Mhalifu ni nani ndani ya Ole Sabaya?

Mhalifu ni nani ndani ya Ole Sabaya?

Ferruccio Lamborghini

JF-Expert Member
Joined
Apr 15, 2020
Posts
1,667
Reaction score
2,595
ALIYEKUWA Mkuu wa Wilaya ya Hai, Lengai Ole Sabaya, alifikishwa mahakamani jana. Ni matokeo ya tuhuma zinazomuandama kwa muda mrefu sasa.

Yameshasemwa na yanaendelea kusemwa mengi. Hisia ni tofauti kuhusu yanayomtokea Sabaya. Kila mtu anataka aseme kitu. Nami nimeshaulizwa kwa nini sisemi chochote. Ngoja basi nitoe neno. Nitachukua muktadha maalum, bila kuingilia uhuru wa mahakama.
Tuhuma za Sabaya ni nyingi, zinaogopesha. Zinashangaza kupita kiasi. Zinahitaji akili ya juu mno kuzichambua. Ukizichukua tuhuma za Sabaya na kuziweka kwenye kapu la uhalifu sawa na uhalifu mwingine, hilo ni kosa kubwa.

Tafakari, Sabaya ni binadamu. Kila binadamu ana ubinadamu, vinginevyo kuwe na shida kwenye ubinadamu wake.

Tafakari zaidi, Sabaya akateuliwa kuwa Mkuu wa Wilaya. Kazi ya kutumikia wananchi. Binadamu wenzake. Kila binadamu anafamu wito wa ubinadamu ni kuwatendea haki binadamu wenzake. Vinginevyo ubinadamu wake uwe na upungufu.

Inafahamika, kuchaguliwa au kuteuliwa kuwa kiongozi ni zawadi kubwa mno. Kuilipa hiyo zawadi si kufanya chochote isipokuwa kuwatumikia watu kwa upendo na uadilifu.

Sabaya akiwa mkuu wa wilaya, akawa anatuhumiwa kupora mali za watu, kuonea anaowaongoza. Kulazimisha mapenzi kwa wanawake na hata kubaka. Hizo tuhuma ukizisikia, kama una kichwa kizuri lazima kwa asilimia 50 utadhani anasingiziwa.

Ni kwa sababu, mtu mwenye akili timamu hawezi kufanya hata robo ya yale anayotuhumiwa nayo Sabaya.

Mtu mzima anawezaje kuteka wake za watu na kulazimisha mapenzi? Anaingiaje kwenye hoteli na kulazimisha aoneshwe chumba cha mteja mwanamke, ili iweje? Anawezaje kulazimisha wafanyabiashara wampe pesa bila kufanyia kazi? Anawezaje kuteka watu na kuwatesa? Anafyatuaje risasi hovyo? Mtu mwenye akili timamu kweli?

Kwa kiongozi, vitendo vyote hivyo kwa sehemu kubwa vinanajisi uongozi. Je, Sabaya kama mtu timamu, hakutambua uongozi ni upendeleo na ulinzi wake ni uadilifu?

Ndio maana nikasema, tuhuma za Sabaya kwa asilimia kubwa hukaribisha hisia kwamba anasingiziwa. Maana mtu mwenye akili timamu hawezi kufanya japo robo ya vitendo anavyotuhumiwa navyo Sabaya.

Sasa, hata baada ya kufikishwa mahamani, lipo eneo la kulisemea. Ni namna ya kuingia ndani zaidi kwenye tuhuma zake.

Nimeshasema, ni kosa kubwa kuziweka tuhuma za Sabaya katika kapu moja la uhalifu, sawa na uhalifu mwingine.

Kama yote ambayo Sabaya anatuhumiwa nayo ni kweli kayatenda, basi uhalifu mkubwa upo kwenye namna ubongo wake unavyofanya kazi. Inawezekana haupokei na kutafsiri mambo kama binadamu wa kawaida.

Kama ndivyo, hata sasa akiwa mahabusu, inawezekana akawa haelewi kwa nini amekamatwa, kwani yote aliyokuwa anafanya (ikiwa ni kweli), yeye anaona alikuwa sahihi. Tena, si ajabu anajiona anasingiziwa.

Watu wenye namna ya kipekee katika kupokea na kutafsiri mambo kijamii huitwa "psychopath". Ni tafsiri sawa na mgonjwa wa akili. Kwa kawaida psychopath huwa wana matatizo ya afya ya akili.

