Miaka Zaidi ya 60 Baada ya Uhuru,Tanzania Imeshindwa Kuondoa Mizizi ya Ukoloni Kwa Nchi kuwa tegemezi wa Uchumi na Mapato Kwa Jiji Moja tuu la Dar

Miaka Zaidi ya 60 Baada ya Uhuru,Tanzania Imeshindwa Kuondoa Mizizi ya Ukoloni Kwa Nchi kuwa tegemezi wa Uchumi na Mapato Kwa Jiji Moja tuu la Dar

ChoiceVariable

JF-Expert Member
Joined
May 23, 2017
Posts
66,537
Reaction score
75,687
Tumejifunza na kuishi kwenye Maisha ya Historia kwamba Wakoloni Hawakutaka Kupeleka maendeleo kwenye Miji ya maeneo mengine ya Nchi na badala yake wakijenga Jiji Moja tuu kama economic hub ya Uchumi wa kikoloni.

Kwa hapa Tanzania (Tanganyika& Zanzibar), Wakoloni wa Kijerumani na baadae Uingereza walijenga Jiji Moja tuu la Dar kama kitovu Cha uchumi wa kikoloni huku maeneo mengine ya Nchi yakiwa ni mashamba ya uzalishaji wa malighaghafi na manamba Kwa Ajili ya kustawisha uchumi wa kikoloni.

Hata baada ya uhuru wa Tanganyika na Zanzyna hatimage Tanzania, Serikali zimeshindwa kukata Mizizi huo wa Kikoloni Kwa Nchi nzima kutegemea Dar Kwa Kila kitu.

1.Asilimia 80% ya Mapato ya Kodi uanatoka Dar

2.Njia zote za Usafiri na vyombo vya usafiri ni baina ya Mikoani na Kuja Dar na sio Mkoa na Mkoa.eg hakunaga Usafiri wa ndege baina ya Miji ya Nchi isipokuwa kuja Dar halikadhalika na reli.

3.Njia kuu za Uchumi Bado ziko na zinaendelea kuwekeza Dar mfano Bandari,viwanja vya ndege, miundombinu ya usafiri , Miundombinu ya Storage , Taasisi Kuu za kifedha.

4.Huduma za Afya za Kibingwa na Bobezi zote zinapatikana Dar.Licha ya Ukubwa wa Nchi yetu na Wingi wa watu lakini Huduma Zenye hadhi ya Kitaifa mfano Hospitali Zenye kutoa tiba Bobezi zote ziko Dar ,yaani tumeshundwa kujenga hata Kwa Kanda eg MNH,JKIC,Mlonganzila,Maaraba za Tiafa,Mkemia Mkuu wa Serikali nk.

5.Bajeti Kubwa ya Matumizi ya Nchi Kutengwa Kwa Ajili ya Kuendekeza Dar.
Pamoja na Nchi kuendelea kuwa na Uchumi tegemezi Kwa Jiji Moja ila hata matumizi ya Nchi karibia 1/3 yote hutumika kuendekeza Dar eg DMDP 2,BRT Expansion pekee Zina zaidi ya Trilioni 1 Kwa Ajili ya kujenga Barabara za Dar tuu wakati Bajeti ya Tarura ya Nchi nzima haifiki hata hiyo Trilioni 1.

Kwa hali hii sishangai kuona Kuna Mikoa Hadi Leo hii hazijaunganishwa na Lami na Serikali inaona sawa tuu.

Kuendelea Kujenga Nchi ya Utegemezi Kwa Mji mmja haikuwa malengo ya Uhuru Bali ni muendelezo wa sera za Ubaguzi za Kikoloni.

Ikiwa Mikoa itaendea Kuzalisha malighafi Kwa Ajili ya Kuendeleza Dar basi kutakuwa hakuna haja ya kuwa huru.Leo hii Mwanza inaitwa Jiji la Pili Kwa Ukubwa Tanzania lakini ukienda huoni huo Ukubwa badala yake Haina tofauti na Mikoani.

