Miaka Zaidi ya 60 Baada ya Uhuru,Tanzania Imeshindwa Kuondoa Mizizi ya Ukoloni Kwa Nchi kuwa tegemezi wa Uchumi na Mapato Kwa Jiji Moja tuu la Dar

Hii sio hoja yangu ya msingi Wala Haina impacts yeyote Kwa hoja yangu.

Kinachotakiwa ni Serikali kujenga Majiji mengine Kwenye Kila Kanda.
Sasa ndio mtoe bil 34 ili kuongeza majengo Dodoma , tunataka kila mkoa uwe na hall za mikutano ..Tusikie mwaka huu mkutano mkubwa wa wakuu wa taasisi umefanyika iringa, Manyara , singida , mbeya sio kila siku Arusha tu na Dar .
 
Hili la kurudi Sina hakika nalo na Kwa jinsi sheria ilivyowekwa haiwezekani kurudi Dar
Sasa kama rais muda wote yeye Yuko Dar unategemea nini? Kwa mwaka siku 365, Samia anakaa Dodoma siku zisizozidi 60, siku 300 yuko Dar.

Taasisi nyingi za serikali bado zina ofisi Dar, nyingi zimehamia Dodoma kisiasa, unakuta mkurugenzi tu ndio ana ofisi Dodoma huku operation wote wako Dar. Hata gharama za uendeshaji wa serikali umekua wa gharama sana kwa sababu watu siku zote wako intransit, Dodoma, Dar.

Ni changamoto sana.
 
Asilimia 90% jmeitoa wapi? Huo ni uongo Dar inachangia asilimia 70% ya makusanyo ila in GPD ya asilimia 17% tu ya nchi nzima!
Kwa maana hiyo bila mikoa mingine Dar pia haipo!
Kikubwa serkali ijaribu kubalance tu maendeleo kwa mikoa yote hasa center kuu za kanda zote!
 
Unaweza kuuliza hata kuhamia huko Dodoma kuna mantiki ipi ? Vikao kila siku wanakaa Arusha na Dar ....Wangeacha tu kupeleka majengo mengi huko ...kila wizara ikae kikanda sio lazima zote zikae Dodoma maana mambo ni yale yale ya kwenda Nje ya mkoa kufanya semina.


Unaweka vip TPA makao makuu yakae Dodoma , mbona wizara ya utalii ina jengo kule Arusha? Wekeni hata wizara ya uvuvi pale kanda ya ziwa ....wizara ya kilimo kule Mbeya ..Mmbo ya Anga wekeni hata pale kilimanjaro .
 
Maajabu ya wanasiasa wa Kitanzania utasikia wanasema watu wasijazane mijini hasa Dar ilihali wanachokipitisha wao Bungeni kwa makofi ya meaning ndicho kinachopelekea.
 
Siku zote nimekua najiuliza why wizara ya kilimo iwe Dar wakati kilimo kinafanyika Mbeya, Iringa, Katavi, Rukwa, Ruvuma na mikoa mingine?

Wizara ya Madini ikae Dar wakati uchimbaji uko kanda ya ziwa? Wizara ya Ulinzi inafanya nini Dar. Mifuko ya hifadhi za jamii inafanya nini Dar. Concentration ya taasisi na idara za serikali sehemu moja ndio inaleta huu ujinga.
 
Upigaji mtupu , huo mji wa Dodoma wanataka wawekeze huko wafanye biashra , maisha yatakuwa juu ....
 
Shida ni kwamba,Alietufikisha hapa kwenye utegemezi huu. Uchumi mbivu ndio anatengeneza barabara ya 2050😂😂
 
Mimi habari ya Nyerere iliyonisikitisha sana ni ile ya yeye kubomoa mifumo ya uongozi ya vyama vya ushirika na serikali za mitaa ili kuua autonomy ya taasisi hizo kwa vile zilikuwa na nguvu sana; zilikuwa zikipambana na serikali kuu kuzuia kuingiliwa kwa madaraka yao kiholela.

Alipoziunda upya alihakikisha maCEO wote na top management zinakuwa na makada wanaowajibika kwanza kwa Rais na mwenyekiti wa CCM. Ndipo wimbi la kutowajibika, wizi, rushwa, undugunaizesheni lilipokithiri kwenye vyama vya ushirika na serikali za mitaa kupoteza kabisa relevance kwenye maeneo yao.

Management hazijali kabisa maslahi ya wanachama wala wakazi wa maeneo taasisi hizo zilipo bali zinatetemekea viongozi wa CCM hasa walioko Dodoma na Lumumba! Progress itoke wapi?
 
Mleta mada waweza kuwa na hoja lakini kulaumu serikali sio sahihi
Mfano wajenzi wa jiji la Dar es salaam City ni wafanyabiashara binafsi

Majengo yote makubwa ya biashara unayoaona Dar asilimia kubwa waliojenga ni wahindi na waarabu walioanzisha makazi yao na biashara Dar

Serikali haijengi miji wala vijiji wananchi wenyewe kwa shughuli za kiuchumi ndio hujengq miji ndio unakuta jiji kama kahama au mji wa Geita limeibuka sababu hiyo
Mji huibuka kwa kuanzia ni kuwa trade centre ndivyo hata majiji yote duniani yaliibuka hivyo yawe London, Paris,nk haikujengwa na serikali kuwa majiji
 
Raia wanajazana Dar mpk mji unakua unanuka jasho

Watawanye rasilimali sawa kikanda,sio kila kitu kinawekwa Dar
 
Hebu jiulize kiwanda kama General tyre cha Arusha mpaka Leo Kipo pale kama gofu.unajiuliza ni nini kinazuia kukifufua na matairi ni biashara ya uhakika na mpira tunauwezo wa kulima.Yaani ni kama kuna li mzimu mkubwa umesimama mbele yeti unasema "Bakia hapohapo"
 
Changamoto hatuna mipango na dira ya Taifa,,fedha nyingi za nchi hii zinaliwa na viongozi wa kisiasa,,,
 
Unadhani wafanyabiashara walijenga Jiji la Dar Kwa bahati mbaya? Jibu ni hapana ni Kwa sababu Serikali imeweka incentives zote hapo Dar,nani aende Mikoani ambako hakuna hizo incentives?

Hakuna Mji bila role ya serikali
 
Maabara ya Taifa ya Kilimo ziko Dar na Sasa Dom na taasisi zingine zinazofanana na hizo zinazojihusisha na Kilimo,uvuvi nk.

Upuuzi kama huu ndio msingi wa hoja yangu.Yaani hapa Tanzania tupo tupo tuu tunajiendea kama gari bovu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…