Miaka michache iliyopita baadhi ya wanajeshi wakiungwa mkono na wakazi wa kisiwa kimojawapo cha vinavyounda nchi ya Komoro waliasi na kutaka kujitenga kwa kutumia nguvu ya wanajeshi walioasi.
Tanzania ilipata umaarufu baada ya kuombwa na kufanikiwa kuyasaidia majeshi ya serikali ya Komoro kuzima maasi hayo, huku kiongozi wao akijaribu kutoroka nchini humo. Inasemekana alitumia mbinu ya kubadili mwonekano wa kijinsia kwa kuvaa baibui (buibui) - vazi linalotumiwa sana na wanawake katika jamii mbalimbali za Arabuni, Mashariki ya Kati, na pwani ya Afrika Mashariki.
Hata hivyo mbinu hii haikumsaidia maana alikamatwa na hadi hivi sasa wengine hatujui hatma yake ilikuwaje.
Rejea miaka 50 iliyopita (1964) nchini Tanzania. Baadhi ya vikosi vya jeshi nchini wakati huo likiitwa "Tanganyika Rifles" viliasi kwa madhumuni ya kushinikiza kuboreshewa maslahi (sina hakika kama kusudio lilikuwa ni kuipindua serikali ya Bwana Nyerere au la, wakati huo ikiwa madarakani).
Vikosi hivi vilizua tafrani kubwa haswa mjini Dar es Salaam naTabora ambapo kambi za vikosi vyenye dhamana ya bohari za silaha vilikuwepo.
Kwa mujibu wa mashuhuda na simulizi tulizokujapata baadaye, inasemekana katika tafrani hiyo, mashaka makubwa yaliwakumba viongozi wa serikali akiwemo Bwana Nyerere na watu wake wa karibu. Suala moja muhimu likawa ni namna ya kumwepusha yeye binafsi na madhara yoyote, haswa endapo wale askari waasi wangeelekeza hasira zao dhidi yake kama Amiri Jeshi Mkuu.
Inasemekana tena, kwamba kuna mtu mmoja (Kambona?) aliyewasaidia kuwaweka salama aliyetoa wazo kwamba njia nzuri ya kuwaokoa ni kuwavisha Nyerere, Kawawa, na wengine vazi la baibui (buibui) na kuwatorosha kwa siri toka sehemu waliokuwepo na kuwapeleka mafichoni (kuwapakiza kwenye mtumbwi na kuwavusha kwenda Kigamboni?).
Kama ni kweli anastahili pongezi kwa ubunifu huo uliowasalimisha viongozi!
Baada ya hapo mambo yalipokuja kutulia Nyerere akalifumua jeshi na kuliunda upya na ndipo lilipoundwa jeshi la"Wananchi" ili kuendana na dhana ya kwamba uhuru uliopatikana miaka michache kabla ya tukio hili, ulikuwa uhuru wenye lengo la kupigania maslahi yaWatanzania wote na sio kundi moja lililokabidhiwa silaha za kivita.
Lakini kwa kweli kama mwalimu alivishwa"buibui" najaribu kutafakari hasira aliyokuwa nayo kutokana na kudhalilishwa kiasi hicho.
Ukiachia mbali kuvishwa buibui akina Nyerere, ni suala lenye ukweli kihistoria kuwa maasi yaliwahi tokea nchini
mwetu, na yale waliyofanya waliomnusuru kutokana na dhahama hiyo yanastahilikurejewa na kuwekewa kumbukumbu stahili.
Aliyoyafanya Nyerere baada ya hayo hayakuwa rahisi na yalihitaji ustadi mkubwa na tafakari ya hali ya juu.
Wapo kina marehemu Kambona na wengine waliochangia kutuliza mambo na hata kwa kuwashawishi
Maaskari kuacha fujo wakati ule na walifanikiwa.
Na ndipo Nyerere katika kuliunda upya Jeshi akaweka mkakati wa kujihami yeye na serikali yake kwa utaratibu wa Jeshi kuchukua vijana wengi zaidi kutoka mikoa fulani ya kaskazini mwa nchi.
Tunapoadhimisha tukio kama hili la miaka 50ya "Jeshi la Wananchi", tusisahau mambo 2 ambayo yana umuhimu mkubwa kwa nchi hii:
1. Kwanza, usalama wa viongozi unategemeapia utulivu wa walinzi wetu
2. Ili taifa liwe salama ni muhimu kwanza kwa kiongozi mkuu kuwa salama.
Lisije likatokea tenala kuvishwa buibui viongozi wa kitaifa.