Matokeo ya sera hizo za kikoloni ni kuzidi kuongezeka Kwa gap la umaskini baina ya watu wa Mjini(Dar) na Mamilioni ya watu wa Vijijini (Mkoani).👇👇

View: https://x.com/africaupdates/status/1815077148794802270?t=8V8XGCu2NeGwOkpnQBZnLQ&s=19

Ushauri
Kumekuwa na juhudi kiduchu Kwa miaka ya karibuni Kwa Serikali kujaribu kuvifikia Vijiji Ili kupunguza umaskini lakini Tija yake imezidi kuwa ndogo Kwa sababu Bado soko kuu la bidhaa na Huduma zinapatikana Dar hivyo kutoa mwanya Kwa wachuuzi na madalali kujinufaisha Kwa jasho la watu wa Mikoani.

Naishauri Serikali kwamba Ili lengo la kusogeza maendeleo Kwa watu wengi hususani wa Vijijini (Mikoani) , Serikali ijenga walau Majiji Makuu Kwa Kila Kanda ambayo yatakuwa na miundombinu na Huduma kama zinazopagikana Dar Kwa lengo la kuwa na industrial centers Mpya ambazo zitakuwa ndio masoko ya wakulima na production centres.

Kwa kufanya hivyo tutasambaza maendeleo Kwa haraka huko Vijijini na kuondoa au kupunguza utegemezi wa Uchumi na Kila kitu Kwa Dar.Nchi za Ulaya na Asia Hazina Maendeleo Wala uchumi unaotegemea Jiji Moja kama huku Kwetu Tanzania.

Kwamba Leo hii nikitaka Kupeleka mbuzi Oman eti lazima niende Dar Kwa sababu kule ndiko Kuna maabara na ndege au meli za uhakika na sio eneo jingine,Sasa uchumi wa hivi ni muendelezo wa ukoloni.

My Take
Nampongeza Marehemu Magufuli Kwa hatua za makusudi kabisa za Kujenga Dodoma,walau tunaanza kuona Jiji lingine kubwa likizaliwa na ambalo litakuwa economic hub.

Hatua hizi ziendelee Kwa Kujenga Majiji ya Kiuchumi na Biashara Kwa Kila Kanda ambayo yatawekewa miundombinu yote mikubwa ya kiuchumi na kijamii.

Vision 2050 Ilizingatie Hilo jambo Kwa kuwa ndio itakuwa centers za kusogeza maendeleo Kwa haraka Mikoani na Wilayani.

Tanzania sio Dar pekee. Pia soma Kwanini hadi leo makao makuu ya mikoa 18 bado kuunganishwa kwa barabara za lami? Je, ni umasikini, ukubwa wa nchi au ufisadi na kukosa akili?
 
Shida sio mkoloni,bali fikra zetu na matendo yetu,ni aibu kwa taifa lenye umasikini wa kutupwa...
Hakuna mahala nimesema shida ni mkoloni Bali nimeshangaa watu weusi Kushindwa kuleta maendeleo kamailivyotarajiwa baada ya uhuru badala yake wame deepen umaskini
 
Mwalimu Nyerere alisambaza viwanda sehemu mbalimbali kama Moprocco na Canvas Morogoro, kiltex na bia ,Arusha, Chuma na Mbolea Tanga, Tanbond na Super Ghee Mwanza na kadhalika.

Siku hizi viwanda vyote ni Dar,Bagamoyo na Pwani kwa ujumla sababu Dar imejaa na huko ni karibu nayo.

Kwa hali hii Dar itaendelea kuwa mlipaji Kodi mkubwa na Kamwe Dodoma haitaifikia hata mama Kila siku yupo Dar.
 
Mwalimu Nyerere alisambaza viwanda sehemu mbalimbali kama Moprocco na Canvas Morogoro, kiltex na bia ,Arusha, Chuma na Mbolea Tanga, Tanbond na Super Ghee Mwanza na kadhalika.
Siku hizi viwanda vyote ni Dar,Bagamoyo na Pwani kwa ujumla sababu Dar imejaa na huko ni karibu nayo.
Kwa hali hii Dar itaendelea kuwa mlipaji Kodi mkubwa na Kamwe Dodoma haitaifikia hata mama Kila siku yupo Dar.
Imekuwa hivyo Kwa sababu tumeshundwa Kuendeleza pale alipoishia.

