Miaka ya 1992,kabla ya kuingia tv,simu za mkononi,bodaboda,daladala na bajaji,tuliwezaje kumaliza siku?

Miaka ya 1992,kabla ya kuingia tv,simu za mkononi,bodaboda,daladala na bajaji,tuliwezaje kumaliza siku?

Tulikuwa tunachonga sana ana kwa ana,tulicheza sana kombolela,michezo kibao.Tulisoma vitabu kwa sana.
 
Una miaka mingapi nani alokwambia mwaka 1992 sinza na ubungo hakukuwa na daladala 7bu neno daladala lilihasisiwa mwanzoni mwa miaka ya 70 katika hiyo thread yako daladala toa labda uweke hizo tv na simu tena useme tv station


Sent using Jamii Forums mobile app
 
mimi kipindi hicho nikiwa darasa la saba nilikuwa nikipenda sana kusikiliza redio hasa ya kenya iliitwa kbs nairobi. kaka yangu alikuwa na redio moja iliitwa mkulima ilinifaa sana

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Na kwa wahenga sidhani km haya yalikua ni matatizo san kulingana na aina ya maisha pamoja na population ndogo ya wakat huo.

Kweli mkuu,kwanza kipindi kile ilikuwa ni mwendo wa story za abunuasi..

Ungewaletea maswala ya smartphone wangeona unawazinguwa.
 
Yani ilikua raha tu kitaa viroja ni zaidi ya cm.
Unakuta we ben 10,alafu kuna jimama la nyumbani mtaa wa pili limekuzimikia mume akienda job unaingia shift una lelewa mpk jioni sa 9-10 hivi unatumika.
Hapo ushakura vidali vya mwenyewe na papuchi kisha umepigwa na jero la viepe jioni.
Hamna kufumaniana
 
Siku hizi watu hatuwezi kumaliza siku bila ya kutumia simu,au kuangalia TV,vinginevo tutaiona Siku ndefu na inayoboa

Hatuwezi kutembea kwa miguu hata kwa umbali mfupi tu kama Sinza madukani hadi Ubungo au Chang'ombe jijini Dodoma hadi kiplefti cha Airport mpaka daladala au Bajaji au bodaboda

Sasa swali hivi miaka hiyo ya 1992 tuliwezaje kumaliza siku sababu sasa hivi serikali ikisema izime data watu watakuwa wagonjwa kama wamemwagiwa maji,hata maeneo ya kazi MTU hawezi maliza siku bila kuangalia meseji,pia TV kila ofisi,zamani sijui ilikuwaje kumaliza siku

Kweli watu tuna tofautiana , miaka 1992 ulikua kijijini nini ?, nilidhani ungeuliza miaka 1930 huko labda , Miaka hiyo ya 1992 wenzako tulikua tuna watch Cosby Show, Different World ,Fresh Prince of Bell Air, Soul Train ,MTV the Grind , Club MTV (with DownTown Julie Brown) ,Yo rap MTV ,Top of the Pops , BET 's Video Soul (Sherry Carter) ,Rap City na vingine vingi, hapa hapa Tanzania kwa video tapes zilizo shuka toka mamtoni ,tape inakuja ni NTSC inabidi uwe na video plate Multy sys la sivyo itabidi uende uka convert .
 
Maisha yamebadilika kwa kiasi kikubwa. Ungeuliza enzi za ujamaa mambo yalikuwaje?
 
Mimi na watafiti wakubwa tushakubaliana maisha ya zamani yalikuwa matamu sana. Sasa karne ni Mwendo wa stress.
 
Technological advancement


Sent from my iPhone using JamiiForums
 
Story kwa sana vijiweni,kusimuliana habari za kina sajenti samuel doe,prince johnson,
mithun chakraboty,hema malini,bolo young,jack shroaf etc.
Kuhadithiana mambo ya kina willy gamba,pappillon,mario puzo,James chase etc.
Kumbuka hali ilikuwa ngumu kwenye upatikanaji hela,kwahiyo mambo ya mademu hayakuwa kwa sana,juu huna hela ya lodge,
tofauti na sasa,tangu jk aruhusu ajira za pikipiki,kijana anamaliza la saba na kupata ajira ya kuendesha pikipiki,
enzi hizo ilikuwa unakaa kwenye mawe kwa miaka kabla hujabahatisha hata kiajira cha kubangaiza
 
kila zama na kitabu chake, kulikuwa na mazuri yake, kuangalia sinema za wanamuziki wa Zaire, enzi hizo ilikuwa big deal sana

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom