Miaka 60 ya uhuru wa Tanganyika 1961: Historia ya wapigania uhuru haifahamiki

Miaka 60 ya uhuru wa Tanganyika 1961: Historia ya wapigania uhuru haifahamiki

Babu...
Niandikie kistaarabu mimi mzee nakimbilia miaka 70 si adabu kuniita, 'We,'' na kuniambia "nawashwa," hilo ni tusi kubwa.

Kunitukana mimi ni sawa na kumtukana baba au mama yako.

Kama kuwashwa basi nimewashwa kwa miaka mingi sana maana nimeandika vitabu 10 na makala wala sijui hesabu yake.

Search hapa JF utazikuta.
Sasa hivyo vitisho vya nini?

Nani nchi hii umesikia kaadhibiwa kwa kuandika historia?

Mbona haya ninayoandika hapa yamo kwenye maandishi yangu mengi sasa zaidi ya miaka 40?
Mzee nakuita tena ,kama nimekosea nisamehe.
Tukirudi kwenye topic usichanganye siasa na history na udini.
Hapo unaharibu.
Ni mwandishi ambao vijana tunajivunia sana maana nimesoma maandiko yako yote.
Mi ni mwandishi pia na msomaji mzuri tu miaka yote.
Kukosoana kumo.
Usikasirike
Nimekusoma mada nyingi sana
 
Hili swala la udini linatoka wapi?. Maswali muhimu ya kujiuliza.
Uhuru ulipiganiwa na wakristo pekee?. Ili wakristo peke yao wawe huru
Uhuru ulipiganiwa na waislamu ili waislamu wawe huru pekee wenyewe na wengine wawe bado chini ya mkoloni?.
Swali hilihili kwa dini nyingine nazo?..
Mleta uzi kwani ame-aknowledge kwamba hawa ndio waislam walioshiriki kupigania uhuru??.. Kama Jibu ni hapana basi haipaswi kubezana kwa mitazamo na fikra za uelewa(Perception and understanding).
Kama kuna mtu ataliona hili kwa angle ya udini, Basi kuna mwingine atakuja kwa angle ya ukabila. Mzanaki atamwambia Muha nilikuletea uhuru, vivyohivyo na makabila mengine.
 
Kusahihisha historia ya Tanganyika sio kuangalia upande mmoja wa shilingi. Kwani hili taifa ni waislamu pekee ndio walipigania uhuru wa Tanganyika? Mbona unataka kuaminisha umma kuwa ni akina Sykes na waislamu ndio walikuwa na mchango mkubwa kudai uhuru.
Idu...
Sijaangalia upande mmoja wa shilingi.

Wapo Wakristo waliokuwa kwenye harakati na nimewaona katika utafiti wangu na nimewataja kwenye kitabu cha Abdul Sykes.

Niliamua kuandika kitabu baada ya kuona waasisi wenyewe wa African Association hadi kufikia TANU hawamo kwenye historia ya uhuru wa Tanganyika.

Historia ya uhuru kama ilivyoandikwa na Chuo Cha CCM Kivukoni inaanza na Mwalimu Nyerere 1954.

Ukisoma Nyaraka za Sykes unakuta kuwa Kleist Sykes alikuwa katibu muasisi wa African Association 1929 na mwanae akashika nafasi ya baba yake kama katibu wa TAA 1950.

Kitabu cha Kivukoni kikawa kimefuta historia ya takriban miaka 50.

Nilichokifanya mimi ni kuandika historia hii tena nikitumia nyaraka za waasisi wenyewe na nikaenda mbele zaidi na kuandika historia ya wale waliopigania uhuru na Nyerere na wengi waliomzunguka Nyerere walikuwa Waislam.

Mchango wa Waislam katika kupigania uhuru wa Tanganyika hauna mfanowe na hii ndiyo sababu kitabu nikakiita: "The Life and Times of Abdulwahid Sykes (1924 - 1968) The Untold Story of the Muslim Struggle Against British Colonialism in Tanganyika."

Kweli hii ni "untold story," yaani haikupata kuelezwa kabla?
Kweli kilikuwa na "Muslim Struggle?''

Mabingwa wa historia ya Tanganyika John Iliffe, James Brennan na Jonathon Glassman wameandika pitio la kitabu hiki na yote yamechapwa katika Cambridge Journal of African History.

Hakuna aliyepinga mchango wa Sykes baba na wanae katika uhuru wa Tanganyika wala mchango wa Waislam.
 
Mzee nakuita tena ,kama nimekosea nisamehe.
Tukirudi kwenye topic usichanganye siasa na history na udini.
Hapo unaharibu.
Ni mwandishi ambao vijana tunajivunia sana maana nimesoma maandiko yako yote.
Mi ni mwandishi pia na msomaji mzuri tu miaka yote.
Kukosoana kumo.
Usikasirike
Nimekusoma mada nyingi sana
Babu...
Nimefurahi kuwa umekanyika na hukuniita, "We."

