Michano/Hiphop/Freestyle

NINATOKA mimi, huwezi zama bila izini/
Ajira ni hasira kwa watu wachini, nchi haina dira haipandi juu bali inashuka chini
Mademu wanauza chini, vyeti vimewekwa kabatini/

Rais anawaza uchaguzi, wakati hospitali zimeishiwa wauguzi/
Serikari imegeuka pisikali, kila kona inapigiwa miruzi/

Natokea kitongoji cha panya rod, hakuna dini/mdudu analiwa mpaka maini na huwezi ukahoji/
 
.
 
Wakati mjuba nasaka fuba, kesho nisije juta/

Ndio muda Yuda, analia eti nimeweka nukta/

Kweli inakuja au hajachuja, kuwa hawezi furukuta/

Iwe kwa Uda au boti za Unguja, bado hawezi nikuta/

Kwenye tungo naonyesha ufanisi/

Nagonga nyundo uki test ku diss/

Vina Rundo mpaka utaanza kujihisi/

Kwamba Mvumbo rabda ni Taasisi/

Hip hop kwangu dawa, zaidi ya mzizi wa Mkungu/

Nikiisikia napagawa, ka' nimeona chupi nyekundu/
 
Do you hear me calling?, Jus pick it up say hello darling

Sina pakwenda nimekuwa kama mkimbizi, hupokei simu ndio sababu nakosa usingizi.../

Najiuliza nini kimekubadilisha siku hizi, au kuna mwanga kakufungia hirizi?.../

Tulipendana sana japo sikuwa na minoti, kama couple basi ni juice wrld na ally lotti.../
 
Respect for not rhyming basic
 
Alionyesha mapenzi, ya kweli na sio kufosi/
Alikataa wenye Mabenz, alikataa wadosi/
Aliniimbia kila tenzi, na kuni kiss utosi/
Hakuwa na ushenzi, japo sikuwa Boss/
Nimnunulie vitamu, ila alinipenda sana/
Amenijua Jamii Forum, akajua amepata bwana/
Kumbe tu nilikuwa na hamu, ya kutaka kuwezana/
Aliponipa utamu, nikahisi kama ananibana/
Nikaanza visa na mateso/ mixer nitakupigia kesho/ Tabitha hakuwa tena Special/ kichwa alitikisa na machozi kwenye leso/
Akajifunza kwenda, japo moyoni analia/
Hiyo nikaipenda, nipate wengine kuwatumia/
Sasa miaka imekata, kwa speed ya honda/
Kila dem nnaempata, anapenda pesa kama konda/
Uwe na za kula bata, ndio utaitwa nyonda/
Mapenzi ya kweli utata, kidume nakonda/
Nimemkumbuka mnyonge wangu/
Ila simu tena hakamati/
Jamani niachieni My wangu/
Mbona hata WhatsApp hachati/
JF namtumia Message zangu/
Lakini nako pia wala simpati/
Napata habari amepata mwenzangu/
Ana ndoa na jamaa wa Muscat/
Anapanda mwewe, kama baiskeli/
Nasikia mumewe, anamiliki Masheli/
Nimebug mwenyewe, hakika nimefeli/
Nipo hapa Ukerewe, nauza mastakafeli/
Nisaidie eeh Mungu, niepushe na majaribu/
Nawaza nichukue chungu, niende kuharibu/
 
