Michael Ballack ndiye mpiga mashuti bora kwenye mchezo wa soka

Tanzania kulikuwa na Mtu Akiitwa Fumo Felician zake ilikuwa anapiga mashuti mpira unaenda nyavuni hadi nyavu zinachanika... sijui ilikuwa Nyavu mbovu au ukali tu wa mashuti
 
Tanzania kulikuwa na Mtu Akiitwa Fumo Felician zake ilikuwa anapiga mashuti mpira unaenda nyavuni hadi nyavu zinachanika... sijui ilikuwa Nyavu mbovu au ukali tu wa mashuti
Kila weekend tunapiga nae pool table pale Kona ya Bwiru Mwanza. Huwa anatusimulia soka lao mpaka raha
 
Tangu nimeanza kushuhudia kabumbu miaka ya 1993 mpaka leo nadiriki kusema hakuna mcheza mpira aliyejaaliwa kupiga mashuti kama Michael Ballack. Mjerumani huyu hana mpinzani kabisa, je tunakubaliana wakuu kwa hili?
Patrick Berger, Ditiman Hamman, Tony Yeboh, Roberto Callos, Adrian Mutu, Jimy Floyd Hasenbank,Paulo Shule,Steve Raid,StiveGerald ao wanapiga Thunder Bolt sio vijishut vya akina Ballack.
 
siungi mkono hoja....
Roberto Carlos,
Wayne rooney,
Paul Scholes,
Frank Lampard,
Lukas Podolsk....
Hao watu ni habari nyingine..... Kuna na huyu Christiano Ronaldo pia.
 
INA MAANA MTOA MADA WEWE HUMJUI RAMADHAN SINGANO MESSI ? HUJAWAHI MSHUHUDIA ENZI ZAKE MASHUTI YAKE YALIVYOKUWA FIRE....
 
Yule alikipiga fainali ya 2002?.Alikuwa anabana nywele hivi?
weder Bremen hiyo ikiwa moto Sana jamaa ndo captain plus kina ozil enzi hizo....ilikiwa moto Sana mkuu. Shukrani kwa kumbukumbu nzuri hii
 
Tanzania kulikuwa na Mtu Akiitwa Fumo Felician zake ilikuwa anapiga mashuti mpira unaenda nyavuni hadi nyavu zinachanika... sijui ilikuwa Nyavu mbovu au ukali tu wa mashuti

Kajora Bhana
 
Peruzi kwenye kabrasha utagundua anayeshikilia rekodi ya kupiga shuti lenye 'spidi' kali ni Roberto Carlos, lakini kwa mtizamo wangu Ariel Batistuta(Bati goals) kwa yale mashuti yake yaliyokuwa mpaka yanatingisha besela hadi unaona kama goli linakaribia kung'oka ndiyo kiboko ya wote.
 
Tangu nimeanza kushuhudia kabumbu miaka ya 1993 mpaka leo nadiriki kusema hakuna mcheza mpira aliyejaaliwa kupiga mashuti kama Michael Ballack. Mjerumani huyu hana mpinzani kabisa, je tunakubaliana wakuu kwa hili?
Mi bana kwenye mashuti bado ni mfuasi mtiifu wa zile ngoma tatu pale England,
1) Paul Scholes,
2) Frank Lampard &
3) Stephen Gerald

Na kwa vile pia ni Mwana Msimbazi basi namuweka na Said Hamis Ndemla
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…