Miamba ya soka ya Africa, Al Ahly wanamfuatilia kwa karibu kocha wa muda wa Simba Sc, Mheshimiwa Juma Guardiola Mgunda ili waweze kuinasa saini yake

ToniXrated

JF-Expert Member
Joined
Sep 21, 2022
Posts
1,134
Reaction score
2,993
Amani iwe nanyi:

Nimepokea taarifa za kushtusha kutoka katika chanzo changu cha kuaminika nchini Misri ikieleza kuwa Rais wa klabu ya Al Ahly, Mahmoud Ibrahim Ibrahim El Khatib ni mfuatiliaji mkubwa wa mechi za Simba Sc na amekuwa akikoshwa na uchezaji wa timu ya Simba toka kocha Guardiola Mgunda kupewa jukumu la kuinoa Simba kwa muda mfupi.

Al Ahly wamekuwa na msimu mbaya kwa mwaka wa 2021/2022 mara baada ya kumaliza katika nafasi ya tatu katika msimamo wa ligi kuu ya misri na pia kumaliza kama mshindi wa pili katika ligi ya klabu bingwa Afrika.

Rais wa Al Ahly ana aamini kuwa Juma Mgunda pekee ndie anaweza kuirudishia makali Al Ahly kama alivyoirudishia makali Simba sc.
 
Anaitwa Juma Guardiola Mgunda?

Kama jina la kati sio lake basi tunafanya makosa sana kuutambulisha uwezo wa kocha wa Simba.
Majina humuwakilisha mtu na kile alicho nacho hutambulika kiurahisi kwa picha yake inayo tambulishwa kwa majina yake.

Juma Mgunda siyo msanii jamii ya akina Joti kiboga, Masanja,nk...

Mungu awe upande wake afike mbali kimafanikio
 
Hoja yako haina mashiko

Ameen kwa dua yako.
 
Wamisri wachukue ule mtumbo waupeleke wapi?
 
Kwani hapo shida nini mzee?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…