Amri hawakutii walitaka kujiunga Nato/

Ghafla zikasikika R.P.G na vifaru vya kushato/

Kuonyesha ahofii Ukraine akajibu Battle/

Alijua atakuwa free Javelin hizo hapo/

Ambush kiwanda cha chuma nyani akatema bungo/

Warusi walisema hakuna kujikuna wala kurusha ungo/

Raia walitia huruma amani ilikuwa fumbo/

Mtaani zimekata huduma hakuna aliyefikiria tumbo/

Risasi na Maguruneti/ visasi na kutest/ wakaasi Mabest/ wasi wasi kwa Zelensky/

Madege yasiyo na rubani/ wakapandisha mlege wahisani/

Vikwazo kede himayani/ wese sio mbege ona shida duniani/

Kila kitu bei juu Nchi zote wanalia/

Uturuki wanapikia vifuu nini kwa Mama Samia/

US hakuna bei nafuu haitoshi Dollar mia/

Na wakisema suu inasukumwa Nyukilia/
 
Bongo fleva imepoteza flavour/
Wasanii hawana plan b, mistari wanaokoteza/
Sina shari bali huu ni ukweli nawaeleza/

Viongozi wengi waana macho makengeza/
hawaoni mbali wao wanachojali fedha/

Sina shari bali huu ni ukweli nawaeleza/
Bongo bila fedha unaweza zikwa bila jeneza/
 
Namshukuru mungu niko hai/
japo nimepitia machungu, ili baki nusu nipoteze uhai/
Nilizungukwa na madeni, kila kona wananidai/
most wanted kama sadam husseni nikapewa kesi za jinai/
 
Ni mistari ya kiutu uzima, watoto nendeni jandoni/

Wako wapi walio pima, nikitimba roho mkononi/

Wafuasi wanasimama wima, nikichana wanaagiza Pop corn/

Mitaa inanipa heshima, japo heshima ninayo mifukoni/

Wakisema najigamba, waambie ndio asili, ya huu utamaduni,

Ni msafara wa Mamba, sio Tumbiri, wala Mbuni/

So kushika namba, sio kubashiri, wala kurubuni/

Ni ubunifu sambamba, vina kuhimili, na kufuata kanuni/

Walipewa mapande, wakabana pua kama wamekabwa/

Leo hii game ipo upande, kama kofia ya Sheikh ubwabwa/
 
Naandika mistari migumu, kama Nakoz za kiduku/
Beat nazinyonga kama ndumu, utasema nina muku/
Ma Mc's nawahukumu, kama wamekwepa Luku/
Na Snitch akitema sumu, tunaulia Panya buku/
Wakati mna Bet, na kuishi kwa malawama/
Nipo juu zaidi ya Chief Fast Jet, Vasco Dagama/
Wajanja hatujazi chest, pesa ndiyo unyama/
Na tukikosa hata ya Guest, atalipa unae muita Baby mama/
Ujumbe sio pendekezo, watakuandikia wazazi/
Naonyesha tu mauwezo, kama mkuu wa kazi/
 
Bado nashusha Bars, wakati wana wana troti/
Amani kwa Scars, na Yuda Iskariot/
Na wote wanazi, wanao songesha hili Boat/
Baada ya kazi, hapa tunastua kama Joti/
Mistari unaweza kutupa, hakuna aliyesomea/
Ukiogopa kunyanyuka, hutaweza kutembea/
Huwezi jua, huenda ukawa Young Killer wa kesho/
Huwezi tambua, huenda ukawa na kitu special/
Hata ukibana pua, bora ufanye Commercial/
Hivyo acha kusua sua, kama chui wa maonyesho/
Mvumbo asikutishe, kwa mistari konde/
Bali ikufundishe, mbinu usiwe kinyonge/
Popote usababishe, mpaka wakupe kombe/
Usiwe chawa kama Aristote, kwa hela ya pombe/
 
Nafumua ubongo, kama nina kinu cha ballistic/
Waliodhani uongo, leo wanasema nimepanic/
Marapa wa michongo, natembeza tu stick/
Nina madini kama Congo, kwenye kichwa hiki/
M.V.U.M.B.O nazielewa herufi hizi sita/

