Mhe. Lema: watanzania 'hawaombi' bali 'wanataka' katiba mpya!

Mhe. Lema: watanzania 'hawaombi' bali 'wanataka' katiba mpya!

hizi za lema ndio porojo na fujo tunataka katiba sio maneno..tunataka katiba mpya lakini uongo wa kudai katiba kufanya fujo....kama munayo munayo pendekeza itoeni hapa tuijadili...kusema tu tunataka katiba mpya bila kusema unataka nini ndani ya hio katiba ni uenda wazimu....katiba sio msahafu au injili ambayo binaadam wameteremshiwa na allah,,,,ni sheria ya nchi inayotungwa na binaadamu so hatutaki porojo la katiba bila kusema nini tunataka...wekeni hapa nini kinatakiwa tukijadili....sio porojo

wewe unaishi Tz kweli?sababu ya kwanza ya kudai katiba mpya ni kwa sababu hii iliyopo haikushirikisha wanananchi.
Kuna mambo mengi specific mfano muundo wa muungano,NEC huru,Wabunge wa kuteuliwa,ukubwa wa cabinet,vyombo vya umma kuwajibika kwa serikali na sio chama tawala.....nikiendelea kutaja naweza kujaza server bure!
Alichokitaka lema ni kwamba serikali iwe wazi,iseme kwamba inaleta mchakato wa katiba mpya na sio kuibuka na porojo na misemo tata kama 'kuhuisha' n.k
tatizo lenu mkiambiwa ukweli mnasingizia fujo.
 
watake wasitake wasahau kilimo kwanza sasa ni KATIBA KWANZA!!!
Katiba oyeeeee

Hivi na ukame huu kuna hata KILIMO KWANZA HAMNA? CDM chama la nguvu, mnawapeleka puta sana hawa wazee wa 1950.
 
Jack mi nafikiri nibora usiongeze neno uliyosema wameshayasikia. Sasa yule Lema anasema katiba haiombwi inatakiwa tena kwa nguvu zote, nakubali. Ila anaposema hakuna cha tume wala wataalamu wa CCM kufanya swala hilo Je hao CCM siyo watanzania? Je ukiachia bunge lifanye kazi hiyo ndiyo itakuwa ya watanzania? Eti tutaandamana nchi nzima kudai katiba mpya, je itashuka toka mbinguni? Lazima kuwe na chombo kitakacho ratibu kupatikana kwa katiba mpya na si vinginevyo hata kama ni bunge lazima bunge lipitishe kanuni la kuweka bunge la katiba.

Cha muhimu ni lema na wananchi wengine kupendekeza tume au chombo husika kihusishe kina nani, katiba iwe na vitu gani (maudhui) na je elimu kwa wananchi ipelekwe kwa njia zipi hasa. Siyo ushabiki wa kichama hapa Mh. Rais alishasema na kurudia aliyosema Prof. Shivji na Ulimwengu kuwa katiba siyo ya chama fulani wala si chombo cha kutafutia umaarufu wa chama. Au mnataka rais aseme chadema wachukue jukumu la kusimamia mchakato?

Mh. Lema anatabia za mbowe kupenda kutumia mabavu huku akiacha wananchi wakibaki na majeraha mwilini na rohoni wakati yeye anatesa kwenye cheo tu ngoja tuanze kudai haki ya kugombea uenyekiti tutaandamana mpaka ang'oke kama ben ali wa tunisia. Lema ni bwana mdogo anapaswa kutulia kupanga mikakati na logical points ili hata akisimama bungeni asikike ameongea jambo la maana na siyo ili tu vijana wamuone ameongea bungeni kumbe anapiga kelele.
 
katiba ya kweli tunayoipigia makelele na ambayo itakidhi maslahi ya wengi, itakayo linda rasilimali zetu na utu wetu tulioachiwa na mwl. Nyerere itapatikana tu yakifanyika mapinduzi kuliko kuwaachia mafedhuli watuamulie aina ya katiba wanayoitaka wao.
watanzania wenzangu tuamke sasa, arusha revolution squre is nmc ground, tutaanzia hapo kwa wakazi wa arusha
 
Back
Top Bottom