Mheshimiwa Rais sidhani kama kupenda Kwako kila mara ' Kumtajataja ' hadharani TISS DG Dkt. Kipilimba ni sawa Kiuweledi

Mheshimiwa Rais sidhani kama kupenda Kwako kila mara ' Kumtajataja ' hadharani TISS DG Dkt. Kipilimba ni sawa Kiuweledi

GENTAMYCINE

JF-Expert Member
Joined
Jul 13, 2013
Posts
60,660
Reaction score
121,325
ANGALIZO

Naomba kama unajijua kabisa kuwa uwezo wako wa kuona vitu vya umbali / unyeti / umuhimu wake basi katika huu ' Uzi ' kaa nao mbali kabisa na waachie wenye ' akili ' zao na ' Wachambuzi ' wa masuala haya ya Kijasusi ambao wapo ( tunao ) wengi humu na Sisi Mangumbaru na Mapopoma wengine tuwe watazamaji tu kuliko Kuchangia halafu ukajikuta umevapa / umekosea.

HOJA KUU

Nashukuru sana Mwenyezi Mungu kwamba karibia awamu zote za nchi hii nilikuwepo japo ya Hayati Baba wa Taifa ilinikutia nikiwa bado katika Ndoo ya Kuogea na nalilia Uji wa Buruga ( namaanisha nikiwa bado Kichanga kabisa ) ila kwa awamu ya Mzee Mwinyi niliishuhudia bila kusahau ya Mzee Mkapa na ya Mzee Kikwete na sasa nipo hii ya Mheshimiwa Dkt. Magufuli natiririka na naserereka nayo.

Katika Awamu zote hizo sikuwahi hata Siku moja kuwasikia hao Watangulizi wake Rais Dkt. Magufuli wakiwa na tabia ya kupenda ' Kumtajataja ' au hata kupenda kuonyesha kwamba Mkurugenzi Mkuu wa Idara Nyeti nchini ya Usalama wa Taifa ( TISS ) yupo eneo ambalo Wao wapo ila ilikuwa ni mpaka tu labda Mtu akutonye / akuambie.

Nimejuiuliza maswali mengi sana kwani Marais wote Wastaafu walikuwa hawapendi kuwatajataja Wakuregenzi wao Usalama wa Taifa ( TISS DG ) lakini kwa Awamu hii ya Gwala / Tano Rais Dkt. Magufuli anapenda mno ' Kumtaja ' na hata kupenda ' Kumuinua ' Kitini Mkurugenzi wa sasa Dkt. Modestus Kipilimba na bado sijapata jawabu / jibu ila najua kupitia ' Majiniasi ' waliotukuka wa Jamvi hili la JamiiForums leo nitayapata.

Sikuishia tu hapo kama kawaida yangu huwa napenda kwenda ' deep ' zaidi kufanya ' references ' na Mataifa mengine mbalimbali kuanzia na haya Jirani ( tunaofanana kwa Vingi ) kisha hupenda pia kuangalia na yale Mataifa makubwa ambayo yana uwezo mkubwa wa Kuanzia Uchumi, Kijeshi na Kiusalama kuliko Tanzania yetu hii na sijaona mahala ambapo Marais wao huwa wanawataja hovyo tena hadharani Wakurugenzi Wakuu wa Idara zao ' Nyeti ' za Usalama wa Taifa ila kwa Tanzania naona hii tabia inaanza Kuzoeleka.

Kwa maoni au mtazamo wangu mdogo tu ( mnaojua zaidi mtanisaidia ) kwa asili ya hizi nchi zetu tena ambazo zina ' Majaribu ' na ' Matatizo ' mengi ya Kimsingi huku kukiwa na ' Maadui ' wengi wa ndani na nje sidhani na siafiki kabisa tena kwa 100% kwa Wakurugenzi wetu hawa wa hii Idara / Taasisi muhimu kama si nyeti ya Usalama wa Taifa ( TISS ) kutajwatajwa hovyo kwa Watu na hata kujulikana kwakuwa Tanzania ya sasa imejaa Watu wa ajabu ajabu wenye ' maslahi ' yao ' hasi ' na nchi hii hivyo kuna uwezekano na Wao wakaanza Kumjua na Kumzoea kisha hali ikaja kuwa mbaya zaidi huko mbeleni.

