Mh, Waziri Mkuu: Vyama Vikuu vya Ushirika vya SHIRECU na NCU vilitia umasikini wakulima wa Kanda ya Ziwa kwa wizi; kama wahusika wapo, wakamatwe.

Kididimo

JF-Expert Member
Joined
Sep 20, 2016
Posts
4,153
Reaction score
3,800
Awali ya yote, niipongeze TAKUKURU kwa namna wanavyoshughulikia wezi wa fedha na mali za vyama vya ushirika. Nimeona kule Kusini hasa zao la Korosho, wezi wakiamriwa kurejesha mamilioni ya fedha, Tabora nako nimeona.

Kwa Mikoa ya Shinyanga na Mwanza, kuna Vyama viwili vya SHIRECU (Shinyanga) na NCU( Mwanza), ambavyo vilijihusisha na ununuzi wa mazao hasa pamba miaka ya nyuma. Siyo jambo la kificho,ukweli ni kuwa vyama hivi vilifilisika kwa sababu ya wizi.

Kulikuwa na viongozi ambao baadhi wapo hadi leo walivifanya kama vile ni mali za familia zao na ndugu zao.

Leo hii, ukipita kwenye Ginneries na vituo vyao utatamani kulia kwa namna mali zilivyotelekezwa huku zikioza bila hata kuhifadhiwa. Ikumbukwe hizi ni mali za wananchi,wakulima.

Kuna tetesi zilikuwepo kuwa,Ofisi ya Waziri Mkuu katika awamu zilizopita ilianza kushughulikia hili jambo japo taarifa kamili haikutolewa.

Mali hizi ni mali za Umma, zinaoza peupe kama hazina mwenyewe. Wahujumu wa hivi vyama ni vyema wapatikane,watendewe haki kama inavyofanyika maeneo mengine.
 
Majizi yanajulikana ni kutoka kile chama cha akina lugola, wizi ukiwa designed kwenye ilani anayotembea nayo Lugo
 
Laana ilianzia pale CCM ilipodhulumu mali za wananchi na kuzifanya za kwake, viwanja vya mpira vilivyojengwa kwa nguvu za wananchi, majengo mbalimbali na viwanja vya wazi..

Siku nikiwa Rais wa nchi hii jambo la kwanza ni kuchukua mali zote za CCM na kuzirudisha kuwa mali ya Tanzania kwa maana ya Serikali ya Tanzania na mapato yako yatarisha yatima na wazee wote wasiojiweza kwenye kambi mbalimbali..

Bila kuifuta CCM kwenye nchi hii hakuna siku matatizo yataisha Tanzania..
 
Mkuu ukifuatilia viongozi wa vyama vyote hivyo vya ushirika utakuta woote ni makada wa CCM.

In God we Trust.
 
Watanzania wote tukuombee utimize ndoto yako maana ni bora kabisa
In God we Trust
 
CCM ni taasisi ambayo nafikiri ilijengwa kwa namna ya mfumo wa Mafia Mob pale Sicil, unaweza kuta hata Mwenyekiti wa Chama ana bosi wake ambaye hamjui..

Siku watanzania na wanaCCM wakimjua mmiliki halisi wa CCM na malengo yake na namna anavyowatumia wanaCCM kuwatawala na kuwatesa watanzania wenzao basi utatokeo ugomvi mkubwa sana..

Wale wanaosoma historia za makundi kama Mafia Mob pale Sicily na Costra nostra, Sinaloa Cartel pale mexico, Black axe, na ----------- ambao ndio wamiliki wa CCM Tanzania wataelewa namna mfumo wa CCM ulivyo..
 
Viongozi wa vyama hivyo pamoja na wizi wao uliokithiri lakini walikuwa wakiabudiwa na wanyonywaji kama miungu watu.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…