Mh.Rais hongera kwa hotuba yako nzuri ktk hafla ya kupokea ripoti na rasimu ya katiba

Mh.Rais hongera kwa hotuba yako nzuri ktk hafla ya kupokea ripoti na rasimu ya katiba

mbeyaman

Member
Joined
Sep 28, 2013
Posts
97
Reaction score
28
Hakika umezidi kudhihirisha ya kwamba wewe ni rais wa watu,rais wa Watanzania wote bila kujali makundi ya kisiasa yanayojaribu kutaka kuhodhi mchakato wa kupatikana katiba mpya.Umewapasha waziwazi baadhi ya makundi hasa ya vyama vya siasa kushinikiza katiba mpya iwe na matakwa yao ya kisiasa au kimakundi. Juhudi zako za kupatikana kwa katiba mpya ni jinsi gani unavyoguswa na mabadiliko ya kisiasa,kiuchumi,kijamii ktk nchi yetu kwa mustakabali wa Taifa letu.Watanzania wote tunaunga mkono na kutambua juhudi zako za kutuongoza ili tupate katiba mpya kwa faida ya Watanzania wote na Ulimwengu kwa ujumla.Vile vile uongozi wako wenye tija ni tunu kubwa kwa Watanzania na Waafrika kwa ujumla.MUNGU AZIDI KUKUBARIKI KTK JUHUDI ZAKO ZA KUWATUMIKIA WATANZANIA.
 
Samahani mkuu unaweza kutuwekea hiyo hotuba hapa japo tuipitie na sisi tulio mbali na home?
 
Hakika umezidi kudhihirisha ya kwamba wewe ni rais wa watu,rais wa Watanzania wote bila kujali makundi ya kisiasa yanayojaribu kutaka kuhodhi mchakato wa kupatikana katiba mpya.Umewapasha waziwazi baadhi ya makundi hasa ya vyama vya siasa kushinikiza katiba mpya iwe na matakwa yao ya kisiasa au kimakundi. Juhudi zako za kupatikana kwa katiba mpya ni jinsi gani unavyoguswa na mabadiliko ya kisiasa,kiuchumi,kijamii ktk nchi yetu kwa mustakabali wa Taifa letu.Watanzania wote tunaunga mkono na kutambua juhudi zako za kutuongoza ili tupate katiba mpya kwa faida ya Watanzania wote na Ulimwengu kwa ujumla.Vile vile uongozi wako wenye tija ni tunu kubwa kwa Watanzania na Waafrika kwa ujumla.MUNGU AZIDI KUKUBARIKI KTK JUHUDI ZAKO ZA KUWATUMIKIA WATANZANIA.


maisha bora kwa kila mtanzania imeota mbawa sasa anaficha mazaifu yake kwenye Katiba yetu.
 
Jk aliwaambia ccm wajiandae kisaikolojia kupokea rasimu ya pili, sasa hatutaki kusikia mheshimiwa fulani kalazwa moi kwa shinikizo la damu, rais aliwaasa mapeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeema
 
Mkuu Munabusule mh.Rais kawachana live na kuwaambia katiba mpya itakuwa ngumu sana iwe na mambo ambayo kila kundi linataka...akazidi kuwachana kwamba haiwezekani katiba ifuata matakwa ya kila kundi...amesema katiba ni ya Watanzania...
 
Mkuu Munabusule mh.Rais kawachana live na kuwaambia katiba mpya itakuwa ngumu sana iwe na mambo ambayo kila kundi linataka...akazidi kuwachana kwamba haiwezekani katiba ifuate matakwa ya kila kundi...amesema katiba ni ya Watanzania...
 
Hakika umezidi kudhihirisha ya kwamba wewe ni rais wa watu,rais wa Watanzania wote bila kujali makundi ya kisiasa yanayojaribu kutaka kuhodhi mchakato wa kupatikana katiba mpya.Umewapasha waziwazi baadhi ya makundi hasa ya vyama vya siasa kushinikiza katiba mpya iwe na matakwa yao ya kisiasa au kimakundi. Juhudi zako za kupatikana kwa katiba mpya ni jinsi gani unavyoguswa na mabadiliko ya kisiasa,kiuchumi,kijamii ktk nchi yetu kwa mustakabali wa Taifa letu.Watanzania wote tunaunga mkono na kutambua juhudi zako za kutuongoza ili tupate katiba mpya kwa faida ya Watanzania wote na Ulimwengu kwa ujumla.Vile vile uongozi wako wenye tija ni tunu kubwa kwa Watanzania na Waafrika kwa ujumla.MUNGU AZIDI KUKUBARIKI KTK JUHUDI ZAKO ZA KUWATUMIKIA WATANZANIA.

hivi mtu ukimkubali wewe ndo wamemkubali watanzania wote acha kuwazungumzia watu ktk fikra zaki wewe acha kujipendekeza
 
1.UONGOZ WAKE UNA TIJA GANI KWA WATZ HASA WATU WA MTWARA AMBAO ALIWATUMIA JWTZ KUWAUA KWA MASLAHI YAKE BINAFSI NA MABWANA ZAKE WAWEKEZAJI WA NJE?