Hii Nchi inaenda enda tuu haieleweki inataka nini kwenye Maendeleo yake
 
Mwalimu Nyerere alisambaza viwanda sehemu mbalimbali kama Moprocco na Canvas Morogoro, kiltex na bia ,Arusha, Chuma na Mbolea Tanga, Tanbond na Super Ghee Mwanza na kadhalika.

Siku hizi viwanda vyote ni Dar,Bagamoyo na Pwani kwa ujumla sababu Dar imejaa na huko ni karibu nayo.

Kwa hali hii Dar itaendelea kuwa mlipaji Kodi mkubwa na Kamwe Dodoma haitaifikia hata mama Kila siku yupo Dar.
Nyerere alisifu utawala wake kwa kuwa na nia ya dhati ya kuleta maendeleo nchini. Alikuwa sahihi sana. LAKINI alikiri kuwa TATIZO na KOSA KUBWA walilofanya ni kutotilia maanani suala la MANAGEMENT! Ndicho hatimaye kilichoua miradi karibia yote ya uchumi iliyoanzishwa.

Ambacho hakusema, na alipaswa kusema au kukiri ni mfumo wa CHAMA KUSHIKA HATAMU aliouanzisha na kuuimarisha ambao uliweka ukada wa CCM kama kigezo kikuu cha kupewa madaraka katika taasisi za zote za umma. Hapo ndipo utamaduni wa kujipendekeza, uchawa, upendeleo wa kindugu, kirafiki, n.k. ulipoanza. Nyerere mwenyewe aliweza kuwavumilia wezi wa fedha za umma kuliko watu waliokuwa wakikosoa sera zake au hata kutaka kuzifanyia marekebisho kuziongezea ufanisi. Siku zote alikuwa na wasiwasi mkubwa na "mabeberu na vibaraka wao". Hilo ndilo chimbuko la kuwa na viongozi wabovu wa idara za serikali, mashirika ya umma na vyama vya ushirika. Sekta ya binafsi aliififisha kabisa. Alikuwa amepania kujenga taifa la kijamaa (kikomunisti) bila kutumia nguvu, ukali/ukatili kama alivyoshauriwa na Mao na viongozi wa Soviet Union.

Hiyo legacy ya Nyerere ndiyo imekumbatiwa na viongozi wa CCM ambao hawataki mabadiliko ya msingi hadi leo. Hatuna management makini ya uchumi na hatutakuwa nayo hadi nyakati tutakapoachana na ujinga wa kutoa kipaumbele kwa makada wa chama (ambao kiasili ni machawa pro-max) katika nafasi nyeti za uongozi wa sekta za kiuchumi na kijamii na kuzingatia ubobezi wa taaluma na meritocracy katika nafasi hizo. Bila hivyo, maendeleo yatakuwa ni suala la propaganda kuaminisha watu kuwa tuko vizuri ilhali uhalisia mitaani ukiendelea kudidimia.
 
Nyerere alisifu utawala wake kwa kuwa na nia ya dhati ya kuleta maendeleo nchini. Alikuwa sahihi sana. LAKINI alikiri kuwa TATIZO na KOSA KUBWA walilofanya ni kutotilia maanani suala la MANAGEMENT! Ndicho hatimaye kilichoua miradi karibia yote ya uchumi iliyoanzishwa.

