nyama shauri ya njaa.
5. Magonjwa:



Tunakabiliwa na magonjwa ya kuambikiza, magonjwa yanayotusumbua ni Malaria na kichocho, malaria inatusumbua kwa ajili ya joto hapa jimboni kwa Mwigulu ni bonde la ufa yaani ardhi imetitia chini hivyo joto kweli usiku na mbu ni wengi , kwenye vituo vya kutolea pia uwezo wa kukata bima ya afya hatuna kwa sababu ya umasikini wa kipato, Kichocho kinasumbua sana hasa wanafunzi ,shule kama Ndago karibu wanafunzi wote wana kichocho dawa ya Parazenguantel hamana katika vituo vyote hadi hospitali ya mkoa ya Singida, halafu dawa yenyewe ni ghali. Pia jimbo la Iramba magharibi karibu lote linakabiliwa na tatizo la mishoo kwa ajili ya kula nyama mbichi za wizi.


6. Mimba kwa wanafunzi wa shule za msingi na secondary


6. Mimba kwa wanafunzi wa shule za msingi na secondary zimekidhili jimbo la Iramba magharibi katika majimbo yote ya singida Ilamba magharibi ndio inayoongoza kwa mimba za utotoni na kwa wanafunzi mashuleni, wanaowapa mimba wanawapa rushwa wazazi wao halafu hawawapeleki panapohusika ili sheria ichukue mkondo wake yeye Mwigulu mguu na njia hayaangilii haya jimboni kwake kazi kuitangaza CHADEMA tu.


Ushauri kwa Mbunge wa Mwigulu



Aje akae jimboni ili waweze kusaidiana kukabili matatizo haya , huko unakozurula kwani ndiko walio mchagua? Aache kuhangaika na LEMA kwani mbunge huyo hamwezi wanaweza wenyewe waliomchagua. Kupenda ni sehemu ya uhai , kumeambatana na uhai kupenda hakuwezi kwisha mpaka uhai umetoweka kwa hiyo kama Arusha wanampenda mbunge wao Mwigulu hata ufanyeje unajisumbua tu njoo jimboni utusaidie wapiga kura wako tunakwisha. Huyo LEMA unayempiga vita yeye anawapigania wapiga kura wake hadi saa ingine bungeni haendi hadi anafungwa jela mahabusu wewe Mwigulu unazurula tu unatusahau,

Kama mbunge una uwezo kutusaidia kupata dawa hasa za kichocho, kulobe chakula kije jimboni ingalao tutanua, Kwenye jimbo la Tundu Lisu mashuleni wanafunzi wanapata mlo wa mchana kupitia Pragram ya WFP, Mbunge wetu Mwigulu yuko wapi na sisi tupate mpango huu. Njoo tusaidiane kuandaa mkakati wa kukabiliana na wizi wa mifugo, njoo tujipange tuweze kukata bima za afya kwa watendaji wa kata ingalao zituwezeshe kupata matibabu hata hayo kiduchu.
Mbunge wetu Mwigulu njoo jimboni sisi wapiga kura wako tunakulilia kwani hiyo jeuri uliyopewa na Rais kwamba wewe unakabiliana na wapinzani hukimbilii polisi isikuvimbishe kichwa kiasi unasahau wajibu wako. Wacha kujishebedua na mkutano huko Dar. Njo site uone mwenywe serikali ya chama chako ilivyotufanya mbaya kwa kutufanya tuwe maskini wa kutupya, ile kambi ya wakoma ya sukamahela imeanza kujaa tena wengi wa wagonjwa wanatoka wilaya ya Iramba.
 
Back
Top Bottom