Ndugu zangu mpende msipende, hawa wakopeshaji sijui BRAC, PRIDE, FINCA nk vimekuwa kama vituo vya kudhalilisha wanawake. Utawakuta mama zetu wanavyonyanyasika kwa kila hali ikiwemo kuombwa ngono na watoa mikopo. Yote hiyo ni kutokana na umaskini. Umaskini kitu kibaya sana.
Si Mhindi wa BRAC tu mwenye rumande binafsi, barabara ya Nyerere kuna Mhindi ana magodown mengi lakini wanawake wanaoingia humo kufanya kibarua cha kupembua choroko, kunde, mpunga nk, wanafungiwa kama mahabusu. Mambo ya ajabu kwelikweli kwenye nchi huru. Tembelea viwanda vya eneo la Chang'ombe jijini Dar, hutaamini kama hayo utakayoyaona yanatokea Tanzania. Wananyanyasika kwelikweli