Ambacho hakusema, na alipaswa kusema au kukiri ni mfumo wa CHAMA KUSHIKA HATAMU aliouanzisha na kuuimarisha ambao uliweka ukada wa CCM kama kigezo kikuu cha kupewa madaraka katika taasisi za zote za umma. Hapo ndipo utamaduni wa kujipendekeza, uchawa, upendeleo wa kindugu, kirafiki, n.k. ulipoanza. Nyerere mwenyewe aliweza kuwavumilia wezi wa fedha za umma kuliko watu waliokuwa wakikosoa sera zake au hata kutaka kuzifanyia marekebisho kuziongezea ufanisi. Siku zote alikuwa na wasiwasi mkubwa na "mabeberu na vibaraka wao". Hilo ndilo chimbuko la kuwa na viongozi wabovu wa idara za serikali, mashirika ya umma na vyama vya ushirika. Sekta ya binafsi aliififisha kabisa. Alikuwa amepania kujenga taifa la kijamaa (kikomunisti) bila kutumia nguvu, ukali/ukatili kama alivyoshauriwa na Mao na viongozi wa Soviet Union.

Hiyo legacy ya Nyerere ndiyo imekumbatiwa na viongozi wa CCM ambao hawataki mabadiliko ya msingi hadi leo. Hatuna management makini ya uchumi na hatutakuwa nayo hadi nyakati tutakapoachana na ujinga wa kutoa kipaumbele kwa makada wa chama (ambao kiasili ni machawa pro-max) katika nafasi nyeti za uongozi wa sekta za kiuchumi na kijamii na kuzingatia ubobezi wa taaluma na meritocracy katika nafasi hizo. Bila hivyo, maendeleo yatakuwa ni suala la propaganda kuaminisha watu kuwa tuko vizuri ilhali uhalisia mitaani ukiendelea kudidimia.
Umenikumbusha usemi wa ndugunaization, kwasasa itakuwa ccmnaization ama uchawanaization, kitaalamu tunaita unyumbu wa kisiasa.

Unyumbu wa kisiasa ni tabia ya watu wanao pewa dhamana kuahirisha kufikiri kwa nafsi kwasababu ya kujipendekeza, kulitumikia kundi fulani kwa masilahi binafsi ama uoga kwa viongozi wao bila utii, (unafiki), a.k.a kujizima data neno zuri zaidi ni kuahirisha kufikiri kizalendo
 
Tumejifunza na kuishi kwenye Maisha ya Historia kwamba Wakoloni Hawakutaka Kupeleka maendeleo kwenye Miji ya maeneo mengine ya Nchi na badala yake wakijenga Jiji Moja tuu kama economic hub ya Uchumi wa kikoloni.

Kwa hapa Tanzania (Tanganyika& Zanzibar), Wakoloni wa Kijerumani na baadae Uingereza walijenga Jiji Moja tuu la Dar kama kitovu Cha uchumi wa kikoloni huku maeneo mengine ya Nchi yakiwa ni mashamba ya uzalishaji wa malighaghafi na manamba Kwa Ajili ya kustawisha uchumi wa kikoloni.

Hata baada ya uhuru wa Tanganyika na Zanzyna hatimage Tanzania, Serikali zimeshindwa kukata Mizizi huo wa Kikoloni Kwa Nchi nzima kutegemea Dar Kwa Kila kitu.

1.Asilimia 90% ya Mapato ya Kodi uanatoka Dar

2.Njia zote za Usafiri na vyombo vya usafiri ni baina ya Mikoani na Kuja Dar na sio Mkoa na Mkoa.eg hakunaga Usafiri wa ndege baina ya Miji ya Nchi isipokuwa kuja Dar halikadhalika na reli.

3.Njia kuu za Uchumi Bado ziko na zinaendelea kuwekeza Dar mfano Bandari,viwanja vya ndege, miundombinu ya usafiri , Miundombinu ya Storage , Taasisi Kuu za kifedha.

4.Huduma za Afya za Kibingwa na Bobezi zote zinapatikana Dar.Licha ya Ukubwa wa Nchi yetu na Wingi wa watu lakini Huduma Zenye hadhi ya Kitaifa mfano Hospitali Zenye kutoa tiba Bobezi zote ziko Dar ,yaani tumeshundwa kujenga hata Kwa Kanda eg MNH,JKIC,Mlonganzila,Maaraba za Tiafa,Mkemia Mkuu wa Serikali nk.