Kama kutakuwa na dhamira ya kumtendea haki Sabaya, basi itabidi kumpima afya ya akili. Maana, kama kweli alitenda yote anatuhumiwa nayo, maana yake atakuwa psychopath. Mtu timamu asingethubutu kufanya hata moja ya 10 ya anayotuhumiwa kufanya.

Binafsi ningetamani, kabla hata hajafikishwa mahakamani, wakati wa kumhoji Sabaya ili kukamilisha taarifa za mashitaka dhidi yake, kungekuwa na wataalamu wa afya ya akili katika mahojiano.

Hapa sipendekezi Sabaya apewe msamaha kama tuhuma dhidi yake zina ukweli, la, haki itendeke. Wahalifu wenye matatizo katika afya ya akili hufungwa, ila kuna namna ya kuwasaidia kipindi wanatumikia adhabu zao.

Kinachonishawishi kuona ulazima wa Sabaya kupimwa afya ya akili ni kwa sababu nataka kujua ubongo wake ulikuwa unawaza nini alipokuwa akitenda uhalifu alioutenda. Hii ni kama kweli alitenda.

Je, ubongo wake ulikuwa unawaza nini? Kwamba yeye ni mkubwa sana kwa hiyo angetenda chochote kwa watu bila lolote kumrudia? Alikuwa anaamini ni haki yake kutendea watu alivyowatendea? Alichokuwa anakitafuta ni kipi hasa? Aliwahi kufikiria kwamba kila tendo lake baya lingemrudia? Ni ni kama kweli tuhuma dhidi yake ni za kweli.

Hata sasa, je, anachukuliaje mashitaka dhidi yake? Anahisi anaonewa? Anachukulia kesi dhidi yake ni ya kisiasa? Anajua mahali alipo? Au kuna mtu alikuwa anamtuma, anampa kiburi, sasa hivi hayupo? Kuna ulazima mkubwa wa kumpima afya ya akili. Itasaidia pakubwa.

Mtazamo wangu katika tuhuma za Sabaya upo hapa, ama anasingiziwa, na kama hasingiziwi, basi kichwani sio mzima. Ni psychopath.

Credit: Luqman Maloto
 
Analysis nzuri,kama mawazo yako yakafanyiwa kazi tutakiwa tutazame tasis zetu za kiuchunguzi kuanzia DSO HAI ilikuaje Sabaya akawa na uhuru wa kufanya yote haya wakati tuna security intelligent officers waliokua wajumbe wa kamati ya ulinzi aliyokua anaiongoza?

Hapa tuna shida kubwa mifumo yetu ya kiusalama ipo kwa ajili kulinda viongozi na sio taifa na watu wake,wapo tayari kutii lolote hata kama ni ujinga na uhalifu?

Tuna option moja katiba itakayo either kufuta mavyeo haya yasiyo na sifa maalum au wasiwe wenyeviti wa kamati ya ulinzi.

Katika hili Jiwe ndio sababu alikua anaendesha nchi kihuni huku akiweka proganda mbele na ofcourse alifanikiwa huko mbeleni tungekua taifa la ajabu,kuna majitu humu ulikua huyambii kitu kwa jiwe.

Swali jiwe alifikaje alipofika?Tuna vetting system mbovu zisizoweka taifa mbele bali maslahi binafsi na kufurahisha viongozi na so far tunaweza tusiwalaumu kwa sbb ya katiba yetu imewapa viongozi wa kisiasa madaraka ya KiMungu.

Tuna wajibu mkubwa sana kubadilisha mfumo wetu
 
Naendelea Kusisitiza kuwa mtakuja na ' Threads ' nyingi tu za Kumponda au Kumtetea ila Mimi GENTAMYCINE nisiposikia Hukumu yake kuwa ni ya Kifungo cha Maisha Jela au Kuuliwa ( Kunyongwa kabisa ambacho ndiyo nakiombea 24/7 ) sitoielewa na hata Kuiamini tena Mahakama ya Tanzania na hata Serikali ya Rais Samia.
 
Kwa hali hii basi hata aliye mteua nae alikuwa na matatizo ya afya ya akili bila shaka. Haiwezekani mtu una akili timamu, halafu umteue kichaa!

Ndege wafananao huruka pamoja.
 
