Mi nilishindwa sijui nyie.

uporoto01

JF-Expert Member
Joined
May 23, 2008
Posts
4,698
Reaction score
1,423
Kuna dada tuliachana vibaya miaka mingi iliopita na muda huo akataka eti tuendelee kuwa marafiki mimi nikampotezea.Sasa kuna siku moja moja tunagongana mitaani na hunilaumu sana eti kwanini simpigii simu au hata sms na siku mojamoja tuweze kupata hata chakula cha mchana.Hivi kuna urafiki baada ya mapenzi kufa ?
 
Kwakuzingatia mlivyoachana nakushauri uachane na huyo fool. Anataka akuweke spare tire siku moja yakivurugika huko aliko akutumie. achana nae she a fool. Mngekuwa mmeachana kwa amani eg ulienda kusoma nje ya nchi au mkoa mwengine sawa lakini ugomvi na nyodo - that chapter is done bro. achana nae
 
Bado anataka kumegwa huyo. Sasa wewe usilete ajizi! Mmege...kama hutaki muunganishie mshikaji.
 
Bado anataka kumegwa huyo. Sasa wewe usilete ajizi! Mmege...kama hutaki muunganishie mshikaji.

Hhahahahahahahah.....Hivi hayo mambo ya kupigiana pass bado yanaendelea??

Nilidhani vijana wa dot com hawafanyi kama sisi wa 1947!! Enzi zile tulikuwa tunawatumia wajanja vizuri hata kuanzisha michakato ingawa wengine walikuwa na tabia mbaya ya kufanya majaribio kabla ya kurusha pande kwa mlengwa!!
 
Kama mliachana vibaya nakushauri uendelee kumpotezea, huezi jua ana lengo gani!..
 
Hamna ubaya wowote kua marafiki baada ya penzi kufa...unless marafiki zako wote una mapenzi nao!!!
tuliachana vibaya sitaki hata kumfahamu tena.Nawapenda rafiki zangu lakini sijawahi kuwa na rafiki ambaye ni ex wangu.

umenielewa asante.

Bado anataka kumegwa huyo. Sasa wewe usilete ajizi! Mmege...kama hutaki muunganishie mshikaji.
hili la kumega tu hapana,sitamuunganisha na mtu nafahamu tabia zake,ni mrembo wa haja atapata hukohuko.
 
Kwa mimi naona kama urafiki unawezekana but inabidi ufuate moyo wako, kama hautaki basi. Mimi naweza sana, Ex wangu ni rafiki yangu wa kawaida sana just like someone i know
 


I can not imagine urafiki wa kawaida na mtu ambae tayari mshafanya mambo kadhaa....

Ila ipo ile ya kushirikiana once in a while, nayo sio ya mazoea na kufuatiliana...
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…