Na sidhani pia kama hata ' Kiuweledi ' hivi anavyofanya Mheshimiwa Rais wa Awamu ya Tano Dkt. Magufuli la kupenda ' Kumtajataja ' Mkurugenzi Mkuu wa Idara / Taasisi ya Usalama wa Taifa ( TISS DG ) Dkt. Kipilimba ni sahihi na kama itapendeza nadhani Watu wa ' Itifaki ' ambao nina uhakika kuwa wengi wenu tunatiririka na kuserereka pamoja 24/7 hapa JamiiForums hili mtaliangalia kwa hayo mapana yake ili utaratibu ule ule uliozoeleka wa zamani wa hawa Wakurugenzi kutojulikana sana au kutajwatajwa hovyo uendelee kwani Kwangu Mimi kwa ' Mazingira ' ya nchi yetu ulikuwa ni utaratibu murua / mujarab / sahihi kabisa kuliko huu wa sasa aliouanzisha Amiri Jeshi Mkuu na Rais Dkt. Magufuli.

Huu ulikuwa ni mtizamo wangu Mimi kama GENTAMYCINE ila nitashukuru na Watu wengine nao wakija hapa wakichangia huku wale ambao ' watanikosoa ' basi wanikosoe ha ' Hoja ' nzito nzito kwani hata Mimi nataka Kujifunza jambo hapa kutokana na kwamba yawezekana huu utaratibu wa sasa ukawa ndiyo sahihi kuliko ule ambalo nimeukariri / nimeuzoea. Nia na madhamuni tupate afya ya Kimjadala na ya Kimantiki juu ya hili ' Suala ' kusudi mwisho wa Siku wote tupate ' maarifa ' na ' ufahamu ' zaidi.

Karibuni!

Nawasilisha.
 
Ndefu sana...

Sijawahi Kuanzisha ' Threads ' fupi hapa JamiiForums Mkuu ( pitia threads zangu zote za mambo sensitive zilivyo ) na nashukuru zote zimekuwa zikisomwa na kupata mrejesho wake hivyo labda hili ni tatizo lako tu. Hata hivyo asante kwa kuja na kuchangia hivyo nikuombe tu kaa pembeni waachie ' Great Thinkers ' waje waweze kunipa ' Madini ' tafadhali.
 
Sasa mbona kipindi anateuliwa kuwa DG media zote za ndani na nje zilichapisha habari na kubandika picha zake sasa hao maadui unaowasema wanashindwa kwenda google na kupata picha ya huyo Kipilimba na pia siku anaapishwa tukio si ilichukukuwa live na video zipo youtube.

Kiongozi mkuu wa idara nyeti asiweze kujulikana hio kitu hakipo popote pale duniani.Mkuu wa intelijensia wa Rwanda bwana Emmanuel Karenza ,chief wa kenya bwana kameru ukitaka picha zao ,information google utazikuta kibao.

Binafsi sijaona mantiki ya hoja hii.
 
Kama kuchaguliwa kwake ikulu inatoa press release,Kuna usiri wowote tena hapo?
 
Hiyo ni defending mechanism tu.
Anajaribu kupeleka ujumbe kwamba anawatumia sana vibarua wa DGoTISS, hawalali hivyo wakosoaji wake lazima watambue unavyoiba mifugo usifikiri kama umewini ila ukumbe yupo mchungaji anaeweka kikao na wenye mifugo.

Kwa hiyo hiyo ni kujaribu kutisha kama alivyo tumia jeshi katika kufanya manunuzi ya korosho na kufungia maduka ya FOREX .

Hatua hii ikizoeleka watesi wake wataona ni kawaida tu hivo hawatahofia kusonga mbele kwani hao wameshakuwa washikaji,wachumba tu!

Njia hii ya kutaja taka wakuu wa vyombo vya ulinzi, usalama na ujasusi hadharani na bila sababu au mazingira yeyote yanayo lazimisha kufanya hivo sio nzuri na mara nyingi huwa na mwisho mbaya kwa mtajaji na mtajwa!
 
Kabla ya huyu DG mpya nakumbuka mzee alikuwa airport pale. Kipindi hicho tumbua tumbua ndio imeshika hatamu. Sasa Sijui kulikuwa na mishe gani pale nikasikia, mkurugenzi wa UWT mambo ya ndani si yuko hapa? Akamtaja jina akamwambia jamaa sogea tueleze ikoje

Jamaa akamwambia kiutaratibu hawezi kusema maana ashapeleka taarifa sehemu husika. Au Kama vipi wakazungumze nje ya kamera zile. Ikaishia hapo.

Jamaa akaja kulamba ubalozi sijui nchi gani huko hadi saivi. Toka Siku ile Mimi binafsi nilizoea Kwamba atataja tu na kuita mbele yoyote. Sio ajabu.
 
Sasa mbona kipindi anateuliwa kuwa DG media zote za ndani na nje zilichapisha habari na kubandika picha zake sasa hao maadui unaowasema wanashindwa kwenda google na kupata picha ya huyo Kipilimba na pia siku anaapishwa tukio si ilichukukuwa live na video zipo youtube.

Kiongozi mkuu wa idara nyeti asiweze kujulikana hio kitu hakipo popote pale duniani.Mkuu wa intelijensia wa Rwanda bwana Emmanuel Karenza ,chief wa kenya bwana kameru ukitaka picha zao ,information google utazikuta kibao.