M - mshindi uwanja wa vita/

V - vumilia na kisha wajibika/

U - usife moyo hata usipo heshimika/

M - Mungu yupo nawe kila dakika/

B - Bora peke yako kuliko ushirika/

O - Okoa Hip Hop hakikisha ina sikika

Ndio maana naendeleza kasumba/ hawawezi hili rumba/
Leo chatu kaliwa na mbwa/ Demu kahonga mavumba/
Mpangaji kamfukuza mwenye nyumba/
Tozi kavaa za mtumba/ kiongozi kacheza akadumba/
Ooh! Naweza chana mpaka majogoo, maana vina vinajiseti/
Hawawezi toa droo, hata Melo akiweka visenti/ [emoji2][emoji2]
 
Uko vizuri shitua kama zakina busta rhymes
 
Bado nasonga, kinara nakonga, kama Bingo/
Nanyonga, wenye mikwara ya Mandonga, kwenye ulingo/
Navunja nyonga, hata ukihonga, ujue natembeza mpingo/
Haina kuchonga, haina kubonga, kama katuni za Kingo/
Nipo hapa kufunza hii kitu/ ni Paka ninaechapa mpaka Mbwa Mwitu/
Tunazisaka hata kwenye misitu/
Na tukizipata hatuna shanapa kama hakijatokea kitu/
Tofauti na madogo, wakibadili chupi ni zogo/
Akili fupi akili ndogo, wakulungwa tumenyuti kama fogo/




Sent from my SM-G532F using JamiiForums mobile app
 
Kuna muda natamani, tuishi kama zamani../
ila sijui mkuda gani, alievuruga amani/
Amani ya ndoa haipatikani, kila kitu ananikosoa hata uwe utani/
Sioni tena raha ya kukaa nyumbani, yaani bora uishi vitani kuliko ndoa isio na amani../
 
Naweza flow bila hata mdundo, na kwenye show wakaja watu lundo/
wasanii hawana plan b wanafata mkumbo,matusi kila tungo/kiki kwao ndio mchongo
Muziki umekosa uhondo/

Me ni mkali wa mistari, si uwongo/
waniniita israel mtoa roho, japo sometime natema nyongo/
Mc wenu wana nguvu ya gongo, hata muwa-push vp, hawafiki kama gari ya udongo/
 
Kuna muda natamani, tuishi kama zamani../
ila sijui mkuda gani, alievuruga amani/
Amani ya ndoa haipatikani, kila kitu ananikosoa hata uwe utani/
Sioni tena raha ya kukaa nyumbani, yaani bora uishi vitani kuliko ndoa isio na amani../
Upendo umefika mwisho, wapendanao wanajinyonga/

Wengine ni vitisho, kama mikwara ya Mandonga/

Hakuna upatanisho, kila mmoja anachonga/

Kifo ndio hitimisho, hata kama alikukonga/

Unaempenda hakupendi kama uteja wa unga/

Usiye mpenda haendi kama kamba umemfunga/

Dharau haijengi siyo tofari la nyumba/

Mapenzi yana mengi bwana mdogo chunga/

Mnunulie simu wenzako wampe vocha/

Jifanye mwalimu ajifanye kocha/

Mpe za kujikimu akakufanye ndondocha/

Yanakata stimu mapenzi ulofa/

Hiyo bastola unayonunua, haitaua kabisa vibaka/

Bali mwenyewe utajiua, utakapokuta mkeo wamempakata/

Wachache wana mapenzi ila tenzi kuwapata/ hauwezi bila Mwenyezi utadata/ kindezi kisa penzi atakukamata/

Kwa mwenye Benz atakuacha/ hauna malezi linavuja pakacha/ hata uwe mbezi na pesa ya kutakata/ bado utafanyiwa ushenzi kwa muuza kashata/

Ule muda unasaka mahitaji, ili Family njaa isijelala/

Wife yupo kifuani kwa mshikaji, huku akikuita fala/

Mapenzi hayana Falsafa, hata uwe umesoma sana/

Mapenzi yanaleta maafa, sio Tarime mpaka Tanga wanauwana/
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…