Ahsante sana.

Ikiwa wewe unaona kuandika mchango wa Waislam katika historia ya uhuru wa Tanganyika ni udini mimi sina la kufanya kubadili fikra zako.

Lazima niheshimu msimao wako na tuendelee na mjadala.

Lakini nami napenda kukuuliza swali.

Wewe umeridhia kwa Kivukoni kufuta historia ya kweli ya uhuru?

Haikukushangaza kuwa wenye kadi no. 2 na 3 ya TANU na kati ya wafadhili wa harakati na waliompokea Mwalimu katika siasa hapa Dar es Salaam wamefutwa kwenye historia na majina yao hayamo kwenye kitabu cha Kivukoni?

1639920666812.png
 
Hakuna PDF za vitabu vyako babu
Remmy...
Ikiwa unapendezwa kwa kunitambulisha kwa makamo yangu usiniite babu niite baba.
Wewe kwa umri wako unaweza kuwa mwanangu.

Sasa wanao ndiyo umri wa wajukuu zangu maana mkubwa hajavuka miaka saba.
Vitabu vyangu haviko kwenye pdf.
 
Remmy...
Ikiwa unapendezwa kwa kunitambulisha kwa makamo yangu usiniite babu niite baba.

Wewe kwa umri wako unaweza kuwa mwanangu.

Sasa wanao ndiyo umri wa wajukuu zangu maana mkubwa hajavuka miaka saba.

Vitabu vyangu haviko kwenye pdf.
Sawa baba shukran
 
Kwani tupoambiwa tufundishwe historia ya kweli ya taifa letu na somonliangaliwe upya tulikuwa tunaelewa nn?
 
Remmy...
Ikiwa unapendezwa kwa kunitambulisha kwa makamo yangu usiniite babu niite baba.

Wewe kwa umri wako unaweza kuwa mwanangu.

Sasa wanao ndiyo umri wa wajukuu zangu maana mkubwa hajavuka miaka saba.

Vitabu vyangu haviko kwenye pdf.
Ila ombi langu kwako kama inawezekana angalau uviweke kwenye pdf,
Maana hautavitoa bure bila gharama za uzalishaji,
Japo sidhani kama gharama ni lengo hama si lengo lako.
 
Kwani tupoambiwa tufundishwe historia ya kweli ya taifa letu na somonliangaliwe upya tulikuwa tunaelewa nn?
Mpi...
Nilikuwa mmoja wa waandishi wa historia mpya iliyokuwa inaandikwa.
Nilijifunza mengi.
 
Ila ombi langu kwako kama inawezekana angalau uviweke kwenye pdf,
Maana hautavitoa bure bila gharama za uzalishaji,
Japo sidhani kama gharama ni lengo hama si lengo lako.
Remmy...
Mimi ni mwandishi tu hapo ndiyo ukomo wangu.

Kuchapa kitabu, uuzwaji wake na usambazaji wake hii ni kazi ya publisher na wauzaji vitabu yaani bookshops.

Kuviweka vitabu katika pdf na kwengineko kama Amazon hiyo ni kazi ya pubisher ikiwa ataona kuna maslahi na biashara yake.

Kwa hapa nyumbani hivi vitabu vinapatikana Ibn Hazm Media Centre Msikiti wa Manyema Mtoro na Mtambani.
 
Remmy...
Mimi ni mwandishi tu hapo ndiyo ukomo wangu.

Kuchapa kitabu, uuzwaji wake na usambazaji wake hii ni kazi ya publisher na wauzaji vitabu yaani bookshops.

Kuviweka vitabu katika pdf na kwengineko kama Amazon hiyo ni kazi ya pubisher ikiwa ataona kuna maslahi na biashara yake.

Kwa hapa nyumbani hivi vitabu vinapatikana kwa Ibn Hazm Media Centre Msikiti wa Manyema Mtoro na Mtambani.
Ooooh sawa ndugu
 
Hili swala la udini linatoka wapi?. Maswali muhimu ya kujiuliza.
Uhuru ulipiganiwa na wakristo pekee?. Ili wakristo peke yao wawe huru
Uhuru ulipiganiwa na waislamu ili waislamu wawe huru pekee wenyewe na wengine wawe bado chini ya mkoloni?.
Swali hilihili kwa dini nyingine nazo?..
Mleta uzi kwani ame-aknowledge kwamba hawa ndio waislam walioshiriki kupigania uhuru??.. Kama Jibu ni hapana basi haipaswi kubezana kwa mitazamo na fikra za uelewa(Perception and understanding).
Kama kuna mtu ataliona hili kwa angle ya udini, Basi kuna mwingine atakuja kwa angle ya ukabila. Mzanaki atamwambia Muha nilikuletea uhuru, vivyohivyo na makabila mengine.
The Chosen 1,
Mimi nimetafiti historia ya TANU na uhuru wa Tanganyika na kuna mengi nimeyaona na nimetaka kujua sababu yake ni nini?