2.UONGOZI WAKE UNATIJA GANI KWA WANYAMONGO AMBAO WALIUAWA KWA: a)SUMU YA MGODI WA NORTH MARA GOLD MINE NA SERIKALI HAIKUCHUKUA HATUA MPAKA WALEO KWA MASLAHI YA MABWANA ZAKE,WAWEKEZAJI WA NJE?, b) RISASI NA POLISI NA KISHA WAUAJI (POLISI) HAO KUIPORA MIILI YA MAREHEMU TOKA MOCHWARI NA KUITELEKEZA POLINI?
3) UONGOZI WAKE UNATIJA GANI KWA RAIA WALIOBUGHUDHIWA NA KUULIWA MIFUGO NA NDUGU ZAO NA JWTZ CHINI YA OPERESHEN TOKOMEZA UJANGILI HUKU RAIS AKIJUA FIKA KUWA KINANA WAKE NDIYE KINARA WA UJANGILI WA MENO YA TEMBO NA SIO WAKULIMA NA WAFUGAJI?

PLZ! ACHAGENI KUFIKIRI KWA KUTUMIA `BATAKO'.
 
hivi mtu ukimkubali wewe ndo wamemkubali watanzania wote acha kuwazungumzia watu ktk fikra zaki wewe acha kujipendekeza

Na ukimkataa wewe pia wamemkataa watanzania wote?? Wakati mwengine tuache siasa Raisi Kikwete hotuba yake ni njema kwa taifa
 
Kwakweli naomba nimpongeze Rais Kikwete kwa jinsi alivyosoma hali ya upepo na kuamua kuweka mambo yote hadharani. Huu nu upeo wa hali ya juu kabisa.

Lakii zaidi ni jinsi Mze wariobaalivyoweza kuonesha bila woga hisia za watnzania.

KARIBU TANZANIA TUNAYOITAKA.
 
Speaking from hotuba ya leo mh rais kaongea mambo ya mcngi sana katiba ni issue ya taifa zima sio ya makundi fulan either ya dini, siasa au kabila fulan ni ya taifa lote ni lazima tuweke pemben ili tupate katiba nzur .... .
 
BABAAKUBWA acha mawazo mgando...hizo hoja ulizozileta hazina mashiko...matukio yote uliyoyataja yanamuhusisha vipi mh.Rais?...ukubali ukatae hotuba ya JK ni ishara njema kupata KATIBA MPYA YENYE KUKIDHI MATAKWA YA WATANZANIA WOTE.Hapa hatuzungumzii kuhusu matukio ya Mtwara,Nyamongo wala operesheni Tokemeza...mada kuu ni hotuba nzuri ya mh.Rais JK iliyojaa HEKIMA,BUSARA,UZALENDO NA UTAIFA.
 
Jk aliwaambia ccm wajiandae kisaikolojia kupokea rasimu ya pili, sasa hatutaki kusikia mheshimiwa fulani kalazwa moi kwa shinikizo la damu, rais aliwaasa mapeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeema

Huyu hapa hawezi kukosa shinikizo la juu kupita kawaida na kupoteza fahamu kabisa. Ndugu zake kaeni naye karibu.
View attachment 129484
 
Samahani mkuu unaweza kutuwekea hiyo hotuba hapa japo tuipitie na sisi tulio mbali na home?
Si rahisi maana kawaida huongeza maneno wakati akiitoa, hivyo speach writer wake lazima wakae na kuandika upya. Tuisubiri ya sauti
 
hotuba ya rais si shida sikuzote amekuwa na hotuba nzuri bado kwenye majanga ( mjengoni) hapo ndipo hutasikia wanapitia katiba hiyo kifungu kwa kifungu na kurekebisha vifungu vyote vilivyoandikwa na wataalamu vizuri, CCM itatumia 3/4 ya wabunge wote kupinga hoja moja baaada ya nyingine kwa hali hiyo msifurahiye hotuba nzuri ya Jk bali tusubiri mjadala utakavyo kuwa bungeni. kama wabunge watakuwa na maslahi kwa taifa itapendeza zaidi
 
Pongezi kwako mheshimiwa Rais Jakaya Mrisho Kikwete kwa hotuba yako ya kiamiri jeshi si ya kisiasa. Hongera sana kwani umeonyesha ujasiri na ushujaa wa hari ya juu . watanzania wengi tunajua jinsi gani chama chako hakiko tayari kuyakubali hayo mabadiliko ya kikatiba. Nasema sana for good speech
 
Pongezi kwako mheshimiwa Rais Jakaya Mrisho Kikwete kwa hotuba yako ya kiamiri jeshi si ya kisiasa. Hongera sana kwani umeonyesha ujasiri na ushujaa wa hari ya juu . watanzania wengi tunajua jinsi gani chama chako hakiko tayari kuyakubali hayo mabadiliko ya kikatiba. Nasema sana for good speech
 
Pongezi kwako mheshimiwa Rais Jakaya Mrisho Kikwete kwa hotuba yako ya kiamiri jeshi si ya kisiasa. Hongera sana kwani umeonyesha ujasiri na ushujaa wa hari ya juu . watanzania wengi tunajua jinsi gani chama chako hakiko tayari kuyakubali hayo mabadiliko ya kikatiba. Nasema hongera sana for good speech
 
Back
Top Bottom