Wewe Sabaya humfahamu vizuri zaidi ya kumsikia radioni na maGazetini. Ila uchawa ndani ya UVccm ndo umetufikisha hapo.
Never again!
Tubadili Katiba yetu tusije pata kiongozi mungu-mtu kama JPM. Yaani wote waliomtetea wazi wazi aliwatuuku vyeo waendelee kumtukuza!!
 
ALIYEKUWA Mkuu wa Wilaya ya Hai, Lengai Ole Sabaya, alifikishwa mahakamani jana. Ni matokeo ya tuhuma zinazomuandama kwa muda mrefu sasa.

Yameshasemwa na yanaendelea kusemwa mengi. Hisia ni tofauti kuhusu yanayomtokea Sabaya. Kila mtu anataka aseme kitu. Nami nimeshaulizwa kwa nini sisemi chochote. Ngoja basi nitoe neno. Nitachukua muktadha maalum, bila kuingilia uhuru wa mahakama.
Tuhuma za Sabaya ni nyingi, zinaogopesha. Zinashangaza kupita kiasi. Zinahitaji akili ya juu mno kuzichambua. Ukizichukua tuhuma za Sabaya na kuziweka kwenye kapu la uhalifu sawa na uhalifu mwingine, hilo ni kosa kubwa.

Tafakari, Sabaya ni binadamu. Kila binadamu ana ubinadamu, vinginevyo kuwe na shida kwenye ubinadamu wake.

Tafakari zaidi, Sabaya akateuliwa kuwa Mkuu wa Wilaya. Kazi ya kutumikia wananchi. Binadamu wenzake. Kila binadamu anafamu wito wa ubinadamu ni kuwatendea haki binadamu wenzake. Vinginevyo ubinadamu wake uwe na upungufu.

Inafahamika, kuchaguliwa au kuteuliwa kuwa kiongozi ni zawadi kubwa mno. Kuilipa hiyo zawadi si kufanya chochote isipokuwa kuwatumikia watu kwa upendo na uadilifu.

Sabaya akiwa mkuu wa wilaya, akawa anatuhumiwa kupora mali za watu, kuonea anaowaongoza. Kulazimisha mapenzi kwa wanawake na hata kubaka. Hizo tuhuma ukizisikia, kama una kichwa kizuri lazima kwa asilimia 50 utadhani anasingiziwa.

Ni kwa sababu, mtu mwenye akili timamu hawezi kufanya hata robo ya yale anayotuhumiwa nayo Sabaya.

Mtu mzima anawezaje kuteka wake za watu na kulazimisha mapenzi? Anaingiaje kwenye hoteli na kulazimisha aoneshwe chumba cha mteja mwanamke, ili iweje? Anawezaje kulazimisha wafanyabiashara wampe pesa bila kufanyia kazi? Anawezaje kuteka watu na kuwatesa? Anafyatuaje risasi hovyo? Mtu mwenye akili timamu kweli?

Kwa kiongozi, vitendo vyote hivyo kwa sehemu kubwa vinanajisi uongozi. Je, Sabaya kama mtu timamu, hakutambua uongozi ni upendeleo na ulinzi wake ni uadilifu?

Ndio maana nikasema, tuhuma za Sabaya kwa asilimia kubwa hukaribisha hisia kwamba anasingiziwa. Maana mtu mwenye akili timamu hawezi kufanya japo robo ya vitendo anavyotuhumiwa navyo Sabaya.

Sasa, hata baada ya kufikishwa mahamani, lipo eneo la kulisemea. Ni namna ya kuingia ndani zaidi kwenye tuhuma zake.

Nimeshasema, ni kosa kubwa kuziweka tuhuma za Sabaya katika kapu moja la uhalifu, sawa na uhalifu mwingine.

Kama yote ambayo Sabaya anatuhumiwa nayo ni kweli kayatenda, basi uhalifu mkubwa upo kwenye namna ubongo wake unavyofanya kazi. Inawezekana haupokei na kutafsiri mambo kama binadamu wa kawaida.

Kama ndivyo, hata sasa akiwa mahabusu, inawezekana akawa haelewi kwa nini amekamatwa, kwani yote aliyokuwa anafanya (ikiwa ni kweli), yeye anaona alikuwa sahihi. Tena, si ajabu anajiona anasingiziwa.