Nimejiuliza kwa nini waliokuja kuandika historia ya TANU na uhuru walifuta majina ya watu muhimu sana katika harakati zile?

Nikapata majibu.

Kwa nini Waislam walikuwa mstari wa mbele katika kupigania uhuru wa Tanganyika?
Nikapata majibu.

Kwa nini Wamanyema walikuwa mstari wa mbele katika TANU?
Nikapata majibu.

Kwa nini leo inapoandikwa historia ya kweli kuna watu wanaumia sana na wengine kufika hata kunitukana matusi?

Nini kinachowaghadhibisha?
Hawapendi kusikia neno Uislam ukinasibishwa na harakati za uhuru?

Kwa nini?
Je hii ndiyo sababu ya kuibadili historia?

Sasa hakuna Mzanaki anaeweza kusema kuwa kaleta uhuru wala hakuna mtu mmoja au kabila moja linaloweza kuja na madai haya.

Ila ipo historia ya watu na makabila ambayo yalijipembua katika harakati hizi kiasi mtafiti makini atagundua na ikiwa ataandika ataeleza.

Haya mambo si ya leo.

Ukisoma historia ya Kleist Sykes: ''Kleist Sykes The Townsman,'' (1968) anasema kuwa wenyeji wa Dar es Salaam yaani Wazaramo, Wangindo, Warufiji na makabila mengine ya pembezoni ambao walikuwa wengi hapo mjini wakiwaita Wazulu, Wamanyema, Wanubi, ''Watu wa kuja,'' na wakiwaambia wanajitia kimbelembele sana katika siasa na mambo yote ya jamii.

(Katika hawa, ''watu wa kuja,'' ni babu yangu Salum Abdallah muasisi wa TANU Tabora na muasisi wa Tanganyika Railways African Union (TRAU) 1955).

Ukienda African Asociation utawakuta akina Kleist na Mzee bin Sudi hawa Wazulu na Wamanyema, Maulidi Commitee Wazulu, Wamanyema na Wanubi wako akina Kleist, Ibrahim Hamisi na Mzee bin Sudi.

Ukienda Al Jamiatul Islamiyya fi Tanganyika utamkuta President Mzee bin Sudi na Secretary Kleist Sykes.

Kila mahali wanachukua nafasi za uongozi.

Ukienda Yanga Afrika utamkuta Hassan Machakaomo, Mzulu kizazi cha kwanza kuzaliwa Tanganyika.

Hii ikiwaudhi sana wenye mji wao wazawa ingawa na hawa, ''watu wakuja,'' wamezaliwa Dar es kizazi cha pili cha Wazulu, Wamanyema na Wanubi kutoka Mozambique, Belgian Congo na Sudan.

Nenda Tabora 1948 wanaunda TAA uongozi na uanachama umeshikwa na Wamanyema akina Abdallah na Maulidi Kivuruga.

Shida kukuta Mmanyema Mkristo na vitu kama hivi ndivyo vilivyotawala historia ya TANU na harakati za kudai uhuru.

Ukijaribu kuukwepa ukweli huu na ukaandika historia kwa msukumo wa nafsi yako na si kwa ukweli wa hali halisi balaa lake kubwa pale anapotokea mtafiti akaandika ukweli kama ulivyokuwa.

Hiki ndicho kilichoipata historia ya Kivukoni.

Ndiyo maana leo tunaisoma upya historia ya TANU na harakati za kupigania uhuru wa Tanganyika.

Ndiyo maana hii leo tunaisoma upya historia ya Baba wa Taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere.

Angalia hiyo picha hapo chini hii ni 1955/56 wakati wa kupigania uhuru wa Tanganyika.
Ukisoma historia za hawa watu ndipo utawathamini wazalendo hawa.

Wote hawa historia zao zimo katika kitabu cha Abdul Sykes.
Nikisema niweke links zote mtachoka kusoma.

Haruna Taratibu muasisi wa TANU Dodoma, Saadan Abdul Kandoro muasisi wa TANU Kanda ya Ziwa, Sheikh Mohamed Ramia muasisi wa TANU Bagamoyo na Iddi Faiz Mafungo yeye alikuwa Mweka Hazina wa Al Jamiatul Islamiyya fi Tanganyika na Mweka Hazina wa TANU na yeye ndiye aliyekuwa mkusanyaji wa fedha za safari ya Nyerere UNO 1955.

Historia yake ni ya kusisimua sana.

Lakini Sheikh Mohamed Ramia yeye kaandikwa kwa kirefu na August Nimtz, ''Islam na Politics in East Africa.''

1639922847661.png


Kulia ni Haruna Taratibu (Mmanyema), Saadan Abdu Kandoro (Mmanyema), Julius Nyerere (Mzanaki), Sheikh Mohamed Ramia (Mmanyema) na Iddi Faiz Mafungo (Mmanyema).



 
Back
Top Bottom