kalacha mateo
Senior Member
- Sep 27, 2021
- 119
- 240
Kuelekea maadhimisho ya Miaka Miwili ya uongozi wa Dkt. Samia Suluhu Hassan Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania, wananchi katika kata za Ubungo, Tandale, Manzese, Kijitonyama, Sinza Ndugumbi, Mwananyamala na Makumbusho katika Halmashauri za Manispaa ya Ubungo na Kinondoni zinazopitiwa na Mto Ng’ombe pamoja na Mto Kiboko wamemshukuru Mheshimiwa Rais Dkt Samia Suluhu Hasan kwa kazi kubwa iliyofanyika ya kuwaondolea adha ya mafuriko iliyokuwa ikawakabili kwa muda mrefu na kuwafanya wakimbizi katika nyumba zao.
Tazama mwonekano wa sasa wa Mto Ng’ombe uliosafishwa na kujengwa kwa Zege pamoja na kujenga machujio ya maji na mabwawa ya kuhifadhi maji (Detention Ponds) katika eneo la ubungo ili kudhibiti mafuriko na kubali kabisa mandhari ya maeneo yote yanayopitiwa na Mto.
Mto wenye urefu wa kilomita nane nukta saba (km 8.7) umejengwa kupitia Mradi wa DMD ulio chini ya Ofisi ya Rais Tamisemi na kusimamiwa na TARURA.
Tazama mwonekano wa sasa wa Mto Ng’ombe uliosafishwa na kujengwa kwa Zege pamoja na kujenga machujio ya maji na mabwawa ya kuhifadhi maji (Detention Ponds) katika eneo la ubungo ili kudhibiti mafuriko na kubali kabisa mandhari ya maeneo yote yanayopitiwa na Mto.
Mto wenye urefu wa kilomita nane nukta saba (km 8.7) umejengwa kupitia Mradi wa DMD ulio chini ya Ofisi ya Rais Tamisemi na kusimamiwa na TARURA.