Watu wenye namna ya kipekee katika kupokea na kutafsiri mambo kijamii huitwa "psychopath". Ni tafsiri sawa na mgonjwa wa akili. Kwa kawaida psychopath huwa wana matatizo ya afya ya akili.

Kama kutakuwa na dhamira ya kumtendea haki Sabaya, basi itabidi kumpima afya ya akili. Maana, kama kweli alitenda yote anatuhumiwa nayo, maana yake atakuwa psychopath. Mtu timamu asingethubutu kufanya hata moja ya 10 ya anayotuhumiwa kufanya.

Binafsi ningetamani, kabla hata hajafikishwa mahakamani, wakati wa kumhoji Sabaya ili kukamilisha taarifa za mashitaka dhidi yake, kungekuwa na wataalamu wa afya ya akili katika mahojiano.

Hapa sipendekezi Sabaya apewe msamaha kama tuhuma dhidi yake zina ukweli, la, haki itendeke. Wahalifu wenye matatizo katika afya ya akili hufungwa, ila kuna namna ya kuwasaidia kipindi wanatumikia adhabu zao.

Kinachonishawishi kuona ulazima wa Sabaya kupimwa afya ya akili ni kwa sababu nataka kujua ubongo wake ulikuwa unawaza nini alipokuwa akitenda uhalifu alioutenda. Hii ni kama kweli alitenda.

Je, ubongo wake ulikuwa unawaza nini? Kwamba yeye ni mkubwa sana kwa hiyo angetenda chochote kwa watu bila lolote kumrudia? Alikuwa anaamini ni haki yake kutendea watu alivyowatendea? Alichokuwa anakitafuta ni kipi hasa? Aliwahi kufikiria kwamba kila tendo lake baya lingemrudia? Ni ni kama kweli tuhuma dhidi yake ni za kweli.

Hata sasa, je, anachukuliaje mashitaka dhidi yake? Anahisi anaonewa? Anachukulia kesi dhidi yake ni ya kisiasa? Anajua mahali alipo? Au kuna mtu alikuwa anamtuma, anampa kiburi, sasa hivi hayupo? Kuna ulazima mkubwa wa kumpima afya ya akili. Itasaidia pakubwa.

Mtazamo wangu katika tuhuma za Sabaya upo hapa, ama anasingiziwa, na kama hasingiziwi, basi kichwani sio mzima. Ni psychopath.

©Luqman Maloto
Naunga mkono hoja, kama tuhuma zote zinazomuhusu Sabaya tunazosoma kwenye gazeti la Raia Mwema na mitandao ya kijamii, ni za kweli, then Sabaya ni Psychopath, ni insane, alikuwa hajui atendalo, anahitaji kusaidiwa. Hatua ya kwanza ni kupata wakili mzuri, atakayecheza na defence ya insanity.

Kuna uwezekano Ole Sabaya ni Insane, hivyo anahitaji kusaidiwa kama nilivyo shauri hapa,

Na hiyo insanity inawezekana umetokana na hoja za bandiko hili.

P
 
Naunga mkono hoja, kama tuhuma zote zinazomuhusu Sabaya tunazosoma kwenye gazeti la Raia Mwema na mitandao ya kijamii, ni za kweli, then Sabaya ni Psychopath, ni insane, alikuwa hajui atendalo, anahitaji kusaidiwa. Hatua ya kwanza ni kupata wakili mzuri, atakayecheza na defence ya insanity.

Kuna uwezekano Ole Sabaya ni Insane, hivyo anahitaji kusaidiwa kama nilivyo shauri hapa,

Na hiyo insanity inawezekana umetokana na hoja za bandiko hili.

P
Shida ni hatuna vetting ya uongozi rekodi ya sabaya ni mbaya tokea alipochoma shule na wahuni wenzake wakati anasoma.
Sasa ukishachoma shule utasomea wapi sasa.
 
Kwa hali hii basi hata aliye mteua nae alikuwa na matatizo ya afya ya akili bila shaka. Haiwezekani mtu una akili timamu, halafu umteue kichaa!

Ndege wafananao huruka pamoja.
Inategemea unataka kichaa akufanyie nn,kumsabaratisha mbowe ilitakiwa kichaa,maana upinzani kwake ilikuwa ni kikwazo cha kubadili katiba atawale milele.Sema tu Mungu aliona tuendako si salama akaamua kumpangia majukumu mengine
 
Back
Top Bottom