Binafsi sijaona mantiki ya hoja hii.

Kwani nimetaka ' ufafanuzi ' wa Kimantiki au ' mabishano ' nawe? Hopeless!
 
Hiyo ni defending mechanism tu.
Anajaribu kupeleka ujumbe kwamba anawatumia sana vibarua wa DGoTISS, hawalali hivyo wakosoaji wake lazima watambue unavyoiba mifugo usifikiri kama umewini ila ukumbe yupo mchungaji anaeweka kikao na wenye mifugo.

Kwa hiyo hiyo ni kujaribu kutisha kama alivyo tumia jeshi katika kufanya manunuzi ya korosho na kufungia maduka ya FOREX .

Hatua hii ikizoeleka watesi wake wataona ni kawaida tu hivo hawatahofia kusonga mbele kwani hao wameshakuwa washikaji,wachumba tu!

Njia hii ya kutaja taka wakuu wa vyombo vya ulinzi, usalama na ujasusi hadharani na bila sababu au mazingira yeyote yanayo lazimisha kufanya hivo sio nzuri na mara nyingi huwa na mwisho mbaya kwa mtajaji na mtajwa!

Kila Siku huwa napenda sana Kukutana na Watu makini, werevu na wenye maono ya mbali na Kujenga ' Hoja ' zenye utulivu Kiakili kama Wewe kuliko ' Mipumbavu / Mipopoma ' inasema huwa hapa hawaoni ' Hoja ' halafu hapo hapo na Wao wamechangia vile vile. Nimekukubali Mkuu kwani una ' Jicho ' la mbali hasa katika hili ' suala ' ambalo ukiwa na ' upeo ' mfupi unaweza ukadhani linastahili lakini kumbe linakosewa mno tu.

Cc: ipo siku utakufa
 
Mkuu Gentamycine uko sahihi, na umeweka wazi kama hivi wasiwasi wako kama hivi" " Tanzania ya sasa imejaa Watu wa ajabu ajabu wenye maslahi ' yao ' hasi ' na nchi hii" nadhani ajuzwe tu

Nashukuru kwa Kunielewa Mkuu na huo ndiyo wasiwasi wangu mkubwa sana japo sina mashaka kabisa na ' Uimara ' wa Taasisi hiyo Nyeti nchini ila nadhani pia si vizuri sana ' Kujiamini ' kupita Kiasi kwakuwa tu Wewe ni ' Intelligence Giant ' kwa Ukanda huu wa Afrika Mashariki na Maziwa Makuu au hata kwa Afrika nzima au Ulimwenguni. Bado naukataa na nitaendelea Kuukataa huu ' utaratibu ' wa Mheshimiwa Rais Dkt. Magufuli ' Kumtajataja ' na ' Kumuinuainua ' hovyo Mkurugenzi wa Idara / Taasisi ya Usalama wa Taifa nchini ( TISS DG ) Dkt. Kipilimba. Hili liangaliwe ' Kiitifaki ' zaidi kwa maslahi mapana.
 
Awamu za nyuma za Analogy mambo haya yalikuwa magumu leo ni digital amtaje asimtaje watu watajua tu tangu akiwa Nida lkn pia huyo ni DG tiss si mtu anayehitajika kuwa covered ila siku akiwapanga watumishiwa tiss na kuwaarika kwa chakula ikulu kama alivyofanya na trafiki hapo ndio itakuwa issue mbaya maana wanatakiwa kuwa covered ili wafanye kazi japo wengine kama wale special group linalovaa suti mbele ya kamera. Lakini wauza magazeti na mchicha ;bodaboda manesi engineers nk walio kitengo hao hatakaa awataje si tu kuwataja wengine hatakaa awajue lkn huyo DG aweza hata kuhamia hata Sumatra asilete madhara hata kuwa opposition leader sema akikiuka masharti tu anaingia saverhouse
 
Hili suala si la kawaida katika uwanja wa ujasusi ni awamu ya tano ndio tumeanza kuona mambo kama haya.Yamkini tunaweza kufikiri hili ni jambo jipya lakini si TISS pekee yake hata vyombo vingine vya ulinzi na usalama.
Mfano nimekuwa nikishangaa Mkuu wa JWTZ au IGP kuambatana na Mkuu wa nchi katika ziara za kisiasa hili nalo si jambo la kawaida.Mfano mwingine wakufunzi wa kozi ya ofisa wa jeshi Monduli miaka yote wamekuwa wakimaliza kozi yao chuoni Monduli lakini katika awamu hii tumeshuhudia wakimaliza gwaride lao uwanja wa mpira Sheck Amri Abeid na wakati mwingine viwanja vya Ikulu.
 
Back
Top Bottom