Tanzania ilipata umaarufu baada ya kuombwa na kufanikiwa kuyasaidia majeshi ya serikali ya Komoro kuzima maasi hayo, huku kiongozi wao akijaribu kutoroka nchini humo. Inasemekana alitumia mbinu ya kubadili mwonekano wa kijinsia kwa kuvaa baibui (buibui) - vazi linalotumiwa sana na wanawake katika jamii mbalimbali za Arabuni, Mashariki ya Kati, na pwani ya Afrika Mashariki.
Hata hivyo mbinu hii haikumsaidia maana alikamatwa na hadi hivi sasa wengine hatujui hatma yake ilikuwaje.
Rejea miaka 50 iliyopita (1964) nchini Tanzania. Baadhi ya vikosi vya jeshi nchini wakati huo likiitwa "Tanganyika Rifles" viliasi kwa madhumuni ya kushinikiza kuboreshewa maslahi (sina hakika kama kusudio lilikuwa ni kuipindua serikali ya Bwana Nyerere au la, wakati huo ikiwa madarakani).
Vikosi hivi vilizua tafrani kubwa haswa mjini Dar es Salaam naTabora ambapo kambi za vikosi vyenye dhamana ya bohari za silaha vilikuwepo.
Kwa mujibu wa mashuhuda na simulizi tulizokujapata baadaye, inasemekana katika tafrani hiyo, mashaka makubwa yaliwakumba viongozi wa serikali akiwemo Bwana Nyerere na watu wake wa karibu. Suala moja muhimu likawa ni namna ya kumwepusha yeye binafsi na madhara yoyote, haswa endapo wale askari waasi wangeelekeza hasira zao dhidi yake kama Amiri Jeshi Mkuu.
Inasemekana tena, kwamba kuna mtu mmoja (Kambona?) aliyewasaidia kuwaweka salama aliyetoa wazo kwamba njia nzuri ya kuwaokoa ni kuwavisha Nyerere, Kawawa, na wengine vazi la baibui (buibui) na kuwatorosha kwa siri toka sehemu waliokuwepo na kuwapeleka mafichoni (kuwapakiza kwenye mtumbwi na kuwavusha kwenda Kigamboni?).
Kama ni kweli anastahili pongezi kwa ubunifu huo uliowasalimisha viongozi!
Baada ya hapo mambo yalipokuja kutulia Nyerere akalifumua jeshi na kuliunda upya na ndipo lilipoundwa jeshi la"Wananchi" ili kuendana na dhana ya kwamba uhuru uliopatikana miaka michache kabla ya tukio hili, ulikuwa uhuru wenye lengo la kupigania maslahi yaWatanzania wote na sio kundi moja lililokabidhiwa silaha za kivita.
Lakini kwa kweli kama mwalimu alivishwa"buibui" najaribu kutafakari hasira aliyokuwa nayo kutokana na kudhalilishwa kiasi hicho.
Ukiachia mbali kuvishwa buibui akina Nyerere, ni suala lenye ukweli kihistoria kuwa maasi yaliwahi tokea nchini
mwetu, na yale waliyofanya waliomnusuru kutokana na dhahama hiyo yanastahilikurejewa na kuwekewa kumbukumbu stahili.
Aliyoyafanya Nyerere baada ya hayo hayakuwa rahisi na yalihitaji ustadi mkubwa na tafakari ya hali ya juu.
Wapo kina marehemu Kambona na wengine waliochangia kutuliza mambo na hata kwa kuwashawishi
Maaskari kuacha fujo wakati ule na walifanikiwa.
Na ndipo Nyerere katika kuliunda upya Jeshi akaweka mkakati wa kujihami yeye na serikali yake kwa utaratibu wa Jeshi kuchukua vijana wengi zaidi kutoka mikoa fulani ya kaskazini mwa nchi.
Tunapoadhimisha tukio kama hili la miaka 50ya "Jeshi la Wananchi", tusisahau mambo 2 ambayo yana umuhimu mkubwa kwa nchi hii:
1. Kwanza, usalama wa viongozi unategemeapia utulivu wa walinzi wetu
2. Ili taifa liwe salama ni muhimu kwanza kwa kiongozi mkuu kuwa salama.
Lisije likatokea tenala kuvishwa buibui viongozi wa kitaifa.