5.Bajeti Kubwa ya Matumizi ya Nchi Kutengwa Kwa Ajili ya Kuendekeza Dar.
Pamoja na Nchi kuendelea kuwa na Uchumi tegemezi Kwa Jiji Moja ila hata matumizi ya Nchi karibia 1/3 yote hutumika kuendekeza Dar eg DMDP 2,BRT Expansion pekee Zina zaidi ya Trilioni 1 Kwa Ajili ya kujenga Barabara za Dar tuu wakati Bajeti ya Tarura ya Nchi nzima haifiki hata hiyo Trilioni 1.

Kwa hali hii sishangai kuona Kuna Mikoa Hadi Leo hii hazijaunganishwa na Lami na Serikali inaona sawa tuu.

Kuendelea Kujenga Nchi ya Utegemezi Kwa Mji mmja haikuwa malengo ya Uhuru Bali ni muendelezo wa sera za Ubaguzi za Kikoloni.

Ikiwa Mikoa itaendea Kuzalisha malighafi Kwa Ajili ya Kuendeleza Dar basi kutakuwa hakuna haja ya kuwa huru.Leo hii Mwanza inaitwa Jiji la Pili Kwa Ukubwa Tanzania lakini ukienda huoni huo Ukubwa badala yake Haina tofauti na Mikoani.

Matokeo ya sera hizo za kikoloni ni kuzidi kuongezeka Kwa gap la umaskini baina ya watu wa Mjini(Dar) na Mamilioni ya watu wa Vijijini (Mkoani).

Ushauri
Kumekuwa na juhudi kiduchu Kwa miaka ya karibuni Kwa Serikali kujaribu kuvifikia Vijiji Ili kupunguza umaskini lakini Tija yake imezidi kuwa ndogo Kwa sababu Bado soko kuu la bidhaa na Huduma zinapatikana Dar hivyo kutoa mwanya Kwa wachuuzi na madalali kujinufaisha Kwa jasho la watu wa Mikoani.

Naishauri Serikali kwamba Ili lengo la kusogeza maendeleo Kwa watu wengi hususani wa Vijijini (Mikoani) , Serikali ijenga walau Majiji Makuu Kwa Kila Kanda ambayo yatakuwa na miundombinu na Huduma kama zinazopagikana Dar Kwa lengo la kuwa na industrial centers Mpya ambazo zitakuwa ndio masoko ya wakulima na production centres.

Kwa kufanya hivyo tutasambaza maendeleo Kwa haraka huko Vijijini na kuondoa au kupunguza utegemezi wa Uchumi na Kila kitu Kwa Dar.Nchi za Ulaya na Asia Hazina Maendeleo Wala uchumi unaotegemea Jiji Moja kama huku Kwetu Tanzania.

Kwamba Leo hii nikitaka Kupeleka mbuzi Oman eti lazima niende Dar Kwa sababu kule ndiko Kuna maabara na ndege au meli za uhakika na sio eneo jingine,Sasa uchumi wa hivi ni muendelezo wa ukoloni.

My Take
Nampongeza Marehemu Magufuli Kwa hatua za makusudi kabisa za Kujenga Dodoma,walau tunaanza kuona Jiji lingine likizaliwa.

Hatua hizi ziendelee Kwa Kujenga Majiji ya Kiuchumi na Biashara Kwa Kila Kanda ambayo yatawekewa miundombinu yote mikubwa ya kiuchumi na kijamii.

Tanzania sio Dar pekee. Pia soma Kwanini hadi leo makao makuu ya mikoa 18 bado kuunganishwa kwa barabara za lami? Je, ni umasikini, ukubwa wa nchi au ufisadi na kukosa akili?
Muda mwingine huwa unashangaza sana kwa kukosa kwako misimamo kuna lipi kwako ambalo magufuli alifanya zuri mpaka ajizime data kusema unampongeza ukicheki nyuzi zote hakuna zuri lilofanywa awamu ya tano!
 
