Miaka 60 ya Uhuru wa Tanganyika 1961: Yaliyomfika Prof. Kighoma Ali Malima hayajamkuta kiongozi yeyote katika historia ya Tanzania

Miaka 60 ya Uhuru wa Tanganyika 1961: Yaliyomfika Prof. Kighoma Ali Malima hayajamkuta kiongozi yeyote katika historia ya Tanzania

Yalimkuta yapi ?

Mwandishi Pascal Mayalla una chochote unachoweza kutujuza kuhusu huyu msomi Prof. Malima (Rip) ?
Nimesoma primary darasa moja na mtoto wake, akiwa Waziri, sekondari nikasoma darasa moja na mtoto wa Kanyama Chiume.

Baada ya kujitoa CCM, alijiunga NRA na likufa ghafla kwa heart attack akiwa UK, watu wanasema kuna mkono wa mtu!. Hata Horace Kolimba akiwa Katibu Mtendaji Mkuu wa CCM, alisema CCM imekosa dira na haina mwelekeo, alikufa ghafla!.

P
 
Mwaka wa pili sasa; tunaendelea kusubiri.
Gagnija,
Unataka kujua yaliyomkuta Prof. Malima?
Katika kitabu cha Abdul Sykes nimeweka tabaruku hiyo hapo chini:

‘’Nakitoa kitabu hiki kwa Profesa Kighoma Ali Malima (1938-1995) ambae akiwa kijana mdogo anapata miaka 19 na hali akiwa mwanafunzi hodari, alikatisha masomo yake Shule ya Sekondari Tabora ili ajiunge na TANU katika harakati za kuikomboa Tanganyika kutoka katika utumwa wa ukoloni wa Waingereza.

Alipotambua kuwa baada ya miaka mingi ya uhuru, kuna jamii moja kwa njama na hila ilikuwa imejenga himaya ya utawala wao ndani ya chama na serikali, utawala uliokuwa na chuki kwa Waislam na Uislam alijitokeza kupinga dhulma hii.

Chama tawala na serikali kikajenga uadui dhidi ya Profesa Malima kwa sababu ya msimamo wake huo.

Profesa Malima hakutikisika.

Aliendelea kudai haki kwa bidii, kwanza akiwa ndani ya chama na serikali yake na baadae akajiuzulu ili kuongoza chama cha upinzani, National Reconstruction Alliance (NRA) na akasimama kugombea uchaguzi wa rais wa nchi ili arudishe haki na usawa kwa raia wote.

Wakati Waislam wanajiandaa kumuunga mkono Profesa Malima kama vile walivyomuunga mkono Julius Nyerere wakati wa kudai uhuru, Profesa Malima akakumbwa na umauti ghafla na kwa njia za kutatanisha tarehe 5 Agosti, 1995 akiwa London (akitokea Maka alikokwenda kufanya umra), siku chache baada ya yeye kutangaza azma yake ya kugombea urais wa Tanzania katika mkutano wa hadhara mjini Tabora.

Daima nitaenzi na kukumbuka ucheshi na kipaji cha hali ya juu cha usomi cha Profesa Malima nilichoshuhudia katika mazungumzo yetu katika siku za mwisho za uhai wake; tukitafakari kuhusu hatma ya nchi yetu.

Kwa kumbukumbu ya Profesa Malima katika kuhisi kwake janga litakaloikumba nchi yetu katika siku za baadae na katika kuenzi ushujaa wake wa kuliweka wazi tatizo nyeti la Uislam na katika kulikumbusha taifa maadili yake na katika bidii yake ya kuurejesha uongozi katika mstari wa haki na usawa kwa raia wote nakitoa kitabu hiki kwake.''

Mohamed Said
Dar es Salaam

1693627004425.png

1693627512376.png

 
Lombo,
Si kama sitaki kuitwa babu.

Umri wangu ni miaka 69 na nina wajukuu wananiita babu kwa nasaba na wengine kwa makamo yangu ya uzee.

Nilichokueleza wewe ni kuwa mimi siwezi kuwa babu yako ila baba yako kwani wewe si umri wa mimi kuwa babu yako.

Nimekueleza hivyo kwa kutaka kuweka kila kitu pale panapostahili.

Kwani wewe baba yako ana umri gani?

In Shaa Allah nitakuwekea hapa yaliyomfika Prof. Malima.
nami unitag, naipenda sana kalamu yako
 
Back
Top Bottom