Muda mwingine huwa unashangaza sana kwa kukosa kwako misimamo kuna lipi kwako ambalo magufuli alifanya zuri mpaka ajizime data kusema unampongeza ukicheki nyuzi zote hakuna zuri lilofanywa awamu ya tano!
La kuhamia Dodoma na kusimamia anachokiamini hata kama ni Cha hovyo eg Sgr
 
Nyerere alisifu utawala wake kwa kuwa na nia ya dhati ya kuleta maendeleo nchini. Alikuwa sahihi sana. LAKINI alikiri kuwa TATIZO na KOSA KUBWA walilofanya ni kutotilia maanani suala la MANAGEMENT! Ndicho hatimaye kilichoua miradi karibia yote ya uchumi iliyoanzishwa.

Ambacho hakusema, na alipaswa kusema au kukiri ni mfumo wa CHAMA KUSHIKA HATAMU aliouanzisha na kuuimarisha ambao uliweka ukada wa CCM kama kigezo kikuu cha kupewa madaraka katika taasisi za zote za umma. Hapo ndipo utamaduni wa kujipendekeza, uchawa, upendeleo wa kindugu, kirafiki, n.k. ulipoanza. Nyerere mwenyewe aliweza kuwavumilia wezi wa fedha za umma kuliko watu waliokuwa wakikosoa sera zake au hata kutaka kuzifanyia marekebisho kuziongezea ufanisi. Siku zote alikuwa na wasiwasi mkubwa na "mabeberu na vibaraka wao". Hilo ndilo chimbuko la kuwa na viongozi wabovu wa idara za serikali, mashirika ya umma na vyama vya ushirika. Sekta ya binafsi aliififisha kabisa. Alikuwa amepania kujenga taifa la kijamaa (kikomunisti) bila kutumia nguvu, ukali/ukatili kama alivyoshauriwa na Mao na viongozi wa Soviet Union.

Hiyo legacy ya Nyerere ndiyo imekumbatiwa na viongozi wa CCM ambao hawataki mabadiliko ya msingi hadi leo. Hatuna management makini ya uchumi na hatutakuwa nayo hadi nyakati tutakapoachana na ujinga wa kutoa kipaumbele kwa makada wa chama (ambao kiasili ni machawa pro-max) katika nafasi nyeti za uongozi wa sekta za kiuchumi na kijamii na kuzingatia ubobezi wa taaluma na meritocracy katika nafasi hizo. Bila hivyo, maendeleo yatakuwa ni suala la propaganda kuaminisha watu kuwa tuko vizuri ilhali uhalisia mitaani ukiendelea kudidimia.
Wengine wameonesha Uongozi upi Hadi Sasa ikiwa tutaendelea kulaumu Nyerere?
 
Mwalimu Nyerere alisambaza viwanda sehemu mbalimbali kama Moprocco na Canvas Morogoro, kiltex na bia ,Arusha, Chuma na Mbolea Tanga, Tanbond na Super Ghee Mwanza na kadhalika.

Siku hizi viwanda vyote ni Dar,Bagamoyo na Pwani kwa ujumla sababu Dar imejaa na huko ni karibu nayo.

Kwa hali hii Dar itaendelea kuwa mlipaji Kodi mkubwa na Kamwe Dodoma haitaifikia hata mama Kila siku yupo Dar.
Mkoa wa pwani ulitokea wapi mpaka ukawa na viwanda? Kuna tatizo sehemu .

Viwanda vingi viko Pwani , Arusha
 
Swali fikirishi je ni mkoa gani Tanzania ambao una watu wengi zaidi ukipata jibu mimi kama mfanya biashara nitawekeza huko
Kama shida Yako ni kuwa na watu wengi kama hoja kuu namba 1 basi haupo,watu wengi wako Dar.

Sababu za watu wengi kujazana Dar nimeshazieleza kwenye hoja hapo Juu.

Ndio athari hiyo ya kuendeleza sera za kikoloni badala ya sera za kiuchumi za mjumuisho.
 